Odhiambo cairo
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 15,989
- 22,078
Aiseeh !!.Mh Mbowe alishupaza sauti kwa kujifanya yupo siriasi kwa kuwaonyesha wafuasi wake watiifu kuwa anayasema maneno yale mbele ya raisi ana uchungu mwingi ilihali anajua jambo lile lina baraka zao na wale wapo pale mpaka wamalize muda wao,
Kutaka kucheza na akili zao na kweli amefanikiwa kwa lengo lake wengi wao wameamini Mbowe hataki covid19 wawepo pale wakati yeye na baadhi ya viongozi ni wanufaika wa wale wanawake kuwepo bungeni.
Lissu hakukosea aliposema mwenyekiti amelamba asali,jibu limepatikana Mbowe hana lawama tena amejivua kiakili kwa kuonyesha kuwa ahusiki ila kwa kuwa anaongoza waliolala milele wamebaki kushangalia hutuba yake ya kimkakati.
Kiufupi Halima's mdee and gangs wameshinda vita kiurahisi na leo hii wanawasiliana na mwenyekiti kupongezana,
Wenye uchungu nendeni mkaiombe mahakama!
Naungana na lissu mwenyekiti kalamba buyu la asali!
Huna akili hivyo ?! Kwahiyo siku hizi Rais wetu ni wa kuambiwa udanganyifu na blah blah tu ! Atakuwa ni Rais wa makatuni au !!.
Mnataka Cdm ifanye nini ?. Kama ni vikao vya kikatiba kuhusu jambo hili. Vimefanyika na maamuzi yakatoka hadharani. Kwamba wamefukuzwa uanachama na asubuhi yake wakapereka barua kwa dispatch bungeni ya kutowatambua. Sasa unataka nini ?
Mahakama na Tulia kuendelea kuwang'ang'ania ni shauri yao. Siyo tena swala la Mbowe