Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Habarin wana jf.
Sote tunafahamu kua kilimo ndio uti wa mgongo wa watanzania kwa sababu kimeajiri watu wengi.

Serikali ya Mh kikwete ilianzisha utaratibu wa ruzuku za pembejeo ili kuhakikisha upatikanaji wake uwe rahisi na kuchochea uzalishaji wa chakula, na mazao mengine ya nafaka.lkn utawala wa awamu ya tano uliacha kutoa ruzuku hizo kwa kisingizio kua, kuna uendeshwaji mbovu wa ruzuku hizo.

Kutokana na hali ya sasa ya maisha, inakua ni vigumu sana kwa mkulima kumudu kununua pembejeo(mbolea) kwa sababu ya gharama yake kubwa.

Naomba serikali sikivu ya mheshimiwa rais samia, ianzishe upya ruzuku Hizi na iweke usimamizi madhubuti ili kuendesha ruzuku hizo kwani kufanya hivyo si tu kutachangia uwepo wa usalama wa chakula kwa kila kaya, bali pia kutatoa fursa za ajira na kukuza uchumi wa taifa.

Sent from my TECNO W4 using JamiiForums mobile app
 
Allah akuongoze Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan katika kila la kheri na akuepushe katika kila la shari wewe na viongozi wezako wa Tanzania katika kuiongoza Tanzania Inshaallah.
 
Mm nimpongeze mama yetu samia Suluhu Hassan, kiukweli saiv tunaona mabadiliko makubwa kivitendo, Enzi za mwenda zake haya mambo yalikera mno,alipenda sifa kupitiliza, na wateule wake walimjua, kila mmoja wao akawa anapigania kuwa front page ya kumpamba!, kila chombo cha habari taarifa ni zake tu!

Hili swala mama Ameliona ni vyema sasa wateuliwa wajifunze kwamba hizi sio zama za mwendazake, waache masiara kazini!!! Na sifa za kijinga!!
 
Mwenye macho hambiwi tazama.

Juhudi za Amiri Jeshi Mkuu, Rais wetu Mpendwa Mama Samia zinaonyesha matumaini makubwa kwa Nchi yetu kupiga hatua kubwa ya kiuchumi ktk siku za mbeleni.

Kwa sasa Tanzania sio kisiwa tena, tumeshatoka ndani ya boksi, tujiandae kuchangamkia fursa lukuki.

Mimi sio msomi wa uchumi wala chochote, ni mkulima tu lakini naona jinsi unavyofungua kufuli, milango ya fursa sasa imefunguka na inaendelea kufunguliwa.

Ahsante sana Rais wetu Mama Samia, naaamini ndani ya kipindi kifupi Tanzania itapaaaaaaaaaaaaaa mawinguni juuuuuuuuuu.

Watanzania wote wanamatumaini makubwa sana. Wakulima sasa tulime kwa bidii, wafanyabiashara aina zote sasa tufanye kwa bidii na ubunifu, sekta zote sasa tuanze kukimbia tusilale wala kutembea.

Mungu mlinde Rais wetu.
 
Sasa ndio tumepata Kiongozi baada ya Mtawala na Mijeledi yake kwenda zake ghafla.

Fungua Nchi kipenzi chetu Mama, Watoto wako wapate Ajira, kama ilivyokuwa kwenye Awamu ya Nne Ajira zilikuwa za kumwaga shukurani ziende kwa Mzee Kikwete.
 
Sasa ndio tumepata Kiongozi baada ya Mtawala na Mijeledi yake kwenda zake ghafla.

Fungua Nchi kipenzi chetu Mama,Watoto wako wapate Ajira,kama ilivyokuwa kwenye Awamu ya Nne Ajira zilikuwa za kumwaga shukurani ziende kwa Mzee Kikwete.
Tuna Imani kubwa kwake
 
Tuna Imani kubwa kwake
Ametia mkono Pipeline Tanga Hoima inaanza hapo Ajira za kumwaga, ametia mkono Pipeline ya Gesi kwenda Kenya inaanza hapo Ajira bwelelee amesema Wawekezaji rukhsa

Ndani ya Ngwe ya Samia naona kabisa ajira zikizalishwa kwa kiwango.

Njaa njaa hizi za mitaani zitapungua.
 
Sasa ndio tumepata Kiongozi baada ya Mtawala na Mijeledi yake kwenda zake ghafla.

Fungua Nchi kipenzi chetu Mama,Watoto wako wapate Ajira,kama ilivyokuwa kwenye Awamu ya Nne Ajira zilikuwa za kumwaga shukurani ziende kwa Mzee Kikwete.
CCM daima, CHADEMA watasubiri sana hapo Ufipa
 
Nianze kwa kumpa Mama yetu mpendwa pongezi za dhati kabisa
Pongezi hizi ni kwa namna anavyojaribu kuwaonjesha watu tofaouti tofauti utamu wa keki ya taifa na pia wengine wa'feel some pain kwa jinsi ilivyowaponyoka kirahisi mfano mzuri Chalamila na wengine kama hao, hii inaleta sura nzuri kwenye mzunguuko wa kugombania ajira
 
Hapo kuna ajira gani ya kugombaniwa?

Hizo za kuteuliwa au zipi Chief?
 
Mama, asilimia kubwa ya chakula cha mmea utafutwa na mizizi. Mti ukiwa na mizizi dhaifu hukosa ustawi na kupelekea kutoa zao dhaifu.

Vivyo ivyo kwa uwongozi wa nchi; kama ubora wa viongozi wa chini ni mdogo, utendaji wa kiongozi wa juu (Rais) na usitawi wake huwa dhaifu.

Bila shaka tunatambuwa hali ilivyokuwa maofisini mwetu, teuzi za wakuu wa idara/Taasisi/vitengo ulivyofanyika. Sehemu kubwa haukuzingatia weledi wa mteuliwa katika kutimiza majukumu yake kisheria.

Hata hapakuangaliwa historia ya mahusiano ya mteuliwa na watumishi kazini. Ni Kamavile UTUMISHI walikuwa wanapelekewa majina ya watu na kulazimishwa kuwaandikia barua ya uteuzi.

Kuna wakuu wa Idara wao ndo kila kitu (mhasibu, mkaguzi wa ndani, afisa mipango, Mtawala n.k).

Kuna wale wanaofanya Kitengo/Taasisi/Idara kama mali ya familia/kabila/mkoa/Kanda. Hawa ni wengi mnoo na pasipochukuliwa hatua mahususi, hali itakuwa sio hali.

Hali hiyo inapelekea kutengwa baadhi ya wafanyakazi na kusingiziwa mengi, matumizi mabaya ya fedha zinazo wanufaisha wachache sehemu husika na kutokuwa na ustawi sehemu ya kazi.

Pia, hali hii ya kubebana inapelekea watu kufanya kazi nje ya taaluma zao na kuharibu kazi

Mama, angalia haya katika Mawizara yetu kama TAMISEMI,NISHATI, AFYA nk, Taasisi zetu kama TANESCO REA, TANROADS n.k.
Naomba Mwenyezimungu akulinde na akuongoze.
 
Kweli kabisa. Mwendazake alikuwa anapachika watu kwenye mashirika, idara na vitengo kwa mihemko.
 
Back
Top Bottom