Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Hukumuelewa.ndio tatizo la "kusomea barua m' bahasha".(msemo wa kiswahil unaomaanisha kutoa maelezo ilihali huna uhakika.
Kasema RC ni hadhi ya Juu uwe mwajibikaj sio kuunda syndicate na kuanza kupiga maji.Rc hana rafiki ili uweze ku exercise mamlaka.
Unajua maana ya syndicate?

Pia kuna shida gani mtu akinywa na marafiki zake nje ya muda wa kazi?
 
Taarifa za watu kuchoma nyama? kama TISS wanampelekea Rais taarifa za namna iyo basi nao wanatakiwa kufanyiwa reformation kama polisi!

Mambo ya watu kuchoma nyama na kunywa kama marafiki tena wakiwa kwenye faragha zao yana faida gani kwa taifa kwenye dunia ya leo?
Uongozi ni dhamana na inatakiwa kuwatendea wote unaowaongoza sawa. Imezuka tabia ya baadhi ya watu kujipenyeza kwa viongozi na kujenga urafiki kwa maslahi yao binafsi.
Mama ameonya na anajua anachosema. Kama mtu unataka kuwa private, usifanye kazi kwenye ofisi za umma. Rais anajua fika wapi watu wanatengeneza mauzauza tunayoyaona...ni katika hizo nyama choma na party za marafiki
 
Uongozi ni dhamana na inatakiwa kuwatendea wote unaowaongoza sawa. Imezuka tabia ya baadhi ya watu kujipenyeza kwa viongozi na kujenga urafiki kwa maslahi yao binafsi.
Mama ameonya na anajua anachosema. Kama mtu unataka kuwa private, usifanye kazi kwenye ofisi za umma. Rais anajua fika wapi watu wanatengeneza mauzauza tunayoyaona...ni katika hizo nyama choma na party za marafiki
Wapi duniani viongozi hawaruhusiwi kuwa na marafiki?

Wewe hauna marafiki? Hao viongozi unaotaka wasiwe na marafiki ni binadamu kama sisi au wameshushwa special kutoka mbinguni?

Kuna namna unaweza tengeneza mfumo mzuri tu wa kuzuia conflicts of interest kwa viongozi na marafiki zao

Mfano kwa Uingereza - Kiongozi wa umma kama ameitwa kwenye kikao cha biashara na mfanyabiashara ni lazima a declare kikao hicho na mahala kinapofanyika kwa ethics Committee

Unaweza kuweka mifumo mizuri na mambo yakaenda vizuri tu sio kuwakataza watu kuchoma nyama na kunywa mvinyo

Nyerere alivyoweka Leaders clubs kwa ajili ya viongozi na Officers mess hakuwaga na akili au?
 
Uongozi ni dhamana na inatakiwa kuwatendea wote unaowaongoza sawa. Imezuka tabia ya baadhi ya watu kujipenyeza kwa viongozi na kujenga urafiki kwa maslahi yao binafsi.
Mama ameonya na anajua anachosema. Kama mtu unataka kuwa private, usifanye kazi kwenye ofisi za umma. Rais anajua fika wapi watu wanatengeneza mauzauza tunayoyaona...ni katika hizo nyama choma na party za marafiki
Naungana na raisi lakini ni ngumu kuzuia hilo na haiwezekani.
Amos makalla akiwa na birthday ya mwanae ni lazima atachoma nyama na kuwaalika rafiki zake.
 
Wapi duniani viongozi hawaruhusiwi kuwa na marafiki?

Wewe hauna marafiki? Hao viongozi unaotaka wasiwe na marafiki ni binadamu kama sisi au wameshushwa special kutoka mbinguni?
Naungana na raisi, lakini hili la party haliwezekani. Mkuu wa mkoa ana ndugu na jamaa, akialikwa kwenye sherehe ni lazima atahudhuria na akihudhuria lazima atakua karibu na ndugu na marafiki zake
 
Naungana na raisi, lakini hili la party haliwezekani. Mkuu wa mkoa ana ndugu na jamaa, akialikwa kwenye sherehe ni lazima atahudhuria na akihudhuria lazima atakua karibu na ndugu na marafiki zake
Mambo ya kishamba tu

How comes unanizuia kuchoma nyama hata nyumbani kwangu na kualika marafiki zangu? Huu utakuwa ushamba na utumwa
 
Jana nimemsikia Rais Samia kwenye hotuba yake wakati wa kuapisha viongozi aliowateua

Pamoja na kuunga mkono sehemu kubwa ya hotuba yake ila Rais wangu aliniangusha pale alipozungumzia kuhusu watu kuchoma nyama na kunywa kama marafiki

Rais Samia kama mtu ninayekwambia na kukushauri ukweli, napenda kukushauri leo, achana na hayo mambo binafsi ya watu

Hata vitabu vitakatifu vinasema kuhusu kupendana kama ndugu. Mambo ya watu kukutana kama marafiki/ ndugu na kuamua kuchoma nyama huku wakifurahi na kubadilishana mawazo ni mambo binafsi sana na nakuomba usijihusishe na mambo binafsi ya watu maana utakuwa unarudia kosa la mtangulizi wako ambapo alifikia hadi hatua ya kuanza kufuatilia mawasiliano binafsi ya wateule wake.

Rais Samia, napenda kukuhusia kwenye teuzi zako angalia weredi wa mtu, uwezo wake kiakili na kikazi, uzalendo wake na uaminifu wake kwa Taifa na wananchi!

Mambo ya kuangalia kama watu wanakutana kuchoma nyama na kula hayo ni mambo ya kishamba sana na hayana nafasi kwenye dunia ya sasa na hata kwenye vitabu vyetu vya dini. Kwa Wakristo Bwana Yesu alishawai kugeuza maji kuwa divai kwenye shughuli fulani ili watu wanywe na kufurahi.

Kama kuna mshauri wako anakushauri uangalie huo ujinga basi mkaripie maana hakuna binadamu asiye na mambo yake binafsi na ndo mana hata Serikali yetu iliwekaga Leaders clubs kwa ajili ya viongozi kupata nafasi za kupumzika na kubadilishana mawazo

Kwa leo naomba niishie hapa!
We mfuasi wa jiwe Huo ushauri peleka chato
 
Moderators tendeni haki please! huu uzi unajitegemea na haustahili kuunganishwa na uzi mkuu wa maoni na ushauri
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzania haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli kafa, lakini spirit yake haijafa. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu, katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli kafa lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, na kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli haijafa. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60, kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Anaweka vizee vya kipemba huku bara kwa kuviteua wakati havina uwezo wowote. Jana kakiapisha kizee fulani kipemba eti ilikua karibu atemwe ndio kampa uteuzi. Halafu anajidai hana upendeleo anafuata uwezo...shwain. eti tumsamehe, wala hatumsamehi tunasubiri 2025 kumtema kama bigjee.
 
Mtapata taabu saana maana Mama Samia is the 'iron lady'! Ukiingia anga zake tu kuvuruga serikali iliyoyaanzisha chini ya JPM, ambayo yy naye alikuwa sehemu ya serikali hiyo lazima apite na weye!

Hamtaamini huyu mama atakavyokuwa zaidi ya Magufuli kwa kutokucheka na nyani! Mama Samia atapandisha viwango vya uongozi kiasi kwamba tutatamani aendelee kutawala kwa muda mrefu!

Nafasi ya mwanamke kuchukua madaraka makubwa inaenda kuhakikishwa kwa utendani bora wa Mama Samia! Wezi mmeula wa chuya! Hamna chenu hapa!
Soma Biblia Mwanzo 2:18, 21-23
 
Mama taarifa kaipata hapa, tusubiri nini kitafuata!
 

Attachments

  • _20220802_122026.JPG
    _20220802_122026.JPG
    228.1 KB · Views: 18
Wapi duniani viongozi hawaruhusiwi kuwa na marafiki?

Wewe hauna marafiki? Hao viongozi unaotaka wasiwe na marafiki ni binadamu kama sisi au wameshushwa special kutoka mbinguni?

Kuna namna unaweza tengeneza mfumo mzuri tu wa kuzuia conflicts of interest kwa viongozi na marafiki zao

Mfano kwa Uingereza - Kiongozi wa umma kama ameitwa kwenye kikao cha biashara na mfanyabiashara ni lazima a declare kikao hicho na mahala kinapofanyika kwa ethics Committee

Unaweza kuweka mifumo mizuri na mambo yakaenda vizuri tu sio kuwakataza watu kuchoma nyama na kunywa mvinyo

Nyerere alivyoweka Leaders clubs kwa ajili ya viongozi na Officers mess hakuwaga na akili au?
Nani kasema viongozi wanakatazwa kuwa na marafiki? Hizo nyama choma na kula bata, halafu kugawiana deal ndio urafiki?
Unafikiri walioondoshwa wameonewa? Ukiona mtu kwenye TV anavyogombeza watu unaweza kufikiri kuna kitu serious...kumbe ntu wa deal.
Urafiki wetu mwingi kwenye siasa za bongo hauna afya kwa jamii iliyo kubwa. Umejaa kujenga mazingira ya kula kwa nafasi tu
 
Naungana na raisi lakini ni ngumu kuzuia hilo na haiwezekani.
Amos makalla akiwa na birthday ya mwanae ni lazima atachoma nyama na kuwaalika rafiki zake.
Ni ngumu mno. Unajua sababu ya ugumu wa kutekeleza sheria za maadili ya uongozi wa umma, kuna wengi wanaotumia hizo fursa kufanya mambo mengine yasiyo na tija kwa Taifa letu
 
Nani kasema viongozi wanakatazwa kuwa na marafiki? Hizo nyama choma na kula bata, halafu kugawiana deal ndio urafiki?
Unafikiri walioondoshwa wameonewa? Ukiona mtu kwenye TV anavyogombeza watu unaweza kufikiri kuna kitu serious...kumbe ntu wa deal.
Urafiki wetu mwingi kwenye siasa za bongo hauna afya kwa jamii iliyo kubwa. Umejaa kujenga mazingira ya kula kwa nafasi tu
Uwe unasoma comment nzima

Nimesema hapo juu namna ya kurekebisha hilo kimfumo na sio kukataza watu kuchoma nyama na kunywa mvinyo
 
Teuzi mh:Raisi zifanyike hata kwa wakulima pia hililinafya,maana ukiteua mkulima ukampeleka sehemu wanazolima mfano.Mapachichi,Mahindi nk,kwa uzoefu wake na shamba darasa tuapata mazao mengi vilevile na mapato ya sehemu husika na Taifa kwa ujumla yataongezeka.Pia hata kwa wafugaji na wafanyabiashara.Ahsante,Jamhuri ya muungano wa Tanzania, kazi iendelee.
 
Back
Top Bottom