Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Hata mfanye nini,hamuwezi kumuondoa samia,kutunga uongo dhidi yake,haiwezi kuwa njia ya kumuondoa,badala yake ndio mnazidi kumuimarisha
 
E
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzania haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli amefariki, lakini spirit yake inaishi. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi, iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli amefariki lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana, usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili, lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli inaishi. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60 kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Endeleeni kumdanganya mama yetu.
 
Salaam,

Nimeshuhdia karibu awamu zote za uongozi wa taifa hili, mpaka sasa rais samia ameonekana bora kuliko watangulizi wake kwa sababu hizi;

1. USTAWI WA DEMOKRASIA
ktk historia ya taifa haujawahi shuhudiwa ustawi wa demokrasia kama ulivyo awamu hii.

Wapinzani wamefanya maandamano na mikutano ktk mikoa tofauti bila bughudha jambo ambalo kabla halikuwahi tokea.

Maandamano pekee yalozuiwa ni ya juzi yalokua na ajenda za kihalifu.


2. MAHUSIANO YA KIMATAIFA
Ktk historia ya taifa letu hakuna wakati tumewahi kua na mahusiano bora na imara ya kimataifa kama wakati huu, ndio maana tunashuhudia misaada na mikopo ikimiminika daily.

3. AJENDA YA MARIDHIANO
Baada ya kupata madaraka, alileta ajenda ya maridhiano ambayo kwa bahati mbaya imehujumiwa na wasiomtakia mema

4. UTAWALA WA SHERIA
Rais samia anaheshimu utawala wa sheria ndo maana huwezi muona akitumia mabavu kuonea wengine.

5.UTEKELEZAJI MIRADI
Ktk historia yetu hakuna rais amewahi tekeleza miradi ya gharama kubwa kuliko samia.

MUNGU MBARIKI MAMA.
 
E

Endeleeni kumdanganya mama yetu.
Mama imemchukua muda mrefu sana kujua kuwa kuna namna moja sahihi ya kuongoza nchi hii kupiga hatua za kimaendeleo kwa kasi. Nayo ni namna ya JPM. Hata hivyo bado hajampatia sawasawa
 
Maoni, ushauri kwa Mama yetu kipenzi Rais wa JMT ambaye ndio mwenye serikali na mwenye mamlaka ya kutoa agizo lolote : kilio walioajiriwa 2014 kudai kupandishwa vyeo kama ilivyostahiki hakijasikilizwa, ni hivi 👉kufikia 2018 walipaswa kupanda vyeo kwa mara ya kwanza, kufikia 2021 walipaswa kuwa kwenye cheo cha pili, kufikia 2024 walipaswa kuwa kwenye cheo cha tatu, lakini ilivyo ni kuwa wapo kwenye cheo cha pili badala ya cheo cha tatu.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Napenda tu mfahamu ya kuwa Mkuu wa Nchi au waweza kusema Rais wa Nchi anaweza kuwafanya wananchi na Taifa kwa ujumla kuwa na Furaha,amani na utulivu mioyoni Mwao.anaweza kuwafanya watu wakaishi pasipo hofu wala wasiwasi wala mawazo ya huzuni au Msongo wa Mawazo.

Matendo ya Rais ,kauli za Rais,sera za Rais,matamko ya Rais ni vitu vinavyoweza kuchochea hayo niliyoyaeleza hapo juu. Ni kauli za Rais zinaweza kujenga umoja wa kitaifa, mshikamano, upendo miongoni mwa wananchi na kwa upande Mwingine ni kauli hizohizo Za Rais zinaweza kuchochea na kujenga hali ya uhasama ,ubaguzi ,mpasuko katika Taifa,kuvunja umoja wa kitaifa na hata kujenga chuki katika mioyo ya watu.

Ni matendo ya Rais Pia yanaweza chochea umoja na mshikamano pamoja na imani ya wananchi kwa serikali yao ,taasisi za serikali na ofisi za umma.na ni matendo ya Rais yanaweza ondoa imani ya wananchi kwa serikali yao,taasisi zao na hata ofisi za umma pamoja na kuwa na chuki nazo.

Lakini pia sera za Rais zinaweza inua matumaini ya watu au kuwakatisha tamaa.zinaweza fanikisha ndoto za watu au kuzima ndoto za watu.ndio maana wengine hufikia hatua ya kutamani kiongozi fulani na utawala wake upite haraka ili wapate kupumua na kupata matumaini kiuchumi.ndio sababu wengine hupata sauti ya kumpinga kiongozi fulani na kumtaka ajiuzuru kwa sababu ya kukosa matumaini chini ya utawala wake.

Ukiangalia tangia kuingia madarakani kwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan unaona namna alivyoinua matumaini ya watu,imani ya watu kwa serikali yao,kujenga umoja wa kitaifa, mshikamano na upendo miongoni mwa wananchi.amaeleta nuru na mwanga kwa maisha ya wengi,amechochea matumaini ya wengi kutimiza ndoto zao na kufikia malengo yao.

Rais Samia amewafanya Watanzania kuwa wenye furaha kutokana na kauli zake zenye kuhimiza umoja na mshikamano,kuhimiza na kutenda haki kwa vyombo vyote vya utoaji haki. Sera zake kiuchumi zimekuwa zenye kuleta matumaini makubwa sana.ndio sababu kila siku mitaani biashara mpya zinafunguliwa na kuongezeka kwa kasi.

Watanzania Tuna kila sababu ya kumshukuru sana Rais Samia kwa uongozi wake huu wenye kugusa maisha ya watu na kumfikia kila mmoja kwa kadri ya mahitaji yake na kiu yake.tuna kila sababu ya kumpa miaka mingine mitano Ya Urais kwa kishindoo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.amani na furaha yetu vipo mikononi mwa Jemedari wetu Hodari Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.View attachment 3074324

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Anashikilia furaha yako kwa vile anakutupia makombo.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kwanza ningependa kuwakumbusheni kwa machache kati ya Mengi kuhusu mtu kuwa Rais. Ningependa kuwaambieni ya kuwa Mtu hawi Rais wala kukidhi vigezo vya Urais kwa kufanya tukio moja au kwa matukio yampito kama mvuke.

wala mtu hawi RAIS kwa kuongea sana maneno mdomoni pake bila mipaka, mpangilio,utaratibu na utulivu.

Urais unahitaji mtu mwenye utulivu wa akili,mwenye afya njema ya akili .mwenye uwezo wa kudhibiti na kutawala hisia zake, hasira zake, Mihemko yake, chuki zake, kinyongo chake na hata matamanio yake binafsi. Urais hauhitaji ujuaji.

Urais ni taasisi inayohitaji mtu mwenye historia ya kiutendaji iliyotukuka. unaweza kumbeba beba mtu kwa njia zote na kumuweka katika nafasi fulani lakini kamwe huwezi kumbeba beba na kumzoa zoa mtu kumuweka kwenye kiti cha Urais.

Kwa hakika ni lazima utalitikisa, kulitetemesha, kulipoteza, kulivuruga, kulisambaratisha, kulikwamisha na kuleta sintofahamu kwa Taifa ikiwa ni pamoja na kuhatarisha usalama na umoja wa kitaifa.unaweza kumpa mtu upendeleo wa kumpatia nafasi yoyote ile na hata akifanya makosa yasiwe na athari kwa Taifa lakini kamwe huwezi kumpa mtu Urais kwa majaribio na matamanio yako tu binafsi.

Urais siyo mahali pa kujifunzia kazi au kufanyia majaribio.Urais ni nafasi inayohitaji mtu aliyepevuka kiakili na kimwili,mtu anayejiheshimu,asiye na utoto utoto hata katika maandishi yake na maamuzi yake.Urais unahitaji mtu mwenye ngozi ngumu na mwenye uwezo wa kuogelea na kupiga mbizi katika Mawimbi ya kila aina na kulivusha Taifa.

Urais hauhitaji ushindi katika kila mjadala. Bali unahitaji maridhiano,subira, uvumilivu,usikivu kila panapotokea jambo lenye kugusa hisia za watu na mivutano.

Urais unahitaji mtu mwenye uwezo, akili ya kuongoza watu na kuwaleta pamoja licha ya tofauti zao za kisiasa, mitizamo,Imani na mengine Mengi. Urais unahitaji mtu mwenye uwezo wa kufikiri ndio kufanya maamuzi na siyo kufanya maamuzi au kutoa maneno au kauli na kisha kufikiria juu ya maamuzi au kauli au maneno yaliyokwisha kutolewa na kutoka kinywani kama Risasi.

Ukiangalia hayo machache niliyoyaeleza utakubaliana nami kuwa hakuna mwenye uwezo wa kuvaa viatu vya Rais Samia vya Uraisi. Ni Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan anayestahili kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa sababu ameonyesha uwezo, utulivu na stamina ya hali ya juu sana hata katikati ya mambo mazito yenye kila aina ya hisa kali, minyukano ya maneno, mawazo na maoni tofauti tofauti yenye kuibua hadi maneno ya ubaguzi na kibaguzi.

Rais Samia wakati wote ameonyesha umakini na utulivu wa kiwango cha juu sana.Historia yake pia ya kiutendaji imetukuka na iliyoonyesha ukomavu na utulivu wa kiuongozi alionao.

Amepita katika majaribu ya kila aina lakini amevuka akiwa imara na madhubuti.tofauti na wengine unakuta jambo dogo tu anajikuta akipaniki, kuhemuka, kupoteza utulivu, umakini na ustahimilivu na kujikuta akitumia na kuongozwa na jazba na hisia.

Rais Samia ameanzia na kupita maeneo mengi mpaka kufika hapo alipo kiutumishi amekaa na kufanya kazi na watu mbalimbali na wenye aina tofautitofauti za kiuongozi.ndio maana yakuona ameiva na kukomaa kisawasawa.

Anajiheshimu na ameiheshimisha taasisi ya Urais. Anajuwa nini anafanya na nini anapaswa kufanya na nini hapaswi kufanya hata kama anatamani kufanya kama binadamu wengine.

Kuna mwingine unakuta ni kiongozi mkubwa lakini anafanya vitu ambavyo vinashusha hadhi na kuchafua kiti alichokalia ni lazima ufahamu ya kuwa kuna vitu binafsi inabidi ujizuie kufanya au kutenda ni lazma ufahamu kuna uhuru binafsi fulani inabidi ukubali kupunguza unapokuwa kiongozi wa juu.
Screenshot_20240809-222814_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Furaha yako tu Mwenyewe imeshikiliwa na Rais Samia na ndio maana inacheza cheka na kufurahi sana huku jukwaani.maana huna msongo wa Mawazo wala wasiwasi ya aina yoyote ile
Furaha yangu inashikiliwa na Bwana Mungu. Huo ujinga wa kuabudu wanadamu baki nao mwenyewe
 
Back
Top Bottom