Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hivi na wewe unahofu na Mungu? Mbona una limdomo lichafu sana lenye kila aina ya Mimatusi na mimameno ya hovyo?Furaha yangu inashikiliwa na Bwana Mungu. Huo ujinga wa kuabudu wanadamu baki nao mwenyewe
Tunaye MboweNdugu zangu Watanzania,
Kwanza ningependa kuwakumbusheni kwa machache kati ya Mengi kuhusu mtu kuwa Rais.Ningependa kuwaambieni ya kuwa Mtu hawi Rais wala kukidhi vigezo vya Urais kwa kufanya tukio moja au kwa matukio yampito kama mvuke.wala mtu hawi RAIS kwa kuongea sana maneno mdomoni pake bila mipaka, mpangilio,utaratibu na utulivu.
Urais unahitaji mtu mwenye utulivu wa akili,mwenye afya njema ya akili .mwenye uwezo wa kudhibiti na kutawala hisia zake ,hasira zake,Mihemko yake,chuki zake, kinyongo chake na hata matamanio yake binafsi. Urais hauhitaji ujuaji. Urais ni taasisi inayohitaji mtu mwenye historia ya kiutendaji iliyotukuka. unaweza kumbeba beba mtu kwa njia zote na kumuweka katika nafasi fulani lakini kamwe huwezi kumbeba beba na kumzoa zoa mtu kumuweka kwenye kiti cha Urais.
Kwa hakika ni lazima utalitikisa,kulitetemesha,kulipoteza,kulivuruga,kulisambaratisha, kulikwamisha na kuleta sintofahamu kwa Taifa ikiwa ni pamoja na kuhatarisha usalama na umoja wa kitaifa.unaweza kumpa mtu upendeleo wa kumpatia nafasi yoyote ile na hata akifanya makosa yasiwe na athari kwa Taifa .lakini kamwe huwezi kumpa mtu Urais kwa majaribio na matamanio yako tu binafsi.
Urais siyo mahali pa kujifunzia kazi au kufanyia majaribio.Urais ni nafasi inayohitaji mtu aliyepevuka kiakili na kimwili,mtu anayejiheshimu,asiye na utoto utoto hata katika maandishi yake na maamuzi yake.Urais unahitaji mtu mwenye ngozi ngumu na mwenye uwezo wa kuogelea na kupiga mbizi katika Mawimbi ya kila aina na kulivusha Taifa.Urais hauhitaji ushindi katika kila mjadala.bali unahitaji maridhiano,subira, uvumilivu,usikivu kila panapotokea jambo lenye kugusa hisia za watu na mivutano. .
Urais unahitaji mtu mwenye uwezo ,akili ya kuongoza watu na kuwaleta pamoja licha ya tofauti zao za kisiasa ,mitizamo,Imani na mengine Mengi. Urais unahitaji mtu mwenye uwezo wa kufikiri ndio kufanya maamuzi na siyo kufanya maamuzi au kutoa maneno au kauli na kisha kufikiria juu ya maamuzi au kauli au maneno yaliyokwisha kutolewa na kutoka kinywani kama Risasi.
Ukiangalia hayo machache niliyoyaeleza utakubaliana nami kuwa hakuna mwenye uwezo wa kuvaa viatu vya Rais Samia vya Uraisi. Ni Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan anayestahili kuendelea kuliongoza Taifa letu.kwa sababu ameonyesha uwezo,utulivu na stamina ya hali ya juu sana hata katikati ya mambo mazito yenye kila aina ya hisa kali , minyukano ya maneno ,mawazo na maoni tofauti tofauti yenye kuibua hadi maneno ya ubaguzi na kibaguzi.
Rais Samia wakati wote ameonyesha umakini na utulivu wa kiwango cha juu sana.Historia yake pia ya kiutendaji imetukuka na iliyoonyesha ukomavu na utulivu wa kiuongozi alionao.amepita katika majaribu ya kila aina lakini amevuka akiwa imara na madhubuti.tofauti na wengine unakuta jambo dogo tu anajikuta akipaniki,kuhemuka,kupoteza utulivu,umakini na ustahimilivu na kujikuta akitumia na kuongozwa na jazba na hisia.
Rais Samia ameanzia na kupita maeneo mengi mpaka kufika hapo alipo kiutumishi.amekaa na kufanya kazi na watu mbalimbali na wenye aina tofautitofauti za kiuongozi.ndio maana yakuona ameiva na kukomaa kisawasawa.Anajiheshimu na ameiheshimisha taasisi ya Urais.Anajuwa nini anafanya na nini anapaswa kufanya na nini hapaswi kufanya hata kama anatamani kufanya kama binadamu wengine.kuna mwingine unakuta ni kiongozi mkubwa lakini anafanya vitu ambavyo vinashusha hadhi na kuchafua kiti alichokalia.ni lazima ufahamu ya kuwa kuna vitu binafsi inabidi ujizuie kufanya au kutenda.ni lazma ufahamu kuna uhuru binafsi fulani inabidi ukubali kupunguza unapokuwa kiongozi wa juuView attachment 3132946
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mimi siyo chawa bali ni msema kweli.na msema kweli siku zote ni mpenzi wa Mungu.Hivi mkuu unaweza hata ukapumzkka kidgo? Yaani tunaelekea uchaguzi ndio sasa umekuwa chawa pro.
Sacco's tu imemshinda kuiongoza .Tunaye mh mbowe
Umenena ukweli mchungu kabisa.Na zaidi sana hakuna Mtanzania mwingine kwasasa, ndani na nje ya CCM.. 🌹
Chawa kama chawa kaziniSacco's tu imemshinda kuiongoza .
Wewe hilo la kwako ni kama njia ya kutolea haja kubwa ovyo kabisa weweHivi na wewe unahofu na Mungu? Mbona una limdomo lichafu sana lenye kila aina ya Mimatusi na mimameno ya hovyo?
Hujitambui hata kidogo.Wewe hilo la kwako ni kama njia ya kutolea haja kubwa ovyo kabisa wewe
Mimi siyo chawa bali ni msema kweli.Chawa kama chawa kazini
Huna akiliHujitambui hata kidogo.
Njoo nikupe kazi uachane na uchawa Kuna kazi ya kuchimba kisimaMimi siyo chawa bali ni msema kweli.
Huyo kabla hajaanza uchawa kazi yake ilikuwa kutapisha vyoo,na hiyo kazi ni kama urithi maana ukoo wao wote ndiyo dili zao.Njoo nikupe kazi uachane na uchawa Kuna kazi ya kuchimba kisima
Mimi ni mkulima.Njoo nikupe kazi uachane na uchawa Kuna kazi ya kuchimba kisima