Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

King Kong III tumepata Rais ujue. Bado pesa kuingia mtaani

Itaingia tu si umeona mikakati ya Mh Rais? Yote hiyo ni kufanya kuwezesha mzunguko wa fedha urudi kwa watu na yeye ameliona hilo na katamka lengo kurudisha mzunguko wa fedha ambao ulirudi nyuma....Ndio kwanza ana siku 19 za urais ,tumpe muda ,si umeona karuhusu vyombo vyote vya habari vilivyofungiwa vifunguliwe,TRA kutumia ubabe kufunga bishara ukome,ajira za walimu zitekelezwe ,hayo yote yatachangia kuongeza mzunguko wa fedha mtaani....Pia kesi za uhujumu uchumi nazo ziangaliwe kama hazina base waachiwe.
 
Naam amegusia vitu vyote muhimu
 
Mama SSH hongera kwa kupata Cheo Kigumu kuliko vyote nchini. Kumbuka kila jicho la Mtanzania na Mabeberu nao wanakukodolea macho. Usiangalie sura ya mtu, wewe fuata ile misingi mizuri aliyoiacha mtangulizi wako, ukiyumba kidogo Mabeberu watafanya Ikulu sebure yao na kila mradi wa kimkakati ulio anzishwa na Mzee Wetu Magu utakwama.

Najua siyo kazi rahisi kufuata nyayo za Hayati Mzalendo Magu lakini jitahidi na wewe uweke Historia ya Mama Chuma, aliyewezesha Tanzania kupiga hatua za maana za maendeleo. Ukifungulia kila kitu kama kutoa vibali vya kazi kama njugu, utairudisha nchi kuwa SHAMBA LA BIBI na watanzania tutakuwa watumwa kwenye nchi yetu wenyewe. Jitahidi usiue spirit ya watu kupata kipato cha halali, usiruhusu watumishi wa umma kujitafutia kipato cha ziada kupitia ofisi za serikali, mfano mtumishi kuondoka kazini kabla ya muda wa kazi, uzembe kwa visingizio mbali mbali-ukemee kwa nguvu zote.

Nisikuchoshe, Mh. Rais ni vyema kuendelea kusimamia misingi ya kujenga nchi kwa njia ya kujitegemea-Tanzania ni Tajiri tunaweza! Tunasubiri tusikie mikakati yako ya miradi midogo midogo ya maendeleo! Tutataka kusikia umekamilisha SGR, Bwawa la Umeme la Mwalimu JKN, Daraja la Magufuli.
Ninakutakia kazi njema ila nasisitiza USIFUNGULIE MADIRISHA yote wazi, nchi itajaa nzi na mbu watatumaliza!
 
Acha kudanganya watu, mzunguko mkubwa wa pesa kipindi kile cha shamba la Bibi ulichangiwa na watumishi wengi wa serikali kutumia ofisi za umma ukipatia vipato haramu kama rushwa, ufisadi na uhujumu uchumi! Sasa hivi watu tulikuwa tunatumia pesa vizuri kwa sababu inatokana na vipato halali!
 
Sukuma Gang mtapata tabu sana...zamu yenu ishakwisha wacha pemba gang nao wapete.
 
Maneno yako yamejaa laana na chuki
 
Wa-Tz bwana,wamesahau kuwa pesa nyingi zilikuwa zinapigwa toka miradi ya serikali zinaingia mitaani.
Hizo ndizo wanazozifurahia.
Serikali ya SSH itavuna mizizi siyo mabua tena....si anacheka na nyani!
 
Mama na dada yangu na Rais wangu
maadamu umeshajionyesha unapenda mitandao basi subiri moto utakuwakia sana
marais wenzako wana timu ya watu wanaodeal na mitandao wewe umesema unaamka asubuhi na mapema eee!
haya subiri kidogo utajionea jinsi mambo yatakavyokuchenjia mpaka utatamani kuikimbia ikulu
halafu Mama mbona unaenda kasi sana kubadilisha mambo ya meko???mh!
inaonyesha ni jinsi gani ulivyo dhaifu kwa sababu umefanya kazi na meko muda wote ina maana ulikuwa umekaa tuu hujui nini kinaendelea???
mimi nakuonea huruma tuu nchi inaongozwa na professionals sio mihemko na maneno mengi
mawaziri wako wamekushtukia utajionea mambo yatakavyokwenda
hivi ile tumbua tumbua ya meko utaimudu?????
eeeh Mungu hii nchi twende wapi sasa,nani atatusaidia ndugu zangu???
huyu Mama keshafeli kabla ya kuanza
uongozi sio maneno mengi jamani mbona najisikia kuogopa mimi????
 
Umeandika nini ???
 
Mmghh kwani dhambi? Kwanini mnamshambulia sana huyu Mama? CCM mliambiwa tutumie Katiba ya Warioba mkakataa, Rasimu ya Katiba ile ingemfanya Mama Samia kuwa Raisi wa Mpito wakati nchi ikiandaa uchaguzi Mkuu mwingine, sasa mlichokikataa kinawatafuna wenyewe. MUNGU awafunge mdomo, mlisahau kuwa kuna KIFO
 
A time will tell [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sijui mnataka Rais wa namna gani, pombe mlikua mnamshutumu kwa mengi, sasa tumempata ambae ana utu bado hamumtaki, basi afande sele awe rais wenu
 
Kaa kwa kutulia, kuimba kupokezana, saivi zamu yenu[emoji16]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…