Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Mataga na nyomi ni mazuri kwani?

Afu leo ndo najua kuwa beberu ni mpinzani kumbe? Teh teh!
 
Nimewaza tu, lkn pia kwenye taasisi mbalimbali waweza wakajitwalia, na je wale walionaswa na vyeti feki Rais mpya anajuanwaweza wakarejeshwa na wale wale waliowapa nafasi na vyeti visivyo vyao??

Punzika kwa Amani Hatari JPM
 
Awafukuze Mwigulu Nchemba, Doto katibu mkuu wizara ya fedha na waziri wa Afya mapema kabsa kwani ndiyo watendaji wa hovyo kupata kutokea Duniani
Asimsahau na Sabaya na Happy
 
Mtapata taabu saana maana Mama Samia is the 'iron lady'! Ukiingia anga zake tu kuvuruga serikali iliyoyaanzisha chini ya JPM, ambayo yy naye alikuwa sehemu ya serikali hiyo lazima apite na weye!..
Waislam hawanaga roho mbaya zenu hizo, huyu mama atakuwa ni rais mwenye busara sana, na ndicho kinachohitajika ktk nafasi hiyo, hasa kwenye taifa kama letu lenye kila rasilimali. Tunaimani na Samia na lori halitachepuka.
 
Wadau wenzangu japokuwa tupo msibani lakini pia lazima tugange yajayo. Miaka mitano iliyobaki ni parefu kwa hiyo lazima tuweke mazingira safi ili tuweze kufika salama.

Wapo viongozi ambao moja kwa moja walihusika kuchafua kurasa huko nyuma. Hawa walihusika moja kwa moja kuhakikisha, haki za watu na uhuru wa watu unaminywa. Kwa hivyo hawafai kuwepo kwenye hii kurasa mpya tunayokwenda kuianza.

Sidhani kama ni vyema tuwe na Igp ambae hakutaka kufanya uchunguzi suala la Lissu kupigwa risasi. Pia kuwa na wakuu wa mikoa kama John Mongela au Chalamila ambao hawa ni viongozi wanafiki ambao waliunga mkono uvunjifu wa haki za binadamu.

Pia kuwa na Waziri kama Mwigulu Nchemba au Simbachawene haitafaa hata kidogo. Maana ni sawa na kutoanza kurasa mpya. Hivyo rais lazima afagie ngazi zote ili kupata kurasa mpya ambayo italeta amani kwa watanzania.

Ni hayo tu wanabodi.
Pia kuwa na Waziri kama Mwigulu Nchemba au Simbachawene haitafaa hata kidogo. Maana ni sawa na kutoanza kurasa mpya. Hivyo rais lazima afagie ngazi zote ili kupata kurasa mpya ambayo italeta amani kwa watanzania.[emoji1752][emoji1752][emoji1752]
 
Waislam hawanaga roho mbaya zenu hizo, huyu mama atakuwa ni rais mwenye busara sana, na ndicho kinachohitajika ktk nafasi hiyo, hasa kwenye taifa kama letu lenye kila rasilimali. Tunaimani na Samia na lori halitachepuka.
Yeah anahekima ya kuhakikisha yote aliyoyasimamia JPM mwa mafanikio ya nchi yetu atayasimamia!
Siyo yale ya JK kujaza sangoma, mashekhe ikulu, na kugawana madeal misikitini!

Hayo hatuyataki! Msema kweli na ambaye pia ni mpenzi wa Mungu ametwaliwa na mpenzi wake! Samia n8 wakati wa kuamua na kuchagua mpenzi! Msemkweli au msemauongo!
 
Mama Samia ,
Nikupongeza kwa dhati kwa kuapishwa kuwa Raisi wetu wa JMT.Hakuna ubishi ya kwamba umepokelewa kwa kishindo na makundi yote hata yale ambayo kimsingi yamekuwa makundi pinzani tangia mwaka 1992.

Mheshimiwa rais ,unayo nafasi ya kuwa raisi wa kwanza tangia mfumo wa vyama vingi kuanzishwa kuwa rais atakaekuwa anakunalika hata na akina Tomas wa upinzani ,hivyo Rais wetu naomba uzingatie yafuatayo:

1.Teuzi zote utakazofanya zizingatie uwezo wa mtu na sio affiliation ya mtu .Mfano former PST marehemu Likwelilie alipatikana kwa kuangalia uwezo na si chama.

2.Wale wenye teuzi na wamebaki kutoa lugha za kejeli kwa waliotofatiana nao ,tengua teuzi zao mara moja kwani wanakiharibia chama cha mapinduzi mfano ;Jerry Muro,Ole Sabaya ,Chalamila na hata yule RC wa Iringa.

3. Hakikisha miradi utakayoibua wewe kama mheshimiwa Rais inafanyiwa tathimini ya kina ,yaani itarudisha hela ya uwekezaji.

4.Jenga mazingira bora kwa ajili ya kukuza sekta binafsi na sio serikali kujikita kuanziasha mashirika ambayo hakika hayana ufanisi wowote mfano Suma JKT.

5.Anzisha sera ya kuvutia wawekeza wa nje ya nchi kwa mgeni yoyote mwenye kuwekeza zaidi ya dola milioni moja za kimarekani apewe resident permit ya miaka mitano bila malipo yoyote.

6.Anzisha Corpote flat rate kwa uwekezaji ambao utachochea ajira kwa wingi, mfano kwenye textile Industries.

Imenibidi nirudi humu jamvini kwani ni nadra saana kuwa na Rais aliepokelewa na makundi yote bila kujali itakadi zao .

Mungu mbariki saaana Raisi wetu Samia aka Mama wa nguvu.
 
Mama Samia ,
Nikupongeza kwa dhati kwa kuapishwa kuwa Raisi wetu wa JMT.Hakuna ubishi ya kwamba umepokelewa kwa kishindo na makundi yote hata yale ambayo kimsingi yamekuwa makundi pinzani tangia mwaka 1992...
Hahahaha Makupa umefufuka
 
Mimi ni mmoja kati ya wengi tuliomkubali uyu mama kwa moyo mmoka! Kwa Mara ya kwanza nimepata mtu nayeweza kutamka kwamba huyu ni raisi wangu
Subiri kwanza zoezi la kumpata vp lipite na tumjue vinginevyo hizi pongezi zako zinaweza kugeuka simanzi.
 
Tuulize kaka zako kuhusu Kikwete mwaka 2005, tathmini ya wakati ule ni haikuwahi rais akakubalika na wananchi kwa zaidi ya 90%, kukubalika siyo kuongoza Mama Samia mpeni mwaka au miezi sita ndo itajulikana mzuri au siyo mzuri.
 
Mwelekeo wake utajulikana baada tu ya kutangazwa kwa Makamu wake na pia iwapo alivunjilia mbali Baraza la Mawaziri la Mtangulizi wake lililojaa Mawaziri wengin vibwengo!
 
CCM ni ile ile, huwezi kupata kivuli kilichonyooka kutoka kwenye mti uliopinda.
 
Back
Top Bottom