Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Usimpangie mh nini Cha kufanya jiandae kupigwa chini mkuu, hivi mwamchukulia poa, mh sio lazima afanye yale ya mtangulizi wake, hoja hapa KWA mh apate kambi mzuri ya kumshauri, na afanye KWA mjibu wa taratibu zake, na hii ndo shida kwamba tz hatuna dira ya kitaifa kwamba kila kiongozi ajae huja KWA mtazamo wake ,ni simple kutawala USA kuliko TZ , tunahitaji katiba mpya kabla ya Mambo mengine
Hajalazimishwa awe kama JPM, hilo haliwezekaniki hata haiba zao (JPM na SSH) zinatofautiana. Anachoshauriwa ni akidhi kiu yetu ya kuona nchi yetu inasonga mbele, nyanja zote. Amerithi msingi mzuri, kama kuna sehemu inahitaji kuboreshwa ana uhuru huo. Uhuru ambao hana ni kuturudisha kwenye ufisadi, kuturudisha kwenye kutembeza bakuli kwa wazungu au kuifanya Tanzania iwe shamba la bibi. Na tunamshauri kwa unyenyekevu huku tukiamini kwamba anaweza, japo pia nguvu tunazo.
 
Wakati tuko mbioni kupata Rais mpya wa sita katika awamu ya tano. Tunamsihi sana apate kutekeleza majukumu yake katika Maslahi Mapana ya taifa. Na apate kutambua pia maana ya kauli ya Maslahi Mapana ya taifa. Maana viongozi wengi huamini Maslahi ya taifa Ni katika vitu tu hususa (miundo mbinu, rasili Mali vitu, n.k) na hukomea hapo.

Kiuhalisia si hivyo, Maslahi Mapana ya taifa huanzia kuunganisha taifa lipate kuwa kitu moja bila kujali itkadi za aina yoyote si za kisiasa na si za kiimani na si kikabila wala za kijinsia. Lengo hapa ni taifa lipate kushikamana na kushirikiana bila chuki Wala ubaguzi. Utawala uliopita ndani yake ulikuwa na chuki na ubaguzi wa wazi wazi.

Pili Maslahi Mapana ya taifa ni upande wa kuindaa rasili Mali watu (wananchi), katika fikra na mawazo ya kisasa na kuwaondolea ujinga (kiufupi ni kuwekeza taasisi za elimu katika elimu ya kisasa ya kuendana na Karne ya 21). Elimu ya Sasa iliyipo nchini Ni duni, maana kwa asilimia zaidi ya 80 Ni theory oriented. Wananchi ndio taifa lenyewe, hawa wananchi hutegemea wameandaliwa na elimu ya ubora aina gani.

Kwa uchumi wetu hatuwezi kutoa elimu bure, na tukitoa elimu basi itakuwa Bora na si elimu Bora. Elimu Bora ni gharama.
Sasa Ni Bora tukawa wananchi elfu 20 wenye elimu Bora (quality education, compatible with 21 century environment) na tukawa wananchi million 60 wanaoujua kusoma na kuandika?

Tatu Maslahi Mapana ya taifa ni pamoja na Sera na Sheria wezeshi kwa wananchi wake. Mfano utawala uliopita Sera za Kodi Ni kandamizi, hazimuinui mwananchi. Tukumbuke mwananchi nae anapaswa kuendelea kiuchumi, na serikali inapaswa kuendelea kiuchumi. Sera za Kodi za Sasa so rafiki kwa mwananchi, Bali Ni rafiki kwa serikali. Kwa biashara za watanzania wengi hususa wa mtaji mdogo baada ya makato ya Kodi na Kodi ya pango hujikuta wamepata pesa ya kula, kuvaa, n.k hapati faida ya kumfanya hafungue biashara nyingine, kiufupi apigi hatua nyingine.

4: Maslahi Mapana ya taifa Ni pamoja na utawala Bora na taasisi imara. Tanzania haitaji kiongozi imara inahitaji taasisi imara za kiserikali. Maana taasisi hudumu Karne na Karne, lakini kiongozi ufa au humaliza muda wake. Ndio maana baada Magufuli alivyokufa watu wametandwa na hofu, yote Ni tokana hatuna taasisi imara, serikali ya awamu tano ilisimama si tokana na taasisi imara Bali raisi imara.

Taasisi imara husimikwa na katiba na Sheria za. Nchi, maanake ya Sasa katiba inapaswa kubadilishwa.
Usifuate utamaduni wa ushabiki tumechika vifo! Fanya jitihada za chanjo kuokoa maisha ya Watanzania. Ushabiki usio na misingi tutapiteza wengi zaidi
 
Vyeti feki havikuwahi kuleta uchumi wa kati ndio maana walikimbilia kwenye uhujumu uchumi n.k vyeti feki watumishi hewa ilikuwa delaying strategy kuminya haki za watumishi. Imagine 5 years mtumishi anaimbiwa nyimbo za uhakiki vyeti feki watumishi hewa huku mshahara aliouacha jk ukiwa vilevile
POINT
 
Kuna watu wenye kujidai eti wanategemea mabadiliko toka kwa samia kama kubadili baraza la mawaziri sera na kadhali.

Fisadi ambao siku zote wameshindwa kukanusha mafanikio makubwa ya magufuli kiuchumi wanajidai hawajui ni kwa sababu ya uongozi wake kutokua na simile na ufisadi na uzembe kama nguzo kuu.

Pamoja na uzalendo uadilifu na ubunifu mkubwa kwa magufuli wateule wake amewaonyesha kwa vitendo cheo ni dhamana tu na amekua akiwatoa bila kusita wale waliyoshindwa kuwajibika.

Pamoja na kusafisha mahakama kuhusu ulaji rushwa bila kujali tuhuma za uongo kuhusu kuingilia uhuru wa mahakama ameshughulikia uhalifu wa kimafia kwa kuwatupa ndani vigogo sugu kama wale wa ipptl, simon group na kadhali ambao kutokana na rushwa kwenye mfumo wa sheria isingewezekana kuwatia mbaroni. Hilo limefanikiwa baada ya kufanya mabadilo kwenye sheria mbalimbali.

Mama samia ikiwa ataanguka kwenye mtego wa eti kulegeza kamba atakua amewadissapoint vibaya watanzania. Wala asisikie mwito eti wa maridhiano na chadema maana huo ni mtego mwingine. Kwanza aridhiane nini na chadema wakati hakina nguvu yoyote sasa kisiada zaidi ya kua chombo hatari kwa kutumiwa na adui wa mapinduzi ya uchumi ya taifa letu.

Sote tumtakie samia suluhu hassan mafanikio kuendeleza umagufuli na sio chochote tofauti.
 
Presha iko juu sana
Hawa watu ni kama walikuwa na ahadi na MUNGU kuwa Magu ataishi milele! Wakati wanampatia nafasi ya makamu hawakujua kuwa kuna kufa na makamu kuchukua nafasi ya Ukuu wa nchi.

Mama anaonekana mstaarabu atakayeileta nchi pamoja bila kubaguana kwa makabila na dini! Inavyoonekana MATAGA walikuwa wafaidika wakubwa na hii tabia ya kuoneana, kubambikiziwa kesi, kutekwa.

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
 
... itarudi kwa mafisadi Chadema au sio?
 
Bi Samia Suluhu alete maridhiano na Umoja wa Kitaifa tutamuelewa apangue na safu ya Mawaziri wa "ndio mzee!!" aweke safu ya Mawaziri wenye weledi ambao sio waoga wenye kuhoji
 
Baada ya Kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli na hatimae Mama wa Afrika Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kushika usukani wa kiliongoza Taifa, kumekuwa na Washauri wa kila aina kuhusu majukumu yake.

Ninapowafuatilia nawaona kabisa namna mlivyokosa utashi wa kujua ukubwa wa Makamo wa Rais, nadhani mkiipitia Katiba ipasavyo mtagundua kuwa Makamo wa Rais ni Rais anayetazamiwa kuongeza Nchi kwa wakati wowote.

Makamo wa Rais huwa anaijua Nchi na mifumo yake yote, anajua mapato, miradi, mwenendo wa Nchi na hali yake. Pia mkumbuke Rais yeyote asiyeweza kufanya kazi na Makamo wake basi Nchi hiyo itayumba. Hili liwafungue akili kuwa Dr. Magufuli na Mama Samia Walifanya kazi pamoja na anaijua hii Nchi.

Hivyo kuongeza Nchi akitokea kuwa Makamo wa Rais, Sio ugeni. Nawaambia atakuwa na mafanikio makubwa kuliko idadi ya ushauri wenu wa kinafiki.

Leo mnadhani anakuja kujifunza kazi ya Urais, mnachelewa, Mheshimiwa Samia ni Rais tangu 2015 na ndio maana aliitwa Mgombea mwenza.

Maana hata Watesi wa Taifa wanajifanya washauri wa karibu na kuijua Nchi, Nchi hii haijatoka vitani, kila kitu kiko kwenye mfumo wake na Mheshimiwa Rais anaujua vilivyo.

Eti munamfundisha kuhusu Demokrasia, Katiba na Muundo wa Serikali yake... "Ajabu kubwa".

Mhe. Amezungukwa na vyombo vinavyofanya tathimini za kina na sio mihemko ya wapiga kelele, Nchi lazima ifanye maamuzi yanayotazama miaka 100 mbele na sio kwa sababu wewe hauko Bungeni au ulikutwa na mkono wa Sheria.

MSIJIVIKE UPENDO USIOKUWA NAO.
 
Kuna watu wanasijogeza ili mama awaone
Si unajua mambo ya teuzi

Ova
 
Nimemwona mzee Mangula jinsi alivyozungumza kaonesha kuwa ana wasiwasi na huyu Rais wetu. Hofu yangu kuna uwezekano wa kuingiliwa na kupangiwa majukumu na baadhi ya wahuni waliopo CCM kwa kisingizio cha kumsaidia kasi kama ya Magufuli. Chondechonde watanzania tuwe makini na hawa watu, wajaribu kmwacha huyu mama atufikishe salama. Naona kuna kagenge kanaundwa ka majungu majungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom