Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Dodoki? Sidhani kama Sabaya anasafishika! Hata kama ni mfumo kwanini iwe yeye tu???

Mama ametupa zawadi nzuri ya Eid. Huu ni ushahidi kuwa Sabaya ameumiza watu wengi ndio maana maamuzi ya kumfurusha yamepokelewa kwa furaha kubwa na nchi nzima.

Jambo la muhimu zaidi mama hajaishia kumfurusha tu bali ameagiza ufanyike uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili ili afikishwe mahakamani. Kwahiyo sasa hivi Sabaya ni mtuhumiwa. Muda wowote tutamuona nyuma ya karandinga.

Sabaya ana tuhuma mbalimbali (lukuki) kama taarifa ya Ikulu ilivyoeleza. Anatuhumiwa kupora, kunyanyasa na kutumia madaraka yake vibaya. Tuhuma hizi zimekuwepo tangu enzi za mwendazake lakini amekua akilindwa.

Yeye mwenyewe amewahi kujitapa kuwa hakuna anayeweza kumpa order isipokua mwendazake pekee. Alimdharau hadi RC wake. Ndio maana mama Mghwira alipomwambia aache kutumia mabavu alimcheka kwa dharau. Mwaka 2019 PM alifanya ziara K'njaro wafanyabiashara wakamueleza jinsi Sabaya anavyowanyanyasa, lakini hakuchukua hatua yoyote. Akasema atayafikisha kwa mamlaka yake ya uteuzi.

Lakini hakuna chochote Sabaya alichofanywa. Badala yake alizidi kuwa kiburi kuliko mwanzo. Wale wafanyabiashara "waliomchongea" kwa PM walipata joto ya jiwe. Na PM hakuwa na chochote cha kumfanya. Hatimaye leo mama amevunja kisiki kilichowashinda maksai.

Sabaya anatuhumiwa kutumia mabavu kupora fedha kwa wafanyabiashara mbalimbali. Mmoja wao ni Cuthbert Swai mmiliki wa Asante Tours na Hoteli ya kitalii ya Weruweru.

Cuthbert anadai mwaka 2018 Sabaya alitaka ampe 10M otherwise atampa kesi ya uhujumu uchumi. Kwa kuhofia jela akampa. Baadae akataka tena 10M, akamwambia hana. Baada ya vitisho vya mara kwa mara, wafanyabiashara wenzake wakamwambia mpe tu, usicheze na mjinga atakutoboa jicho. Akampa kishingo upande.

Baada ya miezi michache Sabaya akamwambia kuna "special mission" amepewa hivyo inatakiwa pesa nyingi kuitekeleza. Kwahiyo wafanyabiashara wanatakiwa wachangie. Akamtaka Cathbert atoe 15M. Cuthbert akamwambia biashara ya utalii imeyumba hivyo hawezi kupata fedha hizo.

Na hapo akatangaza uhasama na Cathbert. Akaenda kwenye mashamba yake huko Rundugai akasema alidhulumu wanakijiji. Akatengeneza wazee feki waliojifanya wamedhulumiwa, halafu akatangaza kuyataifisha.

Hakuishia hapo akavamia hoteli ya kitalii ya Weruweru inayomilikiwa na Cathbert. Siku hiyo Nandy alikua na show Arusha, akalala Weruweru. Usiku saa 9 Sabaya akavamia akiwa na kikosi cha watu 6 wenye silaha. Akalazimisha aoneshwe chumba cha Nandy, mhudumu aliyekua mapokezi akakataa. Sabaya akampiga sana. Walinzi walipotoka nao wakapigwa na mabaunsa wa Sabaya.

Matukio yote yalirekodiwa kwenye CCTV camera but who cares? Pamoja na video hiyo kusambaa lakini hakupewa hata onyo. Utamwambia nini mtoto pendwa wa mwendazake? Aliwahi kujitapa kuwa yeye ndiye DC pekee anayeweza kumpigia simu mwendazake usiku wa manane na akapokea.

Akaendelea kuvuruga biashara mbalimbali za Cathbert na kuagiza TRA wafreeze baadhi ya akaunti zake. Hali ikawa ngumu hadi mali za kampuni ya Asante Tours zikapigwa mnada. Akavuruga shamba la wanyama (zoo) la Cuthbert maeneo ya Maili sita. Akaharibu mizinga 200 ya nyuki kwenye shamba la Cathbert kwa madai hana kibali cha maliasili cha kufuga nyuki.

Baada ya hapo Cuthbert anadai Sabaya alitishia kumuua. Ikamlazimu kukimbilia ziwa Jipe mpakani mwa Kenya akaishi huko. Zaidi ya watu 300 waliokua wameajiriwa kwenye biashara zake mbalimbali wakapoteza ajira kwa sababu ya Sabaya. Just imagine.

Lakini hakuishia kwa Cuthbert, akaendelea kufanya ukatili kwa watu wengine. September 2020 alivamia hoteli ya Protea Aishi iliyopo Machame, inayomilikiwa na Freeman Mbowe. Hotelini hapo kulikua na wageni kutoka nje ya nchi wanaopanda mlima Kilimanjaro.

Sabaya akawakamata na kudai wamekuja kusaidia Chadema kwenye uchaguzi. Wakatolewa hotelini usiku wa manane na night dress kupelekwa kituo cha Polisi Bomang'ombe. Wakahojiwa na kuachiwa, lakini wamesababishiwa usumbufu, na wameweka doa kwenye sekta yetu ya utalii. Kumbuka tunatumia fedha nyingi kutangaza utalii, halafu mtu mmoja anawadhalilisha kwa mihemko tu.

Siku ya uchaguzi (October 25) alivamia tena Aishi hotel akiwa na magari yenye namba za UN. Wakawapiga walinzi na kukamata baadhi ya mawakala wa Chadema waliokua hapo. Wakawatia matambara mdomoni na kuwapiga sana kabla ya kwenda kuwatelekeza maeneo ya Sanya stesheni usiku huo.

Mmoja wa vijana hao Simon Mwacha alivunjwa mkono karibu na joint. Hadi sasa amefanyiwa upasuaji mara 3 lakini hajapona. Wiki iliyopita viongozi wa BAVICHA walimtembelea na kumkuta amewekewa POP jingine. Huu ni mwezi wa 7 tangu avunjwe na Sabaya na bado hajapona.

Kutumia number za UN kufanya uhalifu ni doa katika diplomasia ya nchi, lakini hakujali hilo. Yeye ni mtoto pendwa wa mwendazake, mtamfanya nini? Kama PM alishindwa kumfanya lolote, aliamini wengine hawamuwezi.

Aliwekeza nguvu na akili zake zote kwa mwendazake. Alimtumainia, alimuabudu na kumsujudu. Lema aliwahi kumwambia huyo unayemtegemea si Mungu. Ipo siku hatakuwepo na utakosa mtetezi. Sabaya akacheka kwa dharau. Leo yametimia yale aliyosema Lema miaka mitatu iliyopita.

Sabaya anatuhumiwa kumteka na kumpiga mtia nia wa udiwani huko Machame. Anatuhumiwa kunyanyasa wananchi mbalimbali kwa sababu za kisiasa. Anatuhumiwa kumpiga ngumi na kumpasua uso mfanyabiashara (Shoo) wa Bomang'ombe baada ya kumkuta akiuza vileo kwenye duka la bidhaa za rejareja.

Sabaya alitengeneza kikundi cha "mabaunsa" ambacho kilikua kinatembea nae popote. Hawakua walinzi rasmi wa serikali. Ni "wahuni" tu aliowaokota mtaani na kuwapa silaha, kama alivyofanya(ga) Bashite.

Kikundi hiki kilikua hakina tofauti na "Mungiki" maana kilitii kila order ya boss wao, hata ambazo ni unlawful. Kiliteka, kilijeruhi na kiliharibu mali kwa order ya Sabaya. Kikundi hiki kiliwahi kuteka moja ya magari ya Freeman Mbowe (likiwa imepaki Arusha) na kutia chumvi kwenye engine. Pamoja na Mbowe kuripoti polisi lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa.

Kitendo cha Sabaya kuokota vijana mtaani wasio na mafunzo yoyote ya kijeshi na kuwapa silaha wamlinde ni kosa kisheria. Lakini nani wa kuhoji kama mwendazake alibariki hilo?

Kikundi hiki kimewahi kumpiga mfanyabiashara mmoja (Molel) pub moja maeneo ya Kijenge. Vijana wa Sabaya walimzingira na kumtuhumu kumshika "makalio" mpenzi wa mmoja wao. Wakampiga na kumlazimishwa kutoa kiasi cha pesa ili wamwachie. Kitendo hicho kiliharibu biashara ya eneo hilo, hadi sasa pamepoa licha ya kwamba ni eneo zuri la starehe.

February 09, 2021 Sabaya na genge lake walienda Arusha kumvamia Ally Asaad Ajirin, anayemiliki duka la mapazia la Shaahidi Stores lililopo Barabara ya Nyamwezi jirani na Soko Kuu. Wakamwambia "tuna taarifa unafanya biashara ya kubadili pesa za kigeni kinyume cha sheria" Asaad akakataa.

Anadai Sabaya alimtaka atoe 100M ili asipewe kesi ya uhujumu uchumi. Lakini akamwambia wewe ni DC wa Hai unapata wapi mamlaka ya kuja kunihoji Arusha? Sabaya kusikia hivyo akaagiza milango ifungwe, wakampiga na kumtaka aoneshe pesa zilipo. Wananchi kusikia kilio wakampigia simu Diwani wa Sombetini Bakari Msangi. Alipofika na kuhoji akaunganishwa kwenye kipigo.

Kwa kifupi Sabaya alimiliki kikundi cha kigaidi. Na alikua anaenda nacho popote, iwe ofisini au night club. Hata juzi Dar alikua nacho, akizunguka nacho sehemu mbalimbali.

Mimi ni "survivor" wa kikundi hicho. November mwaka jana nilisema kitendo cha Sabaya kutumia plate number za UN kufanya uhalifu ni doa kubwa kidiplomasia. Akanipigia simu, sikupokea. Akaniandikia 'sms' ya vitisho. Akaniambia akinikamata nitajuta kuongelea vitu nisivyovijua. Sikumjibu lakini nikascreenshot na kumtumia rafiki yangu mmoja ambaye ni kiongozi serikalini just for reference likitokea lolote.

December 26 nikiwa na Don J Mbowe mahali flani Moshi, tukifurahia sikukuu za mwisho wa mwaka, tukaondoka saa 7 usiku. Kesho yake Meneja wa eneo hilo akanipigia simu akasema tulipoondoka tulimuachia balaa kubwa. Sabaya alifika na kikundi chake na kutuulizia. Alipoambiwa tumeondoka, hakuamini.

Akachomoa bastola na kufyatua hewani. Akaleta taharuki, watu wakatawanyika. Hakujali kuharibu biashara, alichojali ni kutimiza matakwa yake. Mabaunsa wakapekua counter hadi vyooni. Hatukuwepo.

Sijui wangetukuta ingekuaje. Pengine tungepigwa na kuwekewa dawa za kulevya mfukoni. Halafu kesho yake dunia ingetangaziwa kuwa tumekutwa na dawa za kulevya. Tungeshtakiwa na kunyimwa dhamana. Huenda hadi leo tungekua tunasota gerezani.

Lakini Mungu wa rehema akakumbuka watanzania tunaowarudishia(ga) tabasamu kwa njia mbalimbali, akaamua kutuokoa. Tuliondoka tukidhani tunaenda kupumzika, kumbe ilikua njia ya Mungu kutuepusha na mkono wa yule mwovu.

Huyu ndiye Lengai Ole Sabaya Jambazi aliyejificha kwenye kivuli cha ukuu wa wilaya na kulindwa na mamlaka za nchi. Mtu aliyewahi kughushi kitambulisho cha idara ya usalama wa taifa, na kushtakiwa mahakamani lakini bado akapewa ukuu wa wilaya. Unampaje uongozi mtu mwenye 'jinai' ya kughushi?

Ajabu ni kwamba kila alipoulizwa kuhusu tuhuma zake alikimbilia kumtaja Mbowe. Nikajiuliza je Mbowe ndiye alimtuma kuteka watu? Mbowe ndiye alimtuma kumvamia Nandy hotelini? Mbowe ndiye alimtuma aweke namba za UN kwenye magari yake ya kufanyia ujambazi? Mbowe ndiye alimtuma ampige diwani wa Sombetini? Kwanini kila anapoulizwa anamtaja Mbowe?

Nikagundua hii ndio njia aliyokua akiitumia kumhadaa mwendazake. Alikua akifanya ukatili anajificha kwenye kivuli cha Mbowe na upinzani. Na mwendazake alimuelewa maana upinzani ulikua adui yake mkubwa. Ukiteka, ukijeruhi, ukiharibu mali ya mtu we sema unafanya hivyo ili kuumaliza upinzani, mwendazake atakuelewa.

Kwahiyo Sabaya alisahau kwamba zama zimebadilika. Ndio maana juzi alipokua CMG alimtaja Mbowe mara nyingi zaidi kuliko tuhuma zinazomkabili. Alidhani kwa kusema amemng'oa Mbowe itamsaidia kujustify maovu yake, kumbe mama ana hofu ya Mungu na hapendezwi na huo uzandiki.

Suala hili la Sabaya lisaidie media kuzingatia profesionalism. Ni aibu media kubwa kama CMG kutumika kumsafisha "jambazi" Sabaya. Ile interview ya juzi ilikua "biased" na ilikosa impartiality and objectivity. Hata Sabaya alivyokua ana-behave sio kama interviewee, bali kama bepari aliyenunua kipindi, akajiandalia maswali na hivyo anajibu anavyojisikia.

Kaka mkubwa Edo Kumwembe aliwahi kusema "Heshimu watu, sponsor hufariki" nadhani hili ndio somo ambalo kila kiongozi anapaswa kujifunza kwa Sabaya. Ukipewa madaraka watendee haki watu wote. Usinyanyase watu kwa sababu una sponsor. Ipo siku sponsor hatakuwepo na utapata tabu sana.

Asante mama kwa kuirudisha nchi kwenye mstari wa haki. Hakika wewe ni zawadi tuliyopewa na Mungu. Tunakuombea ili Munghu mwenyewe awe taa ya njia zako na mwanga wa miguu yako, usiteleze wala kuanguka (Zab 119:105).!

Malisa GJ

Mama ametekeleza ombi la upinzani
 
Badala ya kukomaa na wezi bandarini anakomaa na sabaya kuufurahusha upande x

Ipo siku wapinzani watataka fulan mwengine atolewe atatolewa
Makada tumechutuma kwenye hili
Ila kwa usikivu na ufuatiiaji wa mambo mitandaon atakua ameona wapinzani hawajawai kua na jema over
 
Mkuu kwani wewe umezuiwa kupiga mdundo wako, mama mwenyewe atachagua ngoma ya kucheza....kwa nini kumchagulia ngomaaaa!
 
Baada ya mkuu wa wilaya ya hai kutumbuliwa tunaona wapinzani wakiwa na furaha sana je? ni lini wapinzani wamekua wema kwa chama tawala.

Itoshe kusema upinzani kamwe sio rafiki wema kwenye chama tawala na hawez kua na agenda njema kwa ccm.

Dc mstafau ole sabaya muda mrefu amekua akipambana na upinzani mkubwa sana Kwani eneo la hai ndipo pinzani kuu anatoka hivo amekua akiandamwa sana kwani alizibiti mno mambo mengi.

Wapinzani wamepiga debe sana mtu huyu kuondolewa na imekua hivo hivo. Mama yetu Rais SSH ni wazi wapinzani wanajiona washindi kwenye hili.

Yaani katumbuliwa halafu kawa DC mstaafu.... huna hoja unaleta vioja.

Ka hiyo kupambana na upinzani na kudhibiti democracy ndo anakuwa ametekeleza majukumu yake kama DC... only idiot think alike.

Nikueleze hivi Mama kuna mambo yuko sawa na Mwendazake lkn kuna mambo ambayo hakubaliani nayo kama hayo ambayo mpuuzi mwenzio Nyangoro Sabaya amefanya.
 
Mama kanyaga hao Kima!👏👏👏
View attachment 1784595
nby6543.jpg
 
Sifa zilimuangusha Joyce Banda wa Malawi akitafuta kuwafurahisha wamalawi kuliko mtangulizi wake na wafadhiri hadi akaruhusu ushoga. Yuko wapi leo hii? NGO ni tofauti na nchi. Nchi haihitaji umaarufu binafsi na kusifiwa na wafadhiri, ni heshima kwa wananchi wake.

Rais wetu amemsimamisha mkuu wa wilaya kwa uchunguzi. Uchunguzi upi? Amua tu kwamba nimekuondoa kwa taarifa ulizonazo. Huyu ni afisa aliyefanyiwa vetting, ambaye kila anachokifanya kila siku kinaripotiwa na DSO ngazi za juu hadi taifa? Kumsimamisha ni uzembe na kutafuta kujulikana maana kila kitu kiko mezani kwa rais.

Rais wetu alihitaji muda wa kuifahamu nchi na makabila yake na uhusiano wetu na hata kujua yapi yalifanywa na serikali zilizopita zote, kabla hajaanza hizo papala. Uchagani kuna dhalau ya makabila yote yanayowazunguka na kwa mkuu huyu wa Wilaya, anayetokea mkoa jirani kwao wanaona hastahili kuwatawala. Ni hivyo kote! Iwe ni Shehe, Padri, Askofu, Diwani, mbunge, nk. Hawataki kabila jingine. Ooh! Njoni na matusi sasa lakini huo ndo ukweli.
 
Una uhakika gani kuwa amepata taarifa toka mitandao? After all mitandao ni source of information , ni matter ya kuzichuja.

Mfano wewe hapo jaribu kuandika kuwa utapindua serikali kama utalala nyumbani kwako.. unataka kusema taarifa kama hiyo ipuuzwe? Never!

Pili, Kwani hana njia za kupata taarifa za watu anowataka kupata tarifa zao kwa kutumia official means?

Sifa zilimuangusha Joyce Banda wa Malawi akitafuta kuwafurahisha wamalawi kuliko mtangulizi wake na wafadhiri hadi akaruhusu ushoga. Yuko wapi leo hii? NGO ni tofauti na nchi. Nchi haihitaji umaarufu binafsi na kusifiwa na wafadhiri, ni heshima kwa wananchi wake.

Rais wetu amemsimamisha mkuu wa wilaya kwa uchunguzi. Uchunguzi upi? Amua tu kwamba nimekuondoa kwa taarifa ulizonazo. Huyu ni afisa aliyefanyiwa vetting, ambaye kila anachokifanya kila siku kinaripotiwa na DSO ngazi za juu hadi taifa? Kumsimamisha ni uzembe na kutafuta kujulikana maana kila kitu kiko mezani kwa rais.

Rais wetu alihitaji muda wa kuifahamu nchi na makabila yake na uhusiano wetu na hata kujua yapi yalifanywa na serikali zilizopita zote, kabla hajaanza hizo papala. Uchagani kuna dhalau ya makabila yote yanayowazunguka na kwa mkuu huyu wa Wilaya, anayetokea mkoa jirani kwao wanaona hastahili kuwatawala. Ni hivyo kote! Iwe ni Shehe, Padri, Askofu, Diwani, mbunge, nk. Hawataki kabila jingine. Ooh! Njoni na matusi sasa lakini huo ndo ukweli.
 
Sabaya alikuwepo hai kimkakati kila mmoja anajua , na alichokifanya ni Kwa manufaa ya CCM na ilimlazimu kufanya hvyo ili kufanikisha alichokifanya , kama mama anatafuta namna ya kumweka sehemu nyingine Sawa Ila kama amemfukuza Mazima basi amechochora , lakn ndo hvyo sometyme unajitoa kudhalilika alaf badae unatupiwa vilago
 
Sifa zilimuangusha Joyce Banda wa Malawi akitafuta kuwafurahisha wamalawi kuliko mtangulizi wake na wafadhiri hadi akaruhusu ushoga. Yuko wapi leo hii? NGO ni tofauti na nchi. Nchi haihitaji umaarufu binafsi na kusifiwa na wafadhiri, ni heshima kwa wananchi wake.

Rais wetu amemsimamisha mkuu wa wilaya kwa uchunguzi. Uchunguzi upi? Amua tu kwamba nimekuondoa kwa taarifa ulizonazo. Huyu ni afisa aliyefanyiwa vetting, ambaye kila anachokifanya kila siku kinaripotiwa na DSO ngazi za juu hadi taifa? Kumsimamisha ni uzembe na kutafuta kujulikana maana kila kitu kiko mezani kwa rais.

Rais wetu alihitaji muda wa kuifahamu nchi na makabila yake na uhusiano wetu na hata kujua yapi yalifanywa na serikali zilizopita zote, kabla hajaanza hizo papala. Uchagani kuna dhalau ya makabila yote yanayowazunguka na kwa mkuu huyu wa Wilaya, anayetokea mkoa jirani kwao wanaona hastahili kuwatawala. Ni hivyo kote! Iwe ni Shehe, Padri, Askofu, Diwani, mbunge, nk. Hawataki kabila jingine. Ooh! Njoni na matusi sasa lakini huo ndo ukweli.
Tulia dawa ifanye kazi,dawa ya kushusha homa, vipo vidonge na sindano wewe, chagua sindano ama vidonge.
 
Una uhakika gani kuwa amepata taarifa toka mitandao? After all mitandao ni source of information , ni matter ya kuzichuja. Mfano wewe hapo jaribu kuandika kuwa utapindua serikali kama utalala nyumbani kwako.. unataka kusema taarifa kama hiyo ipuuzwe? Never!
Pili, Kwani hana njia za kupata taarif za watu anowataka kupata tarifa zao kwa kutumia official means?
Endelezeni tu dharau,ukizingua ana zingua,tena uzuri sii kwa fedheha,ila kistaarabu kabisa.Pole kama ndiye mhanga mwenyewe.
 
Sifa zilimuangusha Joyce Banda wa Malawi akitafuta kuwafurahisha wamalawi kuliko mtangulizi wake na wafadhiri hadi akaruhusu ushoga. Yuko wapi leo hii? NGO ni tofauti na nchi. Nchi haihitaji umaarufu binafsi na kusifiwa na wafadhiri, ni heshima kwa wananchi wake.

Rais wetu amemsimamisha mkuu wa wilaya kwa uchunguzi. Uchunguzi upi? Amua tu kwamba nimekuondoa kwa taarifa ulizonazo. Huyu ni afisa aliyefanyiwa vetting, ambaye kila anachokifanya kila siku kinaripotiwa na DSO ngazi za juu hadi taifa? Kumsimamisha ni uzembe na kutafuta kujulikana maana kila kitu kiko mezani kwa rais.

Rais wetu alihitaji muda wa kuifahamu nchi na makabila yake na uhusiano wetu na hata kujua yapi yalifanywa na serikali zilizopita zote, kabla hajaanza hizo papala. Uchagani kuna dhalau ya makabila yote yanayowazunguka na kwa mkuu huyu wa Wilaya, anayetokea mkoa jirani kwao wanaona hastahili kuwatawala. Ni hivyo kote! Iwe ni Shehe, Padri, Askofu, Diwani, mbunge, nk. Hawataki kabila jingine. Ooh! Njoni na matusi sasa lakini huo ndo ukweli.
Hama nchi na umwache mama arudishe nchi kwenye mstari. Hatuwezi kundesha nchi na wahuni kama hao unaowatetea hapa, Mama piga kazi, tuko wote kwa kila hali.
 
Sabaya alikuwepo hai kimkakati kila mmoja anajua , na alichokifanya ni Kwa manufaa ya CCM na ilimlazimu kufanya hvyo ili kufanikisha alichokifanya , kama mama anatafuta namna ya kumweka sehemu nyingine Sawa Ila kama amemfukuza Mazima basi amechochora , lakn ndo hvyo sometyme unajitoa kudhalilika alaf badae unatupiwa vilago
Acha kupotosha ,serikali hakuwahi kumtuma kwenda kupora maduka.
 
Sifa zilimuangusha Joyce Banda wa Malawi akitafuta kuwafurahisha wamalawi kuliko mtangulizi wake na wafadhiri hadi akaruhusu ushoga. Yuko wapi leo hii? NGO ni tofauti na nchi. Nchi haihitaji umaarufu binafsi na kusifiwa na wafadhiri, ni heshima kwa wananchi wake.

Rais wetu amemsimamisha mkuu wa wilaya kwa uchunguzi. Uchunguzi upi? Amua tu kwamba nimekuondoa kwa taarifa ulizonazo. Huyu ni afisa aliyefanyiwa vetting, ambaye kila anachokifanya kila siku kinaripotiwa na DSO ngazi za juu hadi taifa? Kumsimamisha ni uzembe na kutafuta kujulikana maana kila kitu kiko mezani kwa rais.

Rais wetu alihitaji muda wa kuifahamu nchi na makabila yake na uhusiano wetu na hata kujua yapi yalifanywa na serikali zilizopita zote, kabla hajaanza hizo papala. Uchagani kuna dhalau ya makabila yote yanayowazunguka na kwa mkuu huyu wa Wilaya, anayetokea mkoa jirani kwao wanaona hastahili kuwatawala. Ni hivyo kote! Iwe ni Shehe, Padri, Askofu, Diwani, mbunge, nk. Hawataki kabila jingine. Ooh! Njoni na matusi sasa lakini huo ndo ukweli.
Tatizo lenu hamtaki kuamini kuwa baba yenu aliye wapa kiburi cha kufanya mnavyotaka amesha kufa.

Tulia sasa mtazame dunia inavyo kwenda .

Ndiyo msahau kabisa kugusa milango ya Ikulu.
 
Sifa zilimuangusha Joyce Banda wa Malawi akitafuta kuwafurahisha wamalawi kuliko mtangulizi wake na wafadhiri hadi akaruhusu ushoga. Yuko wapi leo hii? NGO ni tofauti na nchi. Nchi haihitaji umaarufu binafsi na kusifiwa na wafadhiri, ni heshima kwa wananchi wake.

Rais wetu amemsimamisha mkuu wa wilaya kwa uchunguzi. Uchunguzi upi? Amua tu kwamba nimekuondoa kwa taarifa ulizonazo. Huyu ni afisa aliyefanyiwa vetting, ambaye kila anachokifanya kila siku kinaripotiwa na DSO ngazi za juu hadi taifa? Kumsimamisha ni uzembe na kutafuta kujulikana maana kila kitu kiko mezani kwa rais.

Rais wetu alihitaji muda wa kuifahamu nchi na makabila yake na uhusiano wetu na hata kujua yapi yalifanywa na serikali zilizopita zote, kabla hajaanza hizo papala. Uchagani kuna dhalau ya makabila yote yanayowazunguka na kwa mkuu huyu wa Wilaya, anayetokea mkoa jirani kwao wanaona hastahili kuwatawala. Ni hivyo kote! Iwe ni Shehe, Padri, Askofu, Diwani, mbunge, nk. Hawataki kabila jingine. Ooh! Njoni na matusi sasa lakini huo ndo ukweli.
Hizo tuhuma za kuomba rushwa,kuvamia sehemu na mabunduki kwako ni sawa?Wacha uchunguzi ufanyike!kwenye ukweli uongo hujitenga tulia,yataonekana yaliyopo!
 
Sifa zilimuangusha Joyce Banda wa Malawi akitafuta kuwafurahisha wamalawi kuliko mtangulizi wake na wafadhiri hadi akaruhusu ushoga. Yuko wapi leo hii? NGO ni tofauti na nchi. Nchi haihitaji umaarufu binafsi na kusifiwa na wafadhiri, ni heshima kwa wananchi wake.

Rais wetu amemsimamisha mkuu wa wilaya kwa uchunguzi. Uchunguzi upi? Amua tu kwamba nimekuondoa kwa taarifa ulizonazo. Huyu ni afisa aliyefanyiwa vetting, ambaye kila anachokifanya kila siku kinaripotiwa na DSO ngazi za juu hadi taifa? Kumsimamisha ni uzembe na kutafuta kujulikana maana kila kitu kiko mezani kwa rais.

Rais wetu alihitaji muda wa kuifahamu nchi na makabila yake na uhusiano wetu na hata kujua yapi yalifanywa na serikali zilizopita zote, kabla hajaanza hizo papala. Uchagani kuna dhalau ya makabila yote yanayowazunguka na kwa mkuu huyu wa Wilaya, anayetokea mkoa jirani kwao wanaona hastahili kuwatawala. Ni hivyo kote! Iwe ni Shehe, Padri, Askofu, Diwani, mbunge, nk. Hawataki kabila jingine. Ooh! Njoni na matusi sasa lakini huo ndo ukweli.
Mtajifunza utawala wa sheria na haki taratibu mpaka muelewe, mmezoea vya kunyonga.
 
Back
Top Bottom