Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Kwa wafuatiliaji watakubaliana na Mimi juu ya mazingira ya ' win-win' anayoyatengeneza kwenye siasa za nchi yetu. Licha ya ukubwa na uimara wa CCM bado Rais Samia anaamini kwenye "win-win" kati ya CCM na Upinzani.

Kwetu Bado tunajifunza mengi kutoka kwake ,amedhihirisha uvumilivu ni msingi wa uongozi bora.

Tuendelee kumuonbea Rais wetu ili tuone matokeo ya win-win yatawanufaisha vipi wapinzani maana naamini watafurahishwa sana ila ni Kwa wale wanaomuelewa na Kwa wale wasiomuelewa wajiandae Kwa namna yao
 
Wadau nawasabahi.Nichukue Nafasi hii kumpongeza Mh.RAIS SAMIA kuwakataa HADHARANI MACHAWA wote wanaojiita "WATOTO wa MAMA". Kitendo hicho ni cha Ushujaa kwani MACHAWA (WATOTO wa MAMA)wanataka kumchonganisha MH.RAIS na WANANCHI kwa kumtengenezea MAKUNDI.Lengo la hawa MACHAWA ni kujinufaisha wao Kama KIKUNDI kumpitia Mh. RAIS Nakupongeza sana Mh.RAIS kuliona hilo.

Niwakumbushe MACHAWA Kazi kubwa anazozifanya Mh.RAIS SAMIA ziko wazi kila Mtanzania anaziona na wala hazihitaji WAPIGA DEBE Muacheni Mh.RAIS afanye kazi zake na VYOMBO HUSIKA vitazitangaza KAZI zake. Watanzania hatuhitaji MAKELELE yenu.

Kuonyesha kuwa MH.RAIS hataki UNAFIKI wenu amesema HANA na HATAKI MAKUNDI.
 
Wadau nawasabahi.Nichukue Nafasi hii kumpongeza Mh.RAIS SAMIA kuwakataa HADHARANI MACHAWA wote wanaojiita "WATOTO wa MAMA".Kitendo hicho ni cha Ushujaa kwani MACHAWA (WATOTO wa MAMA)wanataka kumchonganisha MH.RAIS na WANANCHI kwa kumtengenezea MAKUNDI.Lengo la hawa MACHAWA ni kujinufaisha wao Kama KIKUNDI kumpitia Mh.RAIS
Nakupongeza sana Mh.RAIS kuliona hilo .
Niwakumbushe MACHAWA Kazi kubwa anazozifanya Mh.RAIS SAMIA ziko wazi kila Mtanzania anaziona na wala hazihitaji WAPIGA DEBE Muacheni Mh.RAIS afanye kazi zake na VYOMBO HUSIKA vitazitangaza KAZI zake. Watanzania hatuhitaji MAKELELE yenu.
Kuonyesha kuwa MH.RAIS hataki UNAFIKI wenu amesema HANA na HATAKI MAKUNDI.
bila mbambamba wala shobo ya mtu yeyote,

Rais comrade Dr. SSH atasifiwa bara-bara mara nyingi zaidi kila anapofanya vizuri katika kila jambo linalowagusa Watanzania wote, apende, asipende atalazimishwa tu 🐒

na mimi na sema alazimishwe tu kupokea sifa na pongezi za waTanzania kwa kazi zake nzuri anazofanya,

kwan kuna ubaya gani ndugu mtoa hoja 🐒
 
Wewe mwenyewe umeanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais ,halafu wengine tukimpongeza Rais wetu mpendwa na jemedari wetu kipenzi cha watanzania unatuita chawa. Embu acha kujichanganya akili yako na kuwa na akili kama nyumbu wa CHADEMA
 
Wewe mwenyewe umeanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais ,halafu wengine tukimpongeza Rais wetu mpendwa na jemedari wetu kipenzi cha watanzania unatuita chawa. Embu acha kujichanganya akili yako na kuwa na akili kama nyumbu wa CHADEMA
Mwashambwa watu wanaingilia sana kazi yako humu sijui unafeli wapi 🤣🤣🤣
 
Pongezi nyingi Kwa kuhakikisha tunapata vitambulisho vya NIDA ,ilishindikana miaka 5 iliyopita Samia ameweza
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzania haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli amefariki, lakini spirit yake inaishi. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi, iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli amefariki lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana, usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili, lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli inaishi. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60 kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Pongezi nzuri Kwa Rais Samia kwenye sekta ya Afya

View: https://www.instagram.com/p/C4caIpKNKHk/?igsh=ZGxueDFraWZ6c2c3
 
Wewe mwenyewe umeanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais ,halafu wengine tukimpongeza Rais wetu mpendwa na jemedari wetu kipenzi cha watanzania unatuita chawa. Embu acha kujichanganya akili yako na kuwa na akili kama nyumbu wa CHADEMA
Chadema wanamtesa sana Lucas! Pole sana kuteseka. Ndio chama kubwa limebarikiwa na Mungu
 
Pamoja na pongezi nyingi kwa kazi nzuri inayo fanywa na Rais wetu mpendwa Mama wa Taifa letu, SSH, wananchi Wanamuomba Rais aongeze Ukali kwa watendaji wabovu,

inaonekana baadhi ya watendaji hawaendi bila mjeledi.


ukali kwenye mambo serious, mambo ya msingi sio mbaya

pamoja na kazi nzuri aliyo ifanya ndani ya miaka 3 tu, wananchi tunaamini endapo Mama ataongeza ukali mambo yatakuwa mazuri zaidi.
awe mkali kwa wabadhirifu wa fedha za umma, tusisubiri hadi wizi na ubadhirifu utokeee.
 
● Kwenye Sekta ya Kilimo Serikali ya Rais Samia imeongeza bajeti ya Kilimo kutoka Tsh. 751 mwaka 2022 hadi Tsh. bilioni 970.

● Kuongezeka kwa uzalishaji wa chakula Tani 17,148,290 hadi kufikia Tani 20,402,014 na kufikisha asilimia 124 ya kiwango cha utoshelevu wa chakula.

● Ameipatia wakala wa uhifadhi wa chakula NFRA na bodi na nafaka na mazao mchanganyiko (CPB) kiasi cha Tsh. bilioni 116.

● Ametoa ruzuku ya mbolea ya tani 204,818.16 kwa mikoa yote ya Tanzania yenye thamani ya Tsh. bilioni 67.82.

● Serikali yake imetenga jumla ya eneo lenye ukubwa wa ekari 201,241 kwa ajili kuwaingiza vijana na wanawake kwenye kilimo kupitia mradi wa BBT

● Serikali yake imeendelea kuwekeza katika Skimu za Umwagiliaji kwa kuongeza eneo kutoka hekta 727,000 hadi hekta 822,000.
 
Hongera sana mama kizuri Huwa kinajiuza.

Tanzania sasa ni namba moja duniani kwa furaha ya watu wake

Demokrasia nchini imepanuka hata kila mtu anatukana lakini hakuna anayemkamata

Sekta Binafsi imekua na pesa mtaani zimejaa.

Ajira kila Kona zimejaa
 
Back
Top Bottom