Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 31,913
- 65,514
Wasi kutishe, Raha ya bhangi changanya na Viagra
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huko hawana mabango ya kusifu binadamu wao kazi tu,wajinga mmebaki kusifu na kufisadiHongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.
Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:
Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzania haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.
Pili, Mzee Magufuli amefariki, lakini spirit yake inaishi. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi, iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli amefariki lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana, usicheze nalo.
Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili, lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli inaishi. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.
Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60 kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.
Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Hii kejeli hii!Heshima sana wanajamvi,
Kwakuwa sasa ni sehemu ya utaratibu katika uendeshaji wa shughuli za Serekali kunasibisha kila jambo jema na jina la Mheshimiwa Dr Samia Suluhu Hassan nimeona ni vyema tukatanua utaratibu huu kwa kuyabadili majina baadhi ya maeneo yetu kama Hifadhi ya Serengeti tunaweza tukiita.
1. Dkt. Samia National Park jina la Serengeti tukaaachia wamaasai watajua wakapolipeleka.
2. Ziwa Dr Samia au Lake Dr Samia Suluhu Hassan badala ya Lake Victoria.Waingereza watajua watakalipeleka jina la Malkia wao.
3. Mt Dr Samia au Mlima Samia jina la Kilimanjaro limekaa kichagga sana na linaleta ukakasi sana.
4. Sarafu zetu zote tuweke picha ya Dr Samia uenda ikakoma kuporoka thamani yake dhidi ya Usd.
Mungu wa mbinguni akubarikiPuuzi flan hivi
Utatu wa Uzalendo:Ipende pia CCM, ni baraka tosha!
Cc Lucas MwashambwaHilo ni ombi langu kwa Watanzania wote na Mungu wa mbinguni atawabariki sana
Nawatakia Dominica Njema 😄