Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Nasikia kuna wataalamu wa kucheza na mita za mafuta pale, kuna ukweli wowote juu ya hili?!
 
Kuna ukame ktk hazina ya dola... Serikali haina Money !! Ndo wanafanya uvamizi huu...badala ya kuomba kwa hiyari!!!!
MAHANJU huoni sherehe zimefutwa.....
 
Last edited by a moderator:
Mheshimiwa Waziri Mkuu..

Najua wapo baadhi ya wasaidizi wako wanachungulia chungulia Humu Jamii Forum


Tafadhali nakuomba usikie kilio chetu sisi vijana mafukara tulio wanyonge huko kwenye hiyo mifuko kama jina lako halianzii na Peter au Thomas au Magdalena huwez kufikiriwa hata kuitwa kwenye usaili.

Mfano hata ukiangalia Board members ya PPF na GEPF woote Takriban ni Wakristo pamoja na Top Management Yoote ya PPF kuanzia kwa GD Urio kushuka chini...

Nchi hii ni yetu soote na soote tuna haki sawa katika ajira.

Muislam kupata kazi kwenye mifuko hiyo ni ndoto.

Zaman walikua wanasema hatuna elimu lakn sasa siyo kweli hoja hiyo.

Tunaomba uliangalie hilo.

Shukran.



Hebu KWANZA check NSSF, halafu ndo uje vizuri na maoni yako
 
Ama kweli kuishi kwingi kuona mengi. Yanayoendelea sasa nchini kwetu ni sawa na njia za mkato za kunyanyua uchumi alizokuwa anatumia Dr IDDI AMIN DADA wa Uganda
usishutuke kesho ukasikia wahindi na wapemba wanaandamwa. Kila la heri

Pole. Rais anazuia utajiri haramu, upo hapo.
 
Kuna ukame ktk hazina ya dola... Serikali haina Money !! Ndo wanafanya uvamizi huu...badala ya kuomba kwa hiyari!!!!
MAHANJU huoni sherehe zimefutwa.....
Mirija yote ya walaji milungula ikibanwa tutakua na dola za kutosha na thamani ya shilingi itapanda.
 
Last edited by a moderator:
Neno la leo linatoka katika kitabu cha Watanzania sura ya tano mstari wa pili hadi wa sita.

2.Nao Watanzania waliokuwa katika kifungo cha umaskini waliposikia matendo yake Magufuli, walituma watu kumuuliza 3.Wewe ndiye ajaye, au tumtazamie mwingine? 4.Na saa ile alikuwa ametoka kutumbua majipu kadhaa, ndipo alipowajibu akawaambia, E nendeni mkawaeleze Watanzania mnayoyasikia na kuyaona; 5.Wagonjwa Muhimbili wanalala juu ya vitanda, safari za nje zimekatwa, vigogo wanapigwa chini, majipu yanatumbuliwa hata yale ambayo hayajaiva, na watu wameanza kuisoma namba!
6.Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami.
 
Mh Rais kwenye uingizaji wa mafuta ya vyombo vya moto pale Bandarini pia kuna uozo mkubwa uchunguzi wa kina ufanyike.
Baadaye ntatolea ufafanuzi pia jinsi wamiliki wa mashule wanavyopitisha vifaa vya ujenzi pale Bandarini bila kutozwa kodi kwa madai kwamba wanajenga shule kumbe wana ni wamiliki wa mahardware makubwa mijini kwa ajili ya biashara tu.

Kwenye mafuta ndiyo balaa kubwa zaidi.

Magufuli akiwafungia kazi huko, nina uhakika vituo vingi vya mafuta mitaani na kwenye barabara kubwa vitajifunga vyenyewe.

Kuna mchezo mchafu sana. Mafuta yanatolewa kama yapo transit lakini yanaishia kwenye vituo vyetu. Sijui hili watalifanyia akili gani. Kama kuna njia ya kutenganisha mafuta yakutumika Tanzania na yale ya nchi za jirani ingekuwa jambo muafaka kabisa.

Kituo cha mafuta ya transit kiwe peke yake na mbali ya kituo cha mafuta ya Bongo. Sina uhakika na namna ya kutekeleza hilo
 
Kwenye mafuta ndiyo balaa kubwa zaidi.

Magufuli akiwafungia kazi huko, nina uhakika vituo vingi vya mafuta mitaani na kwenye barabara kubwa vitajifunga vyenyewe.

Kuna mchezo mchafu sana. Mafuta yanatolewa kama yapo transit lakini yanaishia kwenye vituo vyetu. Sijui hili watalifanyia akili gani. Kama kuna njia ya kutenganisha mafuta yakutumika Tanzania na yale ya nchi za jirani ingekuwa jambo muafaka kabisa.

Kituo cha mafuta ya transit kiwe peke yake na mbali ya kituo cha mafuta ya Bongo. Sina uhakika na namna ya kutekeleza hilo
Mafuta ya transit yasafirishwe kwa malori yenye rangi maalum, yakikutwa vituoni tu..
 
Ajipange aweke mambo sawa kila sekta ili huuu ushenz uishe km kweli anamaanisha hii biashara ya kuruka huku na kule haitomfikisha popote
 
Mafuta ya transit yasafirishwe kwa malori yenye rangi maalum, yakikutwa vituoni tu..

Nchi ilikuwa imetawaliwa sana na rushwa.

Tulikuwa tunaelekea kuwa kama Italy. Matatizo waliyoachiwa na Silvio Berlasconi itachukua miaka mingi kutoka humo. Rushwa ilianzia juu hadi chini. Mpaka leo , wanapata shida kukusanya kodi.

Magufuli anahitaji hadi mwaka mzima kwa uchache kuweka mambo sawa kabla hatujaona matunda halisi.
 
Magufuli majipu hayo majipu tumbuaaaaa......aliselemaa Khadija aliselemaa magufuli selema,selema selama.
 
Wana JF.

Hii kampuni inaitwa GOOD ONE ni kampuni kubwa inayoongoza kwa kuuza vifaa vya ujenzi Tanzania kwa hivi sasa.

Hawa GOOD ONE uwa wanaleta meli nzima ya tiles-na vifaa vingine kama masinki, mabomba, vitasa, rangi.

Tiles zote za kariakoo wanauza wao mmiliki wake wa hii kampuni ni mchina.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom