Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Kama amekupa ujumbe umfikishie magufuli basi mwambie akupe na njia ya kuonana nae ili umfikishie ujumbe alio kupa
 
Bwana Yesu Asifiwe!

Unajua Dira Yote Ya Tanzania Ya Kesho Mungu Amewapa Watumishi Wake. Hivyo Viongozi Ni Muhm Sana Kuwa Karibu Na Watumishi Ndipo Watakapoweza Kufikia Malengo.

Nami Nikiwa Kama Mchungaji Mungu Amenipa Ujumbe/ushauri Kwa Rais Magufuli Juu Ya Tanzania Ya Kesho.

Yaan Nataka Hata Mtu Atakaeweza Kulipia Kipindi Kwny Media, Au Anikutanishe Na Mwandishi Wa Habari Awe Ananihoji.
Au Kama Wewe Ni Mwandishi Wa Habari Ebu Tuwasiliane Kwa Cm No.0786100772,au 0757856336.

Maana Tanzania Inayotajwa Ya Mwaka 2025 Haiwezi Kufikiwa Paspo Kujua Mpango,na Mambo Mungu Ameyakusudia Yafanyike.
Ninaomba Iyo Neema Na Kibali Kwa Mamlaka Ya Jina La Yesu Kristo.

Huo ujumbe andika jhapa, atauona
 
Kama amekupa ujumbe umfikishie magufuli basi mwambie akupe na njia ya kuonana nae ili umfikishie ujumbe alio kupa



Inabidi Niutoe Akiwa Anasikia,au Niutoe Kupitia Vyombo Vya Habari Ambapo Baadae Angeuckia, Yote Hayo Yanawezekana.
 
ajitenganishe ili atokee mtu kama lowasa alivyotaka kumfanyia jk! pamoja na urais siasa ziko palepale.
 
Kwa nini hata umpe ushauri/ utoe rai wakati wewe ulishajipambanua kuwa si mwana CCM?

Mimi nataka huyo Magufuli afeli kabisa katika utawala wake ili watu waisome namba kwamba CCM siyo suluhisho la matatizo ya kiuchumi waliyonayo.

Nataka huyo bwana awe rais wa muhula mmoja tu.

Hivyo kamwe sitampa ushauri wowote ule utakamfanya aboreshe utawala wake.

I want him to fail.
 
Mag3,

..umesikiliza hotuba yake ya kushukuru?

..alianza vizuri akizungumza lugha ya usuluhishi.

..akamaliza na lugha ya kibabe na mikwara: "uchaguzi umekwisha na Raisi ni John Pombe Magufuli, na Makamu ni Samia.."

..kwa kweli kuna umuhimu wa kupatikana watu kumsaidia Dr.Magufuli kuelekeza mikwara na ubabe wake kule kunakostahili.

..sidhani kama kwa hali ya kisiasa nchini Dr.Magufuli anatakiwa kutumia ubabe na mikwara ku-deal na vyama vya upinzani.
 
Last edited by a moderator:
Yote safi na kama ni mpenda watu, nadhani atapokea ushauri wako. Wasiwasi wangu ni kupokea ushauri kwenye namba 9. Matusi na tambo ya kina Mkapa ni woga wa utekelezaji wa kuweka mikataba kuwa wazi.
 
Andika tu hapa kile ambacho unataka kusema kwa Rais. It is simple as that.
 
Inabidi Niutoe Akiwa Anasikia,au Niutoe Kupitia Vyombo Vya Habari Ambapo Baadae Angeuckia, Yote Hayo Yanawezekana.

Ndugu mchungaji ngoja nikushauri jambo mimi pia ni mtuishi kama wewe ila haya uliyoyaandika humu JF umepotea njia. Utahishia kupata kejeli na matusi tu nibora hata ungeenda kwenye magazeti ya serikali kama mzalendo na uhuru labda utakuwa mwanzo mzuri wa kupata nafasi ya kumuona Dr.Magufuli Huku JF kuna wapenzi na mashabiki tu wa Lowasa na Magufuli pamoja na puplic figure wengine. So utakacho ambulia nikuitwa mnywa Viroba.hilo moja lapili kama wewe ni mtumishi wa Mungu sidhani kama unahitaji vyombo vya habari viwepo wakati unatoa ujumbe wako kwa Rais kama vile Nathani alipotumwa na Mungu kupeleka habari kwa Daudi hakukuwa na vyombo vya habari ila Roho Mtakatifu pekee. Ubarikiwe mtu wa Mungu. ila hapa siyo mahala pake.
 
    1. Usikubali kofia mbili; wewe ni Raisi, uenyekiti wa CCM muachie mwingine ili chama kibaki chama na serikali ibaki serikali.
    2. Washauri Wabunge wa CCM, watangulize maslahi ya taifa mbele ya maslahi ya chama.
    3. Washauri Wabunge wa CCM kama itawezekana wamchague Spika wa Bunge asiyeegemea upande wowote.
    4. Pokea ushauri kutoka kwa vyama vya siasa lakini uwe huru kufanya maamuzi kulingana na matakwa ya Katiba ukizingatia maslahi ya wananchi.
    5. Usiruhusu Ikulu kutumika kwa maslahi ya CCM, vikao vya chama vifanyike nje ya Ikulu.
    6. Washauri CCM waachie mali za wananchi kwa kuzirudisha mikononi mwa wananchi kupitia serikali.
    7. Agiza vyombo vya dola vitoe haki sawa kwa wananchi bila upendeleo.
    8. Futa sheria zote kandamizi zinazozuia uhuru wa kutafuta, kupokea na kutoa habari. Vyombo vyote vya habari viwe huru.
    9. Hakikisha mikataba yote tunayoingia inawekwa wazi ili vijadiliwe na kupitishwa na Bunge.
    10. Vikumbushe vyombo vya dola kwamba jukumu lao la kwanza ni kuwalinda Watanzania na mali zao na si kupambana nao.


Huwezi kumtenganisha magufuli na ccm.2017 anachukua chama ili asafishe mafisadi waliobaki katika ccm.halafu wewe ni chadema unapata wapi ujasiri wa kumfundisha kazi rais alietoka ccm.
 
Mungu ulionana nae wapi mpaka akakupa huo ujumbe ?
 
Inabidi Niutoe Akiwa Anasikia,au Niutoe Kupitia Vyombo Vya Habari Ambapo Baadae Angeuckia, Yote Hayo Yanawezekana.

jf pia ni chombo cha habari kwa hyo itoe tu ...au kwa tafsiri yako wewe chombo cha habari lazima iwe ni tv na redio huku umezungukwa na maiki za waandishi wa habar
 
jana alienda wizara ya fedha bila shaka leo ataenda hapo nje ya ikulu wizara ya elimu, jitahd kukaa getini pale wizara ya elimu saa tano asbh tunakuja nae
 
Wewe kama nani hata utoe ushauri kwa Magufuli?

Tuondokee hapa.

Mtoa uzi katoa ushauri wake kama raia wa jamhuri ya muungano wa Tz, basi atakuwa rais fazafoxy umshauri wewe,
 
Fuata utaratibu (ITIFAKI izingatiwe), huna haja ya kumwaga mtama mbele ya kuku hapa; wengine wataukanyaga tu na mwishowe hutaonekana mwenye HEKIMA.

Wewe kama Mchungaji, huna viongozi wako wa juu katika kanisa lako; taasisi inayotambulika rasmi serikalini? Huna Askofu Mkuu ambaye kwa nafasi yake anayo heshima na kibali kwenda ikulu, na hata anakutambua wewe?

Kuleta hoja yako hapa sio tu hujatumia hekima ya kiuchungaji, bali pia unafunua siri unazopewa uwape watu wa Mungu wahusika.
Uwe mwangalifu ili usije kupoteza kuaminika kwako (trust) kwa waamini wasije kuwaza unatoa siri zao nje ya chumba cha ushauri.

Naomba kuwasilisha, asante
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom