Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
HATERS AKA WAGONJWA WAMEANZA TENA! UKIWA HAMUISHIWI VITUKO!
 
Ulisubiri umaarufu wake ushuke ndio ukiri kuwa umaarufu wake ulikuwa juu?
Hakuna ubishi kwamba umaarufu wake ulikuwa juu na alianza kuonekana ni kimbilio la wanyonge.
Katika shughuli zangu za kutafuta maisha, napita sana mikoa mbalimbali. Tofauti na ilivyo kuwa Mwezi January kwa mfano ambapo Magufuli alikuwa na approval ratings kubwa sana, kila muda unavyozidi kwenda, anaporomoka. Sidhani kama mna muda wa kujiuliza Kwanini. To put it in a nutshell, ukistaajabu ya awamu ya nne, utayaona ya awamu ya tano.

Matatizo yapo matatu:
Mfumo
Mfumo
Mfumo.
 
Matatizo ya nchi yapo Matatu
LUWASSA
LUWASSA
LUWASSA
 
badala ulete mada za maana we unakaa kujadili umaarufu wa magufuli....wanaume wa dar bhanaa!!
 
Matatizo ya nchi yapo Matatu
LUWASSA
LUWASSA
LUWASSA

-Escrow ya IPTL?
-Mmesikia escrow mpya ya songas gas, zaidi ya escrow ya IPTL?
-Serikali kuchukua mkopo wa zaidi ya Trilioni 21 kwa miaka mitano tu (2009-2013), zaidi ya jumla ya deni la taifa kuanzia 1961 hadi 2008, TZS Trilioni 15 tu kwa miaka 47 ya uhuru, mnafumua zaidi ya hizo miaka mitano tu?
-Lugumi?
-Kodi za home HSC hasara zaidi ya TZS Trilioni nane? Na kawajengea ukumbi wenu mpya wa dodoma? Anakarabati Lumumba, anamjengea kigogo hekalu Masaki? Yumo Kinyerezi 2?

Richmond kawaambia ni ya nani, na mnashindwa kumpeleka mahakamani kama alivyoomba ambapo Mngepata credit kwa kudhihirishia umma kweli mmedhamiria majipu?

Hadi Leo bado tatizo la taifa mnaaminishwa ni Lowassa?
Ama kweli awamu ya nne ilikuwa ni ya nguvu za giza.
 
Wazee wa kuzungurusha mikono wanaungaunga hoja kweli ...kazi yao ni kuhamisha magoli ....unahitaji kuwa kichaa kuwaamini leo ....JPM anapiga kazi tumpe muda ...
Wazee wa kugawa muda... Mlimpa Nyerere.... Mkampa mwinyi..... Mkampa tena Mkapa.... JK na sasa mnampa Magufuli!!!

Waafrika muda kwenu ni kama peremende tu kugawa hamuoni shida ila kwa wenzetu muda ni Mali kuliko dhahabu ukiwapotezea hata dakika unakwenda na maji....

Mtaendelea kugawa muda huku majira yakiwakimbia kwa kasi.
 

Mwaka huu peke yake serikali itakopa 7 trillions ktk benki za biashara kwaajili ya budget ya 2016/17 nawaza trend hii ikienda mfululizo kwa 3 years itakuwaje kwenye deni la taifa?
 
umaarufu wowote wa ghafla huwa sio mzuri kwa kuwa hukosa misingi ...ni vigumu kujenga umaarufu kwenye level ya urais kwa kutegemea juhudi binafsi badala ya mfumo...kwahiyo mleta mada kaleta maono ambayo ni obvious
Kwa maneno yenu kuntu hamteuliwi tena hata ka ukuu wa kijiji. Achilia mbali udisii
 
Well said mkuu[emoji122] [emoji122] . Dah ubarikiwe sana..
 
Mwaka huu peke yake serikali itakopa 7 trillions ktk benki za biashara kwaajili ya budget ya 2016/17 nawaza trend hii ikienda mfululizo kwa 3 years itakuwaje kwenye deni la taifa?
Kwa kipindi chake chote, Magufuli atatumia kodi za wananchi kulipa madeni yanayoiva kuliko kutumikia walipa kodi kwa njia ya huduma za kijamii nk. Mwaka huu peke yake, trillion sio chini ya nne zinatakiwa kulipwa ndio maana ukiangalia mapato ya kodi ya Mwezi, so far zaidi ya nusu yanaenda kulipa madeni pekee yake. Swali la msingi ni je TZS Trilioni zaidi ya 21 zilizokipwa kwa miaka mitano tu (2008-2013) zimefanya nini? Nyingi Zimeenda mfukoni kwani tumeshaona Magufuli akitenga fedha kwa ajili ya miradi ambayo ilishatengewa fedha bajeti iliyopita. Wanasema wao walikusanya TZS billioni 900 kwa Mwezi. Je zilifanya nini? Wanahamisha goli.
 

KUNA KITU NAKIONA SIO SAWA KWA NAMNA GHAFLA MZEE WA RUANGWA ALIVOKUWA KIMYA GHAFLA...PENGINE MZEE HAKAI SAWA NA WATENDAJI...UNAJUWA UNAPOKUWA NA BOSI AMBAYE NI WA KULAUMU TUUU......UNAOGOPA HATA KAZI YENYEWE..........TUSUBIRI...TUONE...SIJUI HUYU ATABADILISHA MARA NGAPI KABLA YA SYSTEM KUMZUIA
 
NATIONAL CONCLUSSION; RICHMOND ni ya RICHARD WA MONDULI......aka LUWASSA....LUWASSA...LUWASSA...
 
Hata walimu tu wana kitu kinaitwa lesson plan.Sasa wewe hauna hata dira wa plan yoyote,unaamka asubuhi hujui unaenda wapi wala hujui hiyo siku utafanya nini,unaanza kuingia kila eneo unalokutana nalo mbele yako,mara hotelini,mara sokoni,mara CRDB,mara kuangalia mechi kwenye banda na huko kote hata hujui unaenda kufuata nini ili mradi tu kwamba huna plan,unategemea huo umaarufu utadumu kwa muda gani?
 
Nani alikuambia aligombea nafasi ya Rais wa Tanzania ili awe maarufu?

Siku hizi ujinga unageuzwa na kuwa hekima na busara!

Hata shetani ni maarufu sana hapa duniani na mbinguni.

viwavi mna sura nyingi mno,mnabadilika kama kinyonga.Ni majuzi tu mlikuwa mnakuja na nyuzi zinazoonesha umaarufu wa Magu nchi za watu hasa kule nigeria,kuna kipindi hadi TBC waliripoti juu ya umaarufu wa Magufuli kule nigeria.Wengi mlijaa humu ni kusifia tu kwenda mbele.Leo mtu kaona umaarufu umeshuka mnabadilika na kusema hakugombea kuwa maarufu.Mnasimama wapi?Uzi huu ungekuwa unasema umaarufu wake umepanda wala tusingewaona kusema hayo kuwa magu hakuchaguliwa kuwa maarufu,mngesifia.Kazaneni,mshapewa green light kuwa business as usual,ukitoa mishipa na povu sana,udc huooooooooooo.
 

ipo siku tutaamka tusikie yuko kwenye foleni ya kununua luku,mizuka aliyosema Sugu ndio hii
 
Kama ilikuwa Neyma,Suarez na Messi basi Atletico (Mafisadi) wameshawanyamazisha tayari imebaki historia
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…