Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Pesa za field bado wanafunzi hawajapewa,kisa ni wanafunzi hewa!Uhakiki ulishafanyika sasa mnadanganya nini?Serikali kama imekwama iseme
 
hahahah tena unajitambulisha kuwa ni kada wa ccm.....
mimi naomba ajira zisitolewe maana maofisini hamna kazi mtaongeza expenditure tuu za chai navikorombwezo

ISOME NAMBA kwanza........au fyatua ndugu yangu muda unaenda.
 
Pesa za field bado wanafunzi hawajapewa,kisa ni wanafunzi hewa!Uhakiki ulishafanyika sasa mnadanganya nini?Serikali kama imekwama iseme

Serikali haina hela kwa vitu/mambo ya maana ila ina hela kwa mambo yasiyo na tija na kwa wakati husika.
 
Dogo ulikuwa mnafiki sana kwenye kampeni za CCM mwaka jana.Ulifikiri maisha ya chuo ndio sawa na ya kitaa.Sasa mtaani kumekunyoosha naona umetulia kimyaaaa!!Naona hata ya bundle siku hizi imekuwa mgogoro.

Tuendelee kuisoma namba kidogo
 
You will never reach your destination if you stop and throw the stones at every dog that barks!
 
Kwa waliosoma form two Civics mtakubalia na Mimi kuwa kuna topic za
Constitution
Law
Democracy
Sioni faida ya hizi topic tena kuendelea kusomwa darasani wakati mtaani uwezi zitumia yaani haziwezi Fanya kazi kwa maana ya uhalisia kuwa hivyo vitu havifuatwi!!

Hivi mwalimu bado anasimama na kumfundisha mwanafunzi eti
Democracy is a power of the people by the people for the people?
Akija mtaani anaweza Ku apply hii definition vipi?

Hakuna haja ya watu kuangaika kusoma vitu ambavyo uwezi Ku apply kwenye maisha ya kawaida!!!

Nashauri Ndalichako na wengine waondoe hivi vitu kwenye mtahara waweke topic ya Magufuli watoto wamsome Rais wetu mwema wamjue vizuri katika kipindi hiki !!;
Unafikiri mnachambua mambo kwa makini mmenielewa!!
 
Rais na Serikali yako,wananchi wako tunauliza bila kukuchukiza. Vipi kuhusu ajira ulizozisitisha bila kutisha nchi nzima kwenye sekta ya umma? Kupanda na kushuka vyeo kulisitishwa;kuingia na kutoka ajirani kulisitishwa.

Kulitangazwa kwa kushangaza miezi miwili. Miezi ya uhakiki wa uhakika wa wafanyakazi hewa na hai. Miezi miwili imekwisha. Watumishi hawajapanda vyeo,hawajapata nyongeza za mishahara wala ajira mpya kuanza. Vipi?

Wasomi walishaomba kazi. Wakaitwa kwenye usaili. Na hata wengine kuitwa kazini. Lakini,tangazo la Serikali liliwapa maumivu makali. Walilazimika kurejea walikotoka bila kutaka kwakuwa ajira zimesitishwa. Kikatiba,kuajiriwa ni haki. Kwanini ukimya huu?

Wananchi wanaomba bila kugomba majibu mujarabu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Vumilieni Watanzania wenzangu... mniamini, sitawaangusha! Kwanza tulikuwa tunafanya ukaguzi wa wafanyakazi hewa, tukaja wanafunzi hewa na hivi sasa tunakagua Watanzania hewa ili tutakapotangaza ajira, tuhakikishe hatuajiri Watanzania hewa! Lakini na wewe sio Mtanzania hewa wewe? Mbona kimbelembele sana!!!
 
Asipoajiri hadi wakati wake unaisha mtamfanya nini?
 
Rais na Serikali yako,wananchi wako tunauliza bila kukuchukiza. Vipi kuhusu ajira ulizozisitisha bila kutisha nchi nzima kwenye sekta ya umma? Kupanda na kushuka vyeo kulisitishwa;kuingia na kutoka ajirani kulisitishwa.

Kulitangazwa kwa kushangaza miezi miwili. Miezi ya uhakiki wa uhakika wa wafanyakazi hewa na hai. Miezi miwili imekwisha. Watumishi hawajapanda vyeo,hawajapata nyongeza za mishahara wala ajira mpya kuanza. Vipi?

Wasomi walishaomba kazi. Wakaitwa kwenye usaili. Na hata wengine kuitwa kazini. Lakini,tangazo la Serikali liliwapa maumivu makali. Walilazimika kurejea walikotoka bila kutaka kwakuwa ajira zimesitishwa. Kikatiba,kuajiriwa ni haki. Kwanini ukimya huu?

Wananchi wanaomba bila kugomba majibu mujarabu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Mungu anamuona maskini sisi dhaambi
 
Kuna baadhi ya watanzania ni wakuwaacha mana bado wanatumia maneno ya kwenye Biblia ngoja tuwe nasubira hadi yesu atavyorudi mara oooh namwachia mungu siku zote wanyonyaji na watenda maovu huwa wanapenda kutumia maneno ya Mungu kuwapumbaza wasiojitambua...Rais yupo mapumziko baada ya Ukuta kuchafua hali ya hewa waendelee kusubiri kama yesu alivyowaahidi wana wa Israel
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom