Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Ninawaza tu.
1. Aseme maji ya chumvi mwisho na sasa hivi maji yatatoka mabomba yote Dar es Salaam na mikoa yenye shida ya maji.
2. Afanye waendesha mipikipiki wawe na mfumo wa kueleweka maana barabarani hawataondoka. Arasimishe sekta ya bodaboda.
3. Awaambie wasaidizi wake wafanye maamuzi na kusimamia na si matamko.

Watanzania mniombee, msema kweli mpenzi wa Mungu.
 
Ningependa aongelee changamoto zinazokabili taifa kwa sasa kama bandari kukosa mizigo huku bandari nyingine zikipokea mizigo mingi, aelezee watanzania hili jambo limesababishwa na mambo gani, na litatatuka lini kwa mipango ipi, hawezi akasema waache wasije kwa sababu hawalipi kodi, wakati bandari tunaihitaji itupatie fedha na ajira, je hizo bandari nyingine zinazopokea mizigo mingi ni kuwa hawalipi kodi?
Kingine ni kauli za vitisho kwa raia na wapinzani hazina tija, wapinzani wafanye mikutano yao ila wakiongea maneno ya kichochezi basi wachukuliwe hatua.

Pia atuambie hili ongezeko la watu kutokuwa na kazi linatatuka vipi maana biashara zinavyokufa na ndivyo ajira zinakufa kwa spidi kubwa zaidi, sio aseme watu wafanye kazi wakati mtaani hakuna cha ku stimulate watu wafanye kazi kwa kuwa mtu huwezi fanya uwekezaji, kilimo ukaajiri kwa kuwa fedha mzunguko umekuwa mdogo
 
Mheshimiwa rais najua kuwa unalo tatizo la kutosikiliza ushauri ila naamini walau utasikiza mara hii moja. Ni hivi, najua kuwa unatamani sana ufanye jambo ambalo vizazi na vizazi vitakukumbuka na kukusifu. Tatizo ni kuwa hadi sasa hujaamua ni jambo lipi ufanye.

Mheshimiwa mkapa atakumbukwa kwa uwanja mpya na daraja la mtwara.
mheshimiwa kikwete atakumbukwa safari zake za nje na pia kuweza kuunganisha Tanzania yote kwa barabara za lami.

Mheshimiwa wewe hadi sasa unakazana kung'ata kuliko uwezo wa mdomo wako kutafuna. Mara mgambo wasisumbue mama ntilie,mara wakuu wa mkoa watengeneze madawati, mara mahakama ya mafisadi, mara fly over, mara daraja busisi, mara kufagia, mara boti ziwa victoria, mara mahakama ya mafisadi, mara kuhamia dodoma.....list is endless.

Pamoja na utitiri huu wa mambo hakuna hata moja lililokamilika hivyo yote yataishia kuwa ubatili tu!
Ushauri wangu ni kuwa hebu achana na yote hayo....wewe kazana na jambo moja tu lililo ndani ya uwezo wako kama vile kuhakikisha usafi unafanyika kisawasawa na watu wanaoga kila siku.
 
hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa watu kuoga kila siku,😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀😀
 
Hakuna namna ndo serikali ilivyo.
.itatuchukuwa muda kupata maendeleo maana no developmental plan kila siku ni jipya
 
Mheshimiwa rais najua kuwa unalo tatizo la kutosikiliza ushauri ila naamini walau utasikiza mara hii moja. Ni hivi, najua kuwa unatamani sana ufanye jambo ambalo vizazi na vizazi vitakukumbuka na kukusifu. Tatizo ni kuwa hadi sasa hujaamua ni jambo lipi ufanye.

Mheshimiwa mkapa atakumbukwa kwa uwanja mpya na daraja la mtwara.
mheshimiwa kikwete atakumbukwa safari zake za nje na pia kuweza kuunganisha Tanzania yote kwa barabara za lami.

Mheshimiwa wewe hadi sasa unakazana kung'ata kuliko uwezo wa mdomo wako kutafuna. Mara mgambo wasisumbue mama ntilie,mara wakuu wa mkoa watengeneze madawati, mara mahakama ya mafisadi, mara fly over, mara daraja busisi, mara kufagia, mara boti ziwa victoria, mara mahakama ya mafisadi, mara kuhamia dodoma.....list is endless.

Pamoja na utitiri huu wa mambo hakuna hata moja lililokamilika hivyo yote yataishia kuwa ubatili tu!
Ushauri wangu ni kuwa hebu achana na yote hayo....wewe kazana na jambo moja tu lililo ndani ya uwezo wako kama vile kuhakikisha usafi unafanyika kisawasawa na watu wanaoga kila siku.
Hapa naomba nimtetee Mtukufu Raisi.Flyover tayari mkandarasi na kazi imeanza,ATCL marubani wanakwenda Canada karibuni,Mahakama ya mafisadi majaji wapo Lushoto wananolewa.Naamini miaka miwili au mitatu ijayo atakuwa na cha kuwaonyesha wananchi na kujivunia.Tusijidanganye kuwa hakuna kinachofanyika!!!
 
Dah ...Rais wangu wa moyoni...
Lala nao mbele mafisadi, wala rushwa na wazembe kama ulivyotuahidi......Tupe raha sisi wanyonge, wavuja jasho, wazalendo na waadilifu....kutesa kwa damu [emoji4] [emoji4] [emoji41]
 
Aache UCCM akumbuke yeye ni Raic wa WTZ.

NA UONGO PIA AACHE. sababu ya wabunge kutolewa nje tunaifahamu ( ni kuuliza maswali kuhusiana kashfa ya Lugumi na Uuzwaji wa nyumba za serkal) sio awasingizie et ndyo wanakwamisha ujenzi wa viwanda.
 
tumechoka kupewa siasa kila siku ,
mkuu wa nchi yetu akiwa jukwaani anatupa siasa sijaona hata moja linalotekelezwa zaidi ya akipanda jukwaani nikutupa ahadi za kwenye kampeni,tanzania ya viwanda,tufyatue watoto wakati mashirika yake yakipoteza pesa nyingi kutuhamasisha tupange uzazi ,
muheshimiwa hatuhitaji siasa tunahitaji uende kuzindua miladi uliyo ahidi siasa zifike mwisho
 
Kwa hilo la kufyatua watoto namuunga mkono, wakina mama mguuuu upande, tunayo kazi moja tu ni kufyatua watoto
 
Tunahamia dodoma jaman where are you guys?
Tulieni tuhamie huko mengine baadae!!
 
SERIKALI ITOE AJIRA MPYA KWA VIJANA WALIOHITIMU VYUONI MWAKA JANA ILI KWENDA SAMBAMBA NA KAULI MBIU YAKE YA HAPA KAZI TU.

Sometimes najiuliza hivi ni kweli Serikali ipo serious kabsa?,hivi unawezaje kushughulikia watumishi hewa Kwa zaidi ya miezi 8?. Suala la watumishi hewa ndio imekuwa kama Kikwazo kikubwa na kisingizio kubwa cha serikali kusitisha Ajira mpya,upandaji wa madaraja kwa watumishi wa umma, uhamisho na nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma.Mheshimiwa Rais wetu aliahidi suala la kushughulikia watumishi hewa lisingeweza kuchukua zaidi ya miezi miwili na sasa ni zaidi ya miezi miwili bado ajira amezuia kwa visingizio vilevile.Vijana waliohitimu vyuoni tangia mwaka jana wapo Mitaani tu wakisubiri serikali itoe ajira, kipindi cha mwanzo serikali ilikuwa inasingizia suala la bajeti,Waziri mkuu alitoa ahadi serikali itatoa ajira mpya baada bajeti kupitishwa mwezi wa saba, baada ya Bajeti kupitishwa serikali ikatoa sababu ya watumishi hewa.

Sio busara kwa serikali kuendelea kuzuia ajira mpya kwa vijana waliohitimu vyuoni halafu wakati huohuo inahamasisha Hapa kazi tu.Ni wajibu wa serikali kuhakikisha Vijana wanaostahili ajira serikalini wanapewa ajira ili kuenda sambamba na kauli mbiu yake ya hapa kazi tu.Namuomba Sana mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Magufuli atoe kibali cha ajira maana kuhusu hili yeye ndiye mhusika mkuu.

Mwisho, namuomba sana Mheshimiwa Rais wetu Dkt John Pombe Magufuli akumbuke ahadi zake kipindi cha kampeni mwaka 2015 kuhusu ajira kwa vijana.Namuomba pia mheshimiwa Rais wetu Mpendwa Dkt John Pombe Magufuli atuambie watanzania hili suala la uhakiki wa Watumishi hewa litaisha lini maana ndio sababu aliyotumia kuzuia ajira mpya, lakini pia atuambie watanzania athari zitakazotokea kama serikali ikitoa ajira mpya wakati zoezi la uhakiki wa Watumishi hewa likiwalinaendelea.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu ibariki Afrika.

Wako,
Abel Magembe Lugimba.
Kada wa CCM kutoka mkoa wa Rukwa, Tanzania.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom