Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Wana bodi nawasalimu.....

Naanzisha uzi huu ili tuweze mshauri mh. Raisi (kwa nia njema kabisa) katika utendaji wa kazi zake wa kila siku.... hapa unaweza weka kero yako na ushauri wowote unavo ona mambo yanapaswa kwenda.... Kama ni ofisini kwako, mtaani nk.... nia ni kumpa yeye urahisi wa kujua watz wanafikilia nini na wanataka nini.....

Ushauri wangu:

Wakati CAG anasema pesa za maendeleo kapelekewa sh 0 mpaka sasa hivi.... taasisi nyingi na wizara zinakumbana na adha hii.....

Ugawaji wa pesa kwa utaratibu wa sasa unafanya baadhi ya taasisi zisizo kuwa usoni au karibu nae kuto pewa kipaumbele kabisa.... mfano kuna kazi za ujenzi wa nyumba wa baadhi ya taasisi na wizara ulianza tangu mwaka wa fedha 2012/13, umesismama kabisa na wakandarasi wako site kwa muda wote huo maana pesa haiendi kabisa... yawezekana sio kipaumbele chake kwa sasa.... kwa nn asingemaliza hizi kazi za zamani maana ziko kimkataba na kuanza upya kwa utaratibu wake wa kuwatumia TBA... watu wanakufa kwa pressure, mabank yanadai na kuuza mali zao .... wakandarasi wanafilisika na kupoteza mitaji waliyo ijenga kwa miaka mingi .... watoto hawaendi shule.... na ni watz wanao teseka zaidi maana watz wana hulka ya kuto pambana na serikali kufuata mikataba....

Ningeshauri bajeti kama ilivo pangwa na bunge itumike hivo kuondoa
matatizo ya pesa za maendeleo kuto enda baadhi ya taasisi au wizara....

Nakaribisha Maoni na ushauri wowote wa kujenga taifa letu kwa Mkuu wetu....
Je atausoma huu uzi ama kushaurika kukataza mikutato ya kisiasa inatosha kujua kwamba hataki kushauruka (usiwe una twanga maji kwenye kinu)
 
Siku tutakayoamua kama watanzania kuongelea vipaumbele vyetu na namna ya kuvifikia itakuwa mwanzo wa hatua za uhakika!HAKUNA shaka kwamba tunahitaji.

1. Maji ya uhakika-hii itasaidia jamii yote yaani wakulima (umwagiliaji), ufugaji,viwanda na maisha kwa ujumla

2. Usafiri/miundombinu- hii itasaidia mtawanyiko wa bidhaa kwa bei nafuu na kwa urahisi hivyo kupunguza makali ya maisha kwa raia

3. Umeme wa uhakika- huu utasaidia viwanda,elimu,afya na sekta nyingine
Lazima tuzungumzie haya na tuyafanye kwa nguvu zetu na Mali zetu zote!Otherwise tutaendelea kuimba wimbo wa Bashite,TLS,usaliti na kila aina yake unaopigwa mbele yetu.
 
Bila kupoteza mda, Mheshimiwa Rais Magufuli usiamini watu wako kupita maelezo na pia sikiliza ushauri wa watu.

Kusikiliza ushauri haina maana lazima uwe ule unaopewa na washauri wako bali maoni ya watu mbalimbali na wengine hatuko huko serikalini.

Tukio la video mpya kutoka radio ya mawinguni linakuchafua wewe moja kwa moja na nikutokana na kutosikiliza sauti za watu, wengine wakiwa mawaziri wako.
Wapo walioamua kukaa kimya, pia ukimya wao ulikuwa ni ushauri kwako lakini uliwapuuza kutokana na imani yako kwa 'dogo' au sababu zingine unazojuwa wewe (inawezekana ni ungumi jiwe).

Natambua pia tukio hili linaweza kuwa ni kijisababu cha kumtema 'dogo' ili kuuwa soo la makaratasi tunayopewa baada ya kumaliza shule halafu wale watu wa mawinguni akamalizane nao pembeni.
 
Enzi hizo kulikuwa na chuo cha kufunza makada wa chama ambao baadae walipatikana viongozi wenye busara na heshima kuongoza serikali na mashirika ya umma,kwani bwana wewe huyu mtoto wa jicho ulimfukua dampo gani!
 
Bila kupoteza mda, Mheshimiwa Rais Magufuli usiamini watu wako kupita maelezo na pia sikiliza ushauri wa watu.

Kusikiliza ushauri haina maana lazima uwe ule unaopewa na washauri wako bali maoni ya watu mbalimbali na wengine hatuko huko serikalini.

Tukio la video mpya kutoka radio ya mawinguni linakuchafua wewe moja kwa moja na nikutokana na kutosikiliza sauti za watu, wengine wakiwa mawaziri wako.
Wapo walioamua kukaa kimya, pia ukimya wao ulikuwa ni ushauri kwako lakini uliwapuuza kutokana na imani yako kwa 'dogo' au sababu zingine unazojuwa wewe (inawezekana ni ungumi jiwe).

Natambua pia tukio hili linaweza kuwa ni kijisababu cha kumtema 'dogo' ili kuuwa soo la makaratasi tunayopewa baada ya kumaliza shule halafu wale watu wa mawinguni akamalizane nao pembeni.


Hiyo video haitoshi, wekeni maongezi yote aliyoyanena. Hakuna ukweli wa maneno yanayoandikwa.

Ni kiongozi na lazima alindwe na polisi.

Makonda oyeeeeeee
 
Mheshimiwa rais Magufuli, huu ni waraka wangu kwako:

Sasa hivi upo katika kuinyoosha nchi, ilikuwa inajiendea tu, watumishi walifanya kazi kwa mazoea, viongozi nao vivyo hivyo, wanaccm alkadhalika.
Mheshimiwa umejitoa mhanga, ni lazima upambane kweli kweli, hasa na watu wa kutoka kwenye chama chako ambao wanajitahidi kukukwamisha kwa kuwa unagusa maslahi yao au ya wafadhili wao au jamaa zao.

"Hapo kwenye kamati kuu, mpaka halmashauri kuu tengeneza vichwa vyako, vyenye maslahi ya chama na nchi kwa ujumla wake, na pale bungeni yule katibu wa wabunge wa ccm akufai, alitakiwa yeye ndiye angemwajibisha mapema kabisa yule mbunge wa CCM aliegawa muda kwa wapinzani, wewe ungepata taarifa tu, hao ndio wachawi wenyewe.

Katika nafasi zako za kuteua wasaidizi, usisikilize mpinzani kasema nini au kataka nn, we angalia utaemteua atakusaidia vipi maadam hauvunji sheria za nchi, watasema mchana usiku watalala.

Mwisho baba angalia wachapa kazi, usiangalie elimu zao, au vyeti vyao, "Mwalimu Nyerere alipomchagua mheshimiwa Kawawa kuwa waziri mkuu, sio kama akuwaona wasomi akina Oscar Kambona, Sir Kahama n.k bali alimchagua kutokana na imani yake, uadilifu, utiifu na kuyasimamia vyema maagizo ya rais wake"

Kwahiyo baba unaowateua, au kuwapitisha katika nyanja mbalimbali za uongozi, akikisha unapitisha watu watakaosimamia na kutekeleza maagizo yako na ilani ya chama chako.
 
Mkabila, mbaguzi, chuki, visasi, roho mbaya hawezi fanikiwa kwa chochote sababu ya hila zake
 
Mheshimiwa rais Magufuli, huu ni waraka wangu kwako:
Sasa hivi upo katika kuinyoosha nchi, ilikuwa inajiendea tu, watumishi walifanya kazi kwa mazoea, viongozi nao vivyo hivyo, wanaccm alkadhalika.
Mheshimiwa umejitoa mhanga, ni lazima upambane kweli kweli, hasa na watu wa kutoka kwenye chama chako ambao wanajitahidi kukukwamisha kwa kuwa unagusa maslahi yao au ya wafadhili wao au jamaa zao.
"Hapo kwenye kamati kuu, mpaka halmashauri kuu tengeneza vichwa vyako, vyenye maslahi ya chama na nchi kwa ujumla wake, na pale bungeni yule katibu wa wabunge wa ccm akufai, alitakiwa yeye ndiye angemwajibisha mapema kabisa yule mbunge wa ccm aliegawa muda kwa wapinzani, wewe ungepata taarifa tu, hao ndio wachawi wenyewe.

Katika nafasi zako za kuteua wasaidizi, usisikilize mpinzani kasema nini au kataka nn, we angalia utaemteua atakusaidia vipi maadam hauvunji sheria za nchi, watasema mchana usiku watalala.
Mwisho baba angalia wachapa kazi, usiangalie elimu zao, au vyeti vyao, "Mwalimu Nyerere alipomchagua mheshimiwa Kawawa kuwa waziri mkuu, sio kama akuwaona wasomi akina Oscar Kambona, Sir Kahama n.k bali alimchagua kutokana na imani yake, uadilifu, utiifu na kuyasimamia vyema maagizo ya rais wake"
kwahiyo baba unaowateua, au kuwapitisha katika nyanja mbalimbali za uongozi, akikisha unapitisha watu watakaosimamia na kutekeleza maagizo yako na ilani ya chama chako.
Huu sio ushauri bali ni kujipendekeza kwako, hakuna ushauri wa hovyo kama huu unao tekelezeka na mwenye akili
 
Ateue watu wake kwasababu nchi na chama ni mali yake....
Asiangalie vyeti wala elimu ya mtu yeye ateue tu....
Mwalimu Nyerere alipomteua Kawawa alikuwa ana degree ngapi kwa majina tofauti?
Nani anapinga Rais kumteua mtu asiye na vyeti?
 
Hii thread iwe Maalum kwa Maoni, Ushauri na Mapendekezo mbalimbali kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Mimi namuomba, Mheshimiwa Rais mteuliwa, kwa heshima na taadhima hili ni ombi binafsi kwako.

Nnaomba uhakikishe huyu mrembo wa ACT Bi Anna Mghwira unamuingiza bungeni na unampa wadhifa anaostahiki, huyu mama ni kichwa adhyim na adim kabisa.

Nimemfatilia mikutano yake mingi sana ya kampeni, anatoa vitu kichwani utafikiri ana word processor inayopanga na kuchuja anachokizungumza kutoka kichwani bila kusoma.

Halikadhalika leo kanifurahisha sana alipostukizwa na kutoa hotuba pale Diamond, ilikuwa fupi na imelenga points zote nzuri na ameeleweka vyema kabisa.

Anna heko sana na nitakuunga mkono katika siasa zako.
























Mshauri afukuze makonda
 
Ukibeba gunia la kimba lazima majimaji yakuchuruzikie mwilini

La bashite tayari,magunia bado yako mengi
 
Mheshimiwa rais Magufuli, huu ni waraka wangu kwako:

Sasa hivi upo katika kuinyoosha nchi, ilikuwa inajiendea tu, watumishi walifanya kazi kwa mazoea, viongozi nao vivyo hivyo, wanaccm alkadhalika.
Mheshimiwa umejitoa mhanga, ni lazima upambane kweli kweli, hasa na watu wa kutoka kwenye chama chako ambao wanajitahidi kukukwamisha kwa kuwa unagusa maslahi yao au ya wafadhili wao au jamaa zao.

"Hapo kwenye kamati kuu, mpaka halmashauri kuu tengeneza vichwa vyako, vyenye maslahi ya chama na nchi kwa ujumla wake, na pale bungeni yule katibu wa wabunge wa ccm akufai, alitakiwa yeye ndiye angemwajibisha mapema kabisa yule mbunge wa CCM aliegawa muda kwa wapinzani, wewe ungepata taarifa tu, hao ndio wachawi wenyewe.

Katika nafasi zako za kuteua wasaidizi, usisikilize mpinzani kasema nini au kataka nn, we angalia utaemteua atakusaidia vipi maadam hauvunji sheria za nchi, watasema mchana usiku watalala.

Mwisho baba angalia wachapa kazi, usiangalie elimu zao, au vyeti vyao, "Mwalimu Nyerere alipomchagua mheshimiwa Kawawa kuwa waziri mkuu, sio kama akuwaona wasomi akina Oscar Kambona, Sir Kahama n.k bali alimchagua kutokana na imani yake, uadilifu, utiifu na kuyasimamia vyema maagizo ya rais wake"

Kwahiyo baba unaowateua, au kuwapitisha katika nyanja mbalimbali za uongozi, akikisha unapitisha watu watakaosimamia na kutekeleza maagizo yako na ilani ya chama chako.


Matumaini yangu pia lazima akaze buti Rais wetu.

JPM oyeeeeeeee
 
Makada wanavamia ofisi za watu na SMG halafu unamwambia mwenyekiti afanyeje? CCM mna matatizo makubwa sana ya akili
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom