Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Katiaka nchi ambazo hazina maendeleo makubwa kama Tanzania ni kitu muhimu sana kuangalia media inafanya nini. Media zinaweza zikatumiwa vibaya kama Rais mwenyewe ulivyosema. Pia tusipende kuilinganisha Tanzania na nchi zilizoendelea tunaweza pata shida kubwa, kwani wananchi wengi hawana elimu ya kuwafanya wawe na reasoning character hiyo unayo ifikiria.

Ni kweli media inaweza kutumika vibaya kupotosha. Lakini inaweza pia kutumika kuelimisha na kunyoosha mambo. Huu uwili (dichotomy) upo kwenye mambo mengi na chaguo letu kuendeleza yale mazuri na kuondoa mabaya kwa kuhakikisha sheria na taratibu zinafuatwa.
 
Sawa, tunapo zungumzia katiba lazima pia tuzingatie uwepo wake ili kujua kuna manufaa gani kwa nchi na watu wake. Katiba ni paper work ambayo inalindwa na mihimili hiyo mitatu; serikali, Bunge na Mahakma. Kuna nchi duniani hazina katiba kwa mfano England na kuna nchi nyingine kama Kenya ambako katiba ipo na wamejaribu kui-reform kuwa kama ya Amerika, lakini je imesaidia kitu chochote? Mimi naona ukabila bado upo pamoja na katiba mpya.
Hili ni hitaji muhimu mno! Linaweka mazingira ya usalama wa nchi kwamba hata kama atakuja kiongozi mbovu bado nchi inabaki salama! Paper work ndiyo na kweli inalindwa na mihimili yote iliyo huru. Kama mihimili hiyo siyo imara na huru basi haisaidii kuweka checks and balances zinazotakiwa.
 
Tusiwe na Illusion ya kuamini kuwa maandishi peke yake yatatusidia kuwa na viongozi bora kama watu wenyewe hawafuati kanuni zake. Nikupe mfano, CCM inakatiba nzuri sana ambayo ilitengenezwa na waanzilishi wa nchi yetu. Uliona mambo yaliyo tokea kwenye CCM ya awamu ya tatu na ya nne? Kuna mambo ya rushwa yameandikwa humo, kuna maswala ya uteuzi wa viongozi yameandikwa huko, lakini je CCM ya awamu ya tatu na ya nne iliyazingatia hayo? Mafisadi wengi walikuwemo kwenye hicho chama mpaka Rais Magufuli alipo ki-reform.
Naomba tuachane na ndoto za mchana kinacho takiwa hapa mabadiliko ya mind set na maendeleo ya mtu binafsi.
Tatizo la kudorora kwa maendeleo ya nchi yetu ni tatizo la kudorora kwa CCM. kudorora kwa CCM kumetokana na kutokuwepo kwa ushindani wa kutosha katika siasa zetu. Kuna haja ya kuweka mazingira ya kuchochea ushindani katika siasa zetu ili ziwe SIASA SAFI.
 
Yaani hii ni theory isiyekuwa na msingi. Of cause serikali inweza kujiingiza katika shughuli ya uzalishaji.
Sikiliza mkuu Ujerumani inamiliki kwa asilimia kubwa Railway yao ya Deutsche Bahn pia kampuni ya magari ya Vokswagen shirika la ndege la Lufthanser na kadhalika kuna hathari zipi zimetokea?

Kipindi cha nyuma serikali ya uiingereza nilisikia ilijaribu ku-privatize Railway yao na shirika la umma la kuzoa taka. Waulize waingereza mambo yaliyowakuta ni yapi? System zao za uendeshaji wa treni mbaya kupindukia. Amerika nako hivyo hivyo. Nenda Kaangalie system ya treni Germany, Sweeden, Switzerland na Ufaransa, utaona tofauti kubwa sana. Hapo ndipo utaona tofauti kati ya private na Parastatal institutions.

Msipende tu kubwabwaja vitu "just for the sake of" kubwabwaja, angalieni mifano iliyopo. Ethiopia Airline mbona ina fanya vizuri? Liko chini ya nani?

Tukija Tanzania Reli yetu ya kati na viwanda vingi ambavyo Rais wa awamu ya kwanza alivianzisha na baada ya serikali ya awamu ya tatu ku-privatize, viko wapi? Na sasa Rais Magufuli ana anza upya tena kuvifufua. Huyu jamaa sio wa kucheza naye ni mzalendo haswa. Amekaa serikalini akisoma matendo yote maovu yaliyo tokea. Anajua nini anafanya na wapi kuna udhaifu.
Reli hakuna mtu binafsi mwenye uwezo wa kujenga na kuendesha. Hivyo Serikali lazima ifanye kile ambacho sekta binafsi haiwezi kufanya. Lakini tujiulize, kuhusu ndege: kuna tija gani ambayo tunaipata sasa hivi baada ya kununua ndege ambayo tulikuwa hatuipati kabla? Jibu ni hakuna na hivyo hizo hela ni bora tungezielekeza kwenye SGR. Lakini kwa vile tumeshanunua nashauri hivi:
Dreamliner inahitaji kuwa hewani angalau masaa 4000 kwa mwaka (just to to break even), assuming itakuwa imejaa abiria. Tupate route mbili au tatu za kujaza hayo masaa na zaidi. Dar - Dubai - Guangzhou, Dar - Dubai - Ankara, Dar - Dubai - Bombay. Route zote hizi ni za wafanyabiashara, wanakuwa na mizigo, hivyo provision kwa ajili hiyo sina hakika imewekwa kwenye confuguration ya ndege hiyo. Then tuuze hizo route kwa wafanyabiashara wetu na wengineo. Tuwaondoe kwenye Emirates, KQ, Etihad n.k. tuwarudishe wote nyumbani. Ili kuwavututia wazambia, Malawi, wakongo nk. kupanda ndege yetu ni lazima ijengwe network ya kuwafikisha kwao (connecting flights)
 
Hapo hata mimi nakuunga mkono. Hapa simweelewi Rais vizuri. Kitu gani kina mshinda kutawanya pipe lines ya gesi asilia Dar es salaam na miji mingine ambako kuna gesi asilia kama Mtwara, Lindi na kadahalika, watu wakawa na Energy ya kutosha kupikia badala ya kutumia mkaa? Energy sio umeme tu. Makaa ya mawe, Geothermy na kadhalika.
Mji kama Dar es Salaam ni sehemu chache sana inafaa kuwekwa miundombinu ya ges . Asilimia karibia 90 haijapangwa. Na sioni juhudi zozote za kulipanga hili jiji. DISASTER!!
Nchi yetu inageuzwa kuwa jangwa kwa sababu ya nishati ya mkaa na DSM ndo haswa mtumiaji mkuu wa mkaa by far. Kwa hiyo faida ya kulipanga jiji ni pamoja na kunusuru nchi yetu kuwa jangwa.
 
Tuna poteza mabilions na mabilions za fedha kwenye mabarabara na ma-flyovers tunashindwa ku-invest kwenye chip energy? Kwa mfano, kulingana na mahesabu yangu tuna hitaji umeme Tera Watt 10 ambazo ni Mega Watt 10,000.
Kulingana speech ya Rais mwenyewe, amesema umeme wa Stiegler utata Mega Watt 2100 yaani Tera Watt 2.1 na huu tulio nao Tera Watt 1.7, kwa pamoja utafanya Tera Watt 3.8.
Rais Amesema pia kwenye General reserve tuna kama bilioni sita hivi US Dola, katika hizo akichukua bilioni nne tuna Pata umeme wa Tera Watt 5, kwani mtambo mmoja wa G&S-Circle una cost milioni $15 nao utazalisha umeme wa Mega Watt 20. Kwa hiyo katika Tera Watt 5 tutaagiza mitambao 250 ya G&S-Circle. Tayari tuna Tera Watt 8.8. Huu umeme utatuwezesha kusambaza kwenye miji yote mikubwa na kwenye Standard gauge yetu. It is so easy. Hatuwahitaji wachina wala Wajapan. Tunafanya sisi wenyewe. Izingatiwe kuwa wauzaji watatuletea ma-specialist wao wanne au watano mengine yote ni kufuata instractions tu. Watanzania wazalendo tunaweza utaalam tunao. Serikali ituite tu kama iko tayari.
Ongeza na Economics, economics!!
 
Msipende tu kubwabwaja vitu "just for the sake of" kubwabwaja, angalieni mifano iliyopo. Ethiopia Airline mbona ina fanya vizuri? Liko chini ya nani?
Hii inasaidia nini kwenye mjadala huu?
Nguvu ya tusi haiwezi kufunika utupu wa hoja!
 
FISIEM msimu wa JIWE MALAIKAmkuu imeamua kutumia asset za CDM maana wafia chamaFISIEM wote ni mazganyanga tu. hawafai hata kuwasimamisha kugombea ujumbe wa mtaa. kwa wewe NZOGERA ndo kabsaaa hata kufuta vumbi viatu vya bwanaenu ndo utaona kwe picha tu[emoji12] [emoji574] [emoji61]
kuna jembe lingine CDM limeunga mkonokiwunomakaliomiguu ya MALAIKAJIWE juzi tu sasa tusubiri wafia FISIEM kama akiteuliwa FISIEM yeyote kugombea nafasi hiyo mnijuze na mie niwaunge makalioyenyu.
Nguvu ya tusi haiwezi kufunika utupu wa hoja!
 
Tunakuomba ifike wakati tutambue kwamba sisi bado ni tegemezi kwa asilimia kubwa sana kwahiyo hatuwezi kusema kibaya au kufanya kibaya kwa tunaowategemea.

Tunaotaka kushindana nao wana nguvu kubwa wakati sisi ni wanyonge hakika tunajiumiza wenyewe na kusimamisha maendeleo yetu nyuma na kuyarudisha nyuma kabisa.

Mwl.Nyerere kusema hafungamani na upande wowote wakati nchi ni changa kimaendeleo alikosea sana.

Kwako mkuu kiongozi wa nchi,kiongozi wa serikali,Amiri jeshi mkuu,kupingana na kutokua karibu na nchi za magharibi ni kutunyima fursa wananchi na kutuongezea matatizo tunakuomba jumuhika nao ili Tanzania iende mbele.
Tunaaamini wewe ni Raisi bora tunaomba uonyeshe ubora wako.
Wanasema" kama una msitu mkubwa unataka kuchana mbao na huna vifaa na aliyenavyo pekee ni yule jirani uliyekorofishana nae Jana basi yajengeni ili wote mfaidike"
Hili ni Ombi mkuu sio ushauri
 
Tunakuomba ifike wakati tutambue kwamba sisi bado ni tegemezi kwa asilimia kubwa sana kwahiyo hatuwezi kusema kibaya au kufanya kibaya kwa tunaowategemea.

Tunaotaka kushindana nao wana nguvu kubwa wakati sisi ni wanyonge hakika tunajiumiza wenyewe na kusimamisha maendeleo yetu nyuma na kuyarudisha nyuma kabisa.

Mwl.Nyerere kusema hafungamani na upande wowote wakati nchi ni changa kimaendeleo alikosea sana.

Kwako mkuu kiongozi wa nchi,kiongozi wa serikali,Amiri jeshi mkuu,kupingana na kutokua karibu na nchi za magharibi ni kutunyima fursa wananchi na kutuongezea matatizo tunakuomba jumuhika nao ili Tanzania iende mbele.
Tunaaamini wewe ni Raisi bora tunaomba uonyeshe ubora wako.
Wanasema" kama una msitu mkubwa unataka kuchana mbao na huna vifaa na aliyenavyo pekee ni yule jirani uliyekorofishana nae Jana basi yajengeni ili wote mfaidike"
Hili ni Ombi mkuu sio ushauri
Hujui thamani ya kura yako!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom