Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
madhara ya DIVISION FIVE hajui majukumu ya makatibu na majukumu ya mawaziri, KATIBA YA NCHI NDO MWONGOZO WA NCHI, RAIS HAWEZI VUNJA KATIBA KWA MIHEMKO YAKO. .
 
Mashangingi yaondolewe tu, nina imani magufuli atalifanyia kazi hili kwani ana mzigo mzito sana wa kufanya mabadiliko ya kiuchumi, hivyo bila kunana bajeti zisizo za lazima malengo hayatatimia
 
kuna mtu nilikuwa namuelewesha kwamba hawa ndio wapiga kazi, Mawaziri ni kofia tu.

Sasa ni vizuri kuona watu wengine wanalifahamu hili.

Hawa Makatibu ndio wamezuia maendeleo ya watanzania, mtu yeyote juu ya Makatibu ni msimamizi wa sera ya Chama kilichomchagua, (na hao wasimamiaji sera huwa wanabadilishwa kama nguo)
 

Atakuwa amevunja Katiba.
 
Nashukuru kwa kuwa sauti zinazididi kuongezeka kuhusu jambo hili.Ni sawa kabisa,hamna haja kabisa ya mawaziri na manaibu wao.Kama kweli JPM anapenda well being ya wananchi wake aachane na watu hao.Ili fedha itakayokuwa saved iende kuwahudumia wananchi.Kwanza sio watalaam halafu wanaleta migongano isiyo ya lazima wizarani.Nashauri pia kusiwepo na Wakuu wa Mikoa na Wilaya.Makatibu tawala wanatosha.Ni vema tukaachana na siasa kwenye serious issues. Afterall we do not have the money to waste.
 
Atatumia katiba ipi? Mihemko soma kwanza katiba aliyoapa kuilinda inasemaje

Katiba iliyopo inampa muda ambao lazima awe ameteua PM, lakini haisemi hivyo kwa mawaziri wa kawaida. Ni vema akaiga rais wa Nigeria ambae kwa miezi kadhaa alifanya kazi bila mawaziri. Yeye ateue PM basi, wengine wasubiri.
 
Landrover 110 ndiyo mwisho wa mchezo. Zinafaa sana na zinavumilia shida na ni rahisi kulihudumia
 
Na kama utaamua kuziuza basi zisiuzwe kwa bei ya kuruka wala kwa kwa mtindo wa "Baba kanituma".Mchakato wote wa uuzwaji uwe wazi kama ni installment au vipi kama ni watumishi wa umma pekee au vipi.
 
Siku za Jumamosi, jumapili na Public Holidays zote gari za serikali iwe marufiku kuwa barabarani.

Zile ST zenye number za kiraia ziondolewe kuziba mwanya wa kukwepa hilo.

Kuna wakati akiwa waziri wa uchukuzi alijaribu lakini alizidiwa nguvu na wakubwa wake. Sasa yeye ndiyo top.
 
Hivi ndio vipimo vya kuonyesha kama JPM yuko serious na "hapa ni kazi tu" au la.Ni kweli madude haya hayana tija yeyote kwa taifa.Frankly ni sifa za kijinga.Watoto hawana madawati,akina mama wajawazito na waliojifungua wanalala chini,vijana wetu wamekosa mikopo,dawa mahospitalini hakuna,halafu wewe unatembelea shangingi ?!Una furaha gani hasa.Ni unafiki na ujinga mtupu.I hope raisi hatawarudishia hayo magari.Yauzwe na badala yake wapewe RAV 4 zinatosha sana. Harier zinakula mafuta.
 
RAV4 na Harrier haziwezi kumudu safari za vijijini rough road huko. Awanunulie landrover au toyota hardtop
 
Hivi ni nani alileta wazo la kutumia mashangingi serikalini?
 
Magufuli anza na baraza la mawaziri la watu kumi tu. Kusiwe na cha naibu waziri
 
Naunga mkono hoja, wanunue land rover 110 au land cruiser hardtop zinafaa sana kuhimili mikiki mikiki mazingira yoyote yale.
 

Nafikiri Suzuki na Landrover au gari ndogo yenye 4WD inatosha kabisa Mbona miaka hile ya zamani Suzuki na Toyota Passat zilifanya kazi vizuri sana na barabara nyingi zilikuwa mbovu,why now days with good road tunatumia mashangingi hili hali maisha yanakuwa magumu kwa wasio na kipato.Mi nafikiri maofisa wa serikali wapewe Pikipiki na suzuki au nature ya kazi landrover refeers those 19's good days, suzuki pikipiki na landrover inatosha sana, mtu atakayeona awezi tumia hivyo vifaa aache kazi wajiriwe vijana wasio na kazi.Mbona private sector kampuni binafsi na kubwa unakuta magari ni maliwi ya md na gm others wanatumia usafiri wao kutokana na kukopa.
 
Hoja yako inasaidia kupunguza matumizi na kuondoa siasa hata katika shughuli za maendeleo, napenda watu mnaofikilia beyond the wall, kila jambo linawezekana Chini ya jua, katiba inaweza kurekebishwa ili jambo Jema liingizwe, mbona huwa hamshangai viongozi wanapoweka pembeni na kufanya mambo yao ya kishenzi?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…