Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Waliokuwa wanamsifia JK ni watumbuaji wakuu waliokuwa karibu naye.

Unadhani ni watumbuaji tuu? Wapo hata wengine waliokuwa wanasukumwa na ushabiki tuu lakini ndugu zao ndio hao walikuwa wanakufa kwa vile mashine hospitalini ni mbovu na hela hawana za kupeleka AgaKhan. Hata hapa JF walikuwepo ila sijui kwa huu uzembe ambao tumeonyeshwa ndani ya siku mbili watakuwa na lipi la kusema.
 
Penye kusifia tusifie huyu mama ni hazina tuache siasa za maji taka.

Mim nilimpa kura yangu japo nilijaribu kushawishi watu lakin wakawa na vichwa vigumu...Ningekuwa ni uwezo wangu ningempa Uwaziri wa elimu
 
kama ilivyo wana ukawa kushangilia kauli za Kagame

Kama unamfuatilia Magufuli the way anavyo tenda utakubaliana na wapinzani kum support Paul Kagame. Hiyo ndio style ya PK, habari zilizo vuja ni kwamba hata mawaziri nao watakua kwenye kipindi cha matazamio ya miezi 6. Wapinzani kwa sehemu kubwa hua wanazungumza mambo ambayo yana masirahi kwa Watanzania wakati viongozi wengi wa ccm huzungumza mambo yenye either maslahi kwa chama chao or wao wenyewe. Kampeni zilizo muweka madarakani Ben Mkapa mwaka 1995 zilikua kali na za nguvu sana kwa ccm but Mkapa huyo huyo mwaka 2000 wala hakufanya kampeni za maana, kazi zake zilijionesha kwa wapiga KURA. Nakumbuka kuna wakati alikaa tu studio za RFA Mwanza na kupiga kampeni, sina hakika but i think hata bajeti yao ya mwaka 2000 ilikua ndogo sana, kampeni za jk mara zote na hasa ya mwaka 2010 wote ni mashahidi, nina hakika Pombe akienda kwa mwendo hu, uchaguzi wa mwaka 2020 anaweza hata kuamua kukaa tu studio ya television mojawapo nabkupiga kampeni na bado atashinda, JK aliiua kabisa ccm na ukweli ndio maana hata watu wanatilia mashaka ushindi because of him.
 
Mheshimiwa JPJM,

Naomba sana uangalie mfumo wa kila kitengo wizarani kujibadilisha kuwa "AGENCY" na "COMMISIONS". Hizi ni kama EWURA, TFDA, Government Chemist, TBS, TBA, TANROADS, TCU, etc. Sababu kubwa ni hizi:
  1. Hii imekuwa namna ya watu kujitengenezea mishahara mikubwa ya ajabu na marupurupu mengi yasiyo na tija.
  2. Vitengo vya huduma vimejigeuza kuwa vya biashara na kutoza wananchi gharama kubwa ili kujinenepesha
  3. Imesababisha mawakala hawa kuingiliana kwenye majukumu (hasa yale yanayoingiza kipato)
  4. Huduma za kudhibiti zinasababisha "conflict of interest" na kuathiri matokeo ya kumlinda mlaji (mwananchi)
  5. Nyingi ya hizo taasisi zimekuwa ndio njia ya mkato ya maafisa wizarani kujichotea fedha kwa ulaini
Nawasilisha
 
Udhaifu wa ccm haujifichi,Uchaguzi umeisha wamepata ushindi wa mezani.Lakini kila kukicha chadema,Mbowe ukawa.Mara viti maalumu,Vinawahusu nini nyie?
Acheni kuweweseka jikiteni kwenye kazi na mambo ya msingi kudhiirisha falisafa yenu ya #Kazitu
2020 Ndio kwanza tumeanza safari ya kuitafuta,Mmepoteza kujiamini kabisa mnaishi kwa hofu kila sekunde
Msaidieni rais Uchaguzi ujao mpate kura mwache kutegemea jeshi.La sivyo mtaishia njiani
Yapo mambo mengi ya kujadili kuhusu taifa ni ujuha kuijadili Ukawa/Chadema na ikulu ni yenu.Au hamjaamini kama Magufuli ndio rais?
Badilikeni acheni CDM ifanye kazi zake.Mpeni mwenyekiti wetu nafasi ya kuimarisha taasisi yetu 2020 mpigwe knock out ili mfute kama Zanzibar.
 
Wengi wetu tumeguswa na jinsi ulivyoanza kazi, all we can say is KUDO'S.

Kinachofuatia ambacho wengi tungependa kukiona, na ambacho ni rahisi sana kuonekana na kuacha alama ya kumbukumbu, ni hizi Shangingi zilizojaa mjini, kwakweli kwa wengi zinatuumiza kuona matumizi yake yasivyokua na ulazima sana hata kwa watu ambao si lazima sana kuzitumia kwani zinanyonya hazina yetu bila kua na impact yoyote.

Kwakweli gharama za kuzihudumia hata kuzinunua ni juu sana na badala yake, sisi wanyonge tunashauri magari mengine yasiyo ya anasa sana wapewe hawa wakubwa zetu hawa ili watutumike vyema.

Mkuu Magufuli kuna hizi Rav 4 hizi ama hata toyota harrier kwa wale wakuu kabisa zitawatosha kabisa walau tusave pesa watoto waende shule na tupate vitanda mahospitalini.

Wengi wetu, tunahamu kuziona hizi shangingi hizi zikifutika hapa mjini, hakuna haja ya kuishi maisha ya anasa namna hii wakati wengi wetu mlo wa siku ni wa mashaka.

Asante mkuu Magufuli, natanguliza shukrani.
 
Wengi wetu tumeguswa na jinsi ulivyoanza kazi, all we can say is KUDO'S.

Kinachofuatia ambacho wengi tungependa kukiona, na ambacho ni rahisi sana kuonekana na kuacha alama ya kumbukumbu, ni hizi Shangingi zilizojaa mjini, kwakweli kwa wengi zinatuumiza kuona matumizi yake yasivyokua na ulazima sana hata kwa watu ambao si lazima sana kuzitumia kwani zinanyonya hazina yetu bila kua na impact yoyote.

Kwakweli gharama za kuzihudumia hata kuzinunua ni juu sana na badala yake, sisi wanyonge tunashauri magari mengine yasiyo ya anasa sana wapewe hawa wakubwa zetu hawa ili watutumike vyema.

Mkuu Magufuli kuna hizi Rav 4 hizi ama hata toyota harrier kwa wale wakuu kabisa zitawatosha kabisa walau tusave pesa watoto waende shule na tupate vitanda mahospitalini.

Wengi wetu, tunahamu kuziona hizi shangingi hizi zikifutika hapa mjini, hakuna haja ya kuishi maisha ya anasa namna hii wakati wengi wetu mlo wa siku ni wa mashaka.

Asante mkuu Magufuli, natanguliza shukrani.

naunga mkono ushauri huu. faida zake zipo wazi kwa Taifa.
 
Fuatilia matumizi yake uone, kuna kila 7bu kuziondoa kabisa, kuna kibosile moja naona anaitumia kufanya mawindo
 
Wengi wetu tumeguswa na jinsi ulivyoanza kazi, all we can say is KUDO'S.

Kinachofuatia ambacho wengi tungependa kukiona, na ambacho ni rahisi sana kuonekana na kuacha alama ya kumbukumbu, ni hizi Shangingi zilizojaa mjini, kwakweli kwa wengi zinatuumiza kuona matumizi yake yasivyokua na ulazima sana hata kwa watu ambao si lazima sana kuzitumia kwani zinanyonya hazina yetu bila kua na impact yoyote.

Kwakweli gharama za kuzihudumia hata kuzinunua ni juu sana na badala yake, sisi wanyonge tunashauri magari mengine yasiyo ya anasa sana wapewe hawa wakubwa zetu hawa ili watutumike vyema.

Mkuu Magufuli kuna hizi Rav 4 hizi ama hata toyota harrier kwa wale wakuu kabisa zitawatosha kabisa walau tusave pesa watoto waende shule na tupate vitanda mahospitalini.

Wengi wetu, tunahamu kuziona hizi shangingi hizi zikifutika hapa mjini, hakuna haja ya kuishi maisha ya anasa namna hii wakati wengi wetu mlo wa siku ni wa mashaka.

Asante mkuu Magufuli, natanguliza shukrani.
Ma dealers ndio balaa. Yaani wanatoa commission kubwa wacha tu kwa maafisa wanaoagiza hizo gari na bei inakua na cha juu ile mbaya. kutokana na hivyo wanaagiza hata kama waziri mkuu pinda akikataa analetewa gari jipya kwa nguvu. sasa magufuli anachotakiwa kufanya ni kuchagua gari za kawaida kwa serikali halafu kama ni gari 100 agency ya serikali inaagiza yenyewe toka foreign supplier au kiwandani. hapo utabakiza hela ya kusomesha watoto na change kibao. utakata bomba la unyonyaji. hapa kazi tu itakua kweli.
 
Service yake ni nouma na ni Toyota tu sio vinginevyo yaani service tu unanunua IST

KWELI, servise ya V 8 , NI 3 million.....overhaul ya engine ni 45 million...unaongeza hapo 20 million inakuwa 65 million unapata double cabin mpya without vat for gvt and public use....ukiongeza hapo 11 miliion unapata full na kodi zote kama private use.......

hizi ngoma zenyewe ukiweka wese bovu tu kuna mawili...mashine kwishney au ikikuonea huruma haimuvu hata sentimita moja...

wajinga ndio tuliwao.....mjapan huangalia unachotaka ndo anakupa...
 
Kasi kubwa ulioanza nayo imetupa moyo mkubwa sisi wananchi Ni matumaini yetu mpaka 2025 spidi utakayomaliza itakuwa sawa na usain bolt amalizapo mbio zake.
kwa ushauri wangu ili kupunguza matumizi ya serikali Ni vizuri usiwateue mawaziri na manaibu waziri ili kupunguza mzigo WA serikali yako.

Fanya kazi na makatibu wakuu na manaibu wake ili maelekezo yako yatekelezeke moja kwa moja bila kuchakachuliwa na mawaziri na manaibu wake kwa sababu kiuhalisia makatibu na manaibu ndiyo watendaji wakuu na mawaziri na manaibu waziri wanabaki kutokuwa na kazi yoyote ya kufanya.

Na hili unaweza kulitekeleza kwa kuomba marekebisho ya katiba yafanywe na wabunge kwa kipindi cha sasa kwa kikao cha dharura.

Kwa kudhihirisha mawaziri na manaibu Ni mzigo angalia sasahivi kazi za serikali zinafanyika bila uwepo wao.
 
katiba ndo kila kitu mzee,, chamsingi ni kuteua viongozi ambao wataendana na kasi yake na kuleta maendeleo ya kasi kwa wananchi, ila awalipe mishahara stahiki ila mambo ya posho posho ndo awakatalie ktk serikali yake
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom