Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Hivi wabunge wa kuchaguliwa kutoka Zanzibar CUF wako wangapi? Nisaidieni jamani
 
Bora mimi naumia kidogo mana kura yangu cjawapa ccm kazi kwako uliewapa kura na ajira wanakutenga
 
Mh Magufuli. Salamu nyingi sana hapo ulipo. Sisi wapiga kura wako wazima.

Mh. tunakupenda sana na hatutaki ukosee. Hizi wizara zinakutosha na tunakuomba ufanye utafiti mzuri wa watu wa kuwaweka. Kuna watu wamechokwa na jamii, kamwe usiwaweke hao watakuharibia jina. Ukikosa watu nenda vyuoni na kwenye taasisi binafsi utapata watu wazuri wa kukupigia kazi. Hapa kazi tu

Maoni yangu


  1. Uchumi na fedha
  2. Utawala bora, uhusiano na uratibu
  3. Utumishi wa umma
  4. Mambo ya Nje na mahusiano ya Afrika mashariki/kikanda
  5. Mambo ya ndani
  6. Ulinzi na jeshi la kujenga taifa
  7. Afya na Ustawi wa jamii
  8. Maji, Nishati na Madini
  9. Biashara, Utalii na maliasili
  10. Muungano, Katiba na sheria
  11. Tamisemi
  12. Elimu , Mawasiliano na Teknolojia
  13. Ujenzi na Uchukuzi
  14. Ardhi, Nyumba na Makazi
  15. Kilimo, Ufugaji na Uvuvi

Wizara zenye kuhitaji manaibu ni- Naibu mmoja anatosha


  1. Uchumi na fedha
  2. Afya na Ustawi wa jamii
  3. Maji, Nishati na Madini
  4. Elimu , Mawasiliano na Teknolojia
  5. Ujenzi na Uchukuzi
  6. Kilimo, Ufugaji na Uvuvi


Mungu akubariki sana
Mwana Kolekole kwa Mtwangile wa Nyekwele
 

Kama huyu mama angepata nafasi ya kuwa kiongozi serikalini,naamini kabisa atasaidia kuleta mabadiliko chanya.
 
Raisi JPM kwa mujibu wa tume amepata kura kama milioni 8 na zaidi. Hizi kura ni za watanzania.
Tungependekeza Raisi akaunda Serikali ya watanzania kwa maana siyo serikali ya CCM. hayo ndiyo mabadiliko ya kweli.

Kuanzaia Bunge spika CCM naibu upinzani na wajivue uwanachama wa vyama vyawo
Taasisi zote za vyombo vyadola wasiwe wanachama wachama chochote
Vyombo vya dola ni Mahkama , Takakuru, Usalama wataifa, Jeshi la ulinzi, Polisi , vyombo vya sharia, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu wa wizara na wote wengine.


Wakurugenzi asichague yeye wacha bodi ya utumishi iwa chague kwa mujibu wa CV zao.

Mheshimiwa wacha mihimili ya taifa viwe huru .
Kumuingiza Dk Tulia na kumpa unaibu spika ni kulidhibiti bunge.

Inavytakikana hawa wote wawe hawana chama na wafanye kazi bila ya utashi wa siasa.


Mheshimiwa Magufuli lete mageuzi ya kweli.
Ukiwa na wana CCM kila pahala mambo yale yale. kama nyumba inavuja utahama kila chumba na utahamisha kila kitu nyumba itabaki kuvuja. Chakufanya weka paa jingine jipya.
 
Kuwa mwanachama wa chama cha siasa lipo kikatiba. Mtanzania yeyote ana haki ya kujiunga na chama, shirikisho au taasisi yoyote ilimradi tu afuate kanuni, taratibu na sheria. Au kujiunga na kikundi chochote kile kwa kufuata vitu nilivyo vitaja hapo.

Majaji, Mwanasheria mkuu, Makamishna, mkuu wa majeshi, mkuu wa jeshi la polisi na yeyote yule serikalini, hazuiliwi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
 
Ni jambo la kawaida kwa Vijana wa Leo kupita Na bahasha maofisini wakiomba kazi.
Aidha imefikia Wakati mpaka wazazi wanawahangaikia watoto wao kupata kazi au field sehemu tofauti tofauti,lakini pia tumeshuhudia Tanzania imekuwa I matumizi makubwa Sana ya kiutawala kuliko maendeleo mfano wakati WA MKapa alijitahidi wakurugenzi wakuu,wakuu wa majeshi walikuwa Na miaka 45-50 Ili watumikie nchi kipindi kirefu wakiwa Na nguvu Na ukifika mda wa kustaafu hamna wapi sijamaliza.
Wakati wa jk tumeshuhudia watu wanapewa vyeo wakiwa wazee Sana Na atastaafu muda mfupi Na kula pesa ya umma bure bila ya kuleta tija stahiki au ataongezewa umri wa kustaaf kwa kuona aibu ameteuliwa hv karibuni.
Namuomba Rais Wangu DR Magufuri teuzi zake ziangalie Hilo la umri Mdogo Na pia kutowaongezea muda wazee wote ambao Ni wakuu wa mikoa Na wilaya kwani Ni Wakati wa kupimzika Na kubaki Kama washauri WA ulinzi Na usalama Na kupisha promotion zifanye kazi Na kuajiri vinana wapya.
 
Nimeshangaa leo Waziri Mkuu ana miaka zaidi ya 50 anasema bado ni kijana..hivi ujana mwisho miaka mingapi?
 
Hawa vijana nao kwakweli awana nidhamu kabisa sijui ni kwa sababu ya improper preparation za uongozi, unstructured ascendency to leadership maana mtu anaweza kufika juu bila ya merit or whatever the cause; yaani bungeni leo imekuwa fujo kabisa wakati wa maswali kila upande, jamaa wana poor etiquette za leadership utadhani wako mtaani wabunge wanaropka ovyo 'wape somo hao'; and the likes of nonsense calls kwakweli ni aibu.

Halafu kuna tabia zinaibuka vijana sio watu wakutambua utaratibu wa sheria for them they think power is enough of an authority to demand ata kama lengo ni jema. Bado sana sehemu zenye mamlaka ya power za juu zibaki kwa wazee wasaidizi wawe vijana kusaidia ubunifu kuna sababu ya kuwafunza hawa vijana nidhamu za uongozi, namna ya kutatua matatizo ya jamii na humbleness.
 
Nasikitika kwamba Mgao imerudi lwa kasi pamoja na mvua kunyesha, tuliambiwa mabwawa yamekauka, sasa kwa sasa hatujaelezwa kama bafo hayajaa au kuna sababu mpya kama nguzo kudondoka na kazalika?
 
Ni kweli kabisa. Ulipokuwa unatuomba kura ulisema kuwa hawa Jamaa wa Tanesco siku zao zinahesabiwa. Iweje mvua zinanyesha, mabwawa yamejaa maji lakini tatizo la umeme uko pale pale. Hapa Mwanza maeneo ya Nyakato tangu saa 12.30 asubuhi walikata umeme na mpaka sasa saa 1.20 za usiku hawajarudisha umeme.Mhe. Rais umeme ndiyo kila kitu katika maisha ya binadamu na hasa wakati huu wa utandawazi. Nakuomba aliyekuwa Waziri wa Nishati usimteue kuwa Waziri na Mkurugenzi wa Tanesco avuliwe madaraka mara moja.
 
MSHAHARA wa RAISI na WABUNGE NA MARUPURUPU yawekwe wazi ili tujue sisi kama mabosi wao tunawalipa tsh..na POSHO ZA KUYAKALISHA MAKILIO TU ZIFUTWE kwan ni sehemu ya kaz kama hawatak wajadil huku wamelala.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…