Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
Hauwezi kutemgeneza viwanda huko mali za kichina kinavurunda mjini
 
Ktk eneo ambalo naona Magufuli akienda kufeli ni hili la viwanda. Inabidi atumie wataalamu kweli kweli, na siyo kufanya mambo kwa pupa au kisiasa.

Wazo la kuchukua hayo mashamba na viwanda toka kwa walioshindwa kutimiza masharti yake ni zuri na naliunga mkono asilimia mia.

Ila baada ya kuvichukua, what next? hapa ndo mawazo ya wataalamu yanahitajika sana. Kwa vyo vyote itakavyokuwa sitasapoti wazo la eti serikali ndo iviendeshe. Lengo iwe kutafuta mwekezaji mpya na si serikali kufanya biashara



Watu watamuingiza Magufuli bonge la mkenge
Why awanyan'ganye bila kuuliza nini kimewafanya washindwe?
je kina nani hao watakao pewa baada ya kunyang'anywa?

wata qualify vipi kupewa?

serikali ikiamua iviendeshe itaweza?
kwa miaka mingapi vitaweza leta faida?

huu mkenge ni mkubwa sana...time will tell....
 
ndio maana rais anataka viwanda viwe vingi
atakama hayo yapo nikwasababu hamna viwanda azam ndio monopoly na srkl inambembeleza
 
Itafika muda mtamwambia magufuli aweke idadi ya goli za kupiga wake zenu
 
Tunajiaminisha kwa matumaini yasiyokuwepo. Baadhi ya hivyo viwanda vilivyouzwa havipo tena au teknolojia ya wakati huo imepitwa na wakati...ni nafuu kujenga viwanda vipya kuliko kuvifufua hivyo! Kumbuka tuko katika mfumo tofauti wa kisiasa; serikali si mtendaji wa biashara. Sasa sijui mnataka huyo mwenye mali yake aliyoinunua kihalali na pengine kashindwa kuiendeleza afanyeje. Basi tukimaliza hayo ya viwanda turudi kwenye nyumba pia waliozibadilisha kinyume na mikataba wazirejeshe serikalini! Itaisha kutafutana uchawi. We shuold soldier on and build new industries with appropriate today's technology

Ni bora mtu kama wewe uwe kaburini huenda kuoza kwa mwili wako kutarutubisha ardhi yetu ya Tanzania kuliko kuwa na mtu mwenye mawazo kama yako humu JF.
 
kinga'amuz gan ambacho hawaonyeshi free channel?



Zuku Ni Mojawapo.

Lakini Hata Hao Walioweka Wameweka Tu Kama Kuvutia Wateja, Kinachotakiwa Ni Sheria Kabsa Iwepo. Unakumbuka Hata Azam Ilikuwa Bure, Baada Ya Wateja Kuongezeka Wakaweka Bei Lakini Ndogo Kuliko Vingine Na Wateja Walipoongezeka Zaidi Na Bei Ikapanda.
 
Watu watamuingiza Magufuli bonge la mkenge
Why awanyan'ganye bila kuuliza nini kimewafanya washindwe?
je kina nani hao watakao pewa baada ya kunyang'anywa?

wata qualify vipi kupewa?

serikali ikiamua iviendeshe itaweza?
kwa miaka mingapi vitaweza leta faida?

huu mkenge ni mkubwa sana...time will tell....

Hakuna kiwanda wala shamba litakalo rejeshwa serikalini kutoka kwa mmiliki wake wa sasa bila kwanza mmiliki huyo kuulizwa sababu za kushindwa kutekeleza masharti ya mkataba. Zoezi hili zima litafanywa na wataalam ambao wapo kwenye ofisi ya msajili hazina...hivyo hata kama alitumia kiwanda kama dhamana...yote hayo yatatazamwa.
 
Ni bora mtu kama wewe uwe kaburini huenda kuoza kwa mwili wako kutarutubisha ardhi yetu ya Tanzania kuliko kuwa na mtu mwenye mawazo kama yako humu JF.
Umemwelewa lakini au unahara tu,

Teknolojia tuliyonayo ni tofauti na wakati viwanda vinabinafsishwa ni bora kujenga vipya kwa teknolojia ya kisasa.

Ulichotakiwa wewe ni kutoa maoni yako kuanzia alipoishia badala ya kutoa matusi.
 
Ktk eneo ambalo naona Magufuli akienda kufeli ni hili la viwanda. Inabidi atumie wataalamu kweli kweli, na siyo kufanya mambo kwa pupa au kisiasa.

Wazo la kuchukua hayo mashamba na viwanda toka kwa walioshindwa kutimiza masharti yake ni zuri na naliunga mkono asilimia mia.

Ila baada ya kuvichukua, what next? hapa ndo mawazo ya wataalamu yanahitajika sana. Kwa vyo vyote itakavyokuwa sitasapoti wazo la eti serikali ndo iviendeshe. Lengo iwe kutafuta mwekezaji mpya na si serikali kufanya biashara

Shirika la nyumba la taifa (NHC) kwa data za December 2014 lilikuwa linaingiza Bilioni 9.763 kama wastani kila mwezi kama faida. Na ni shirika la umma hili 100%. Kabla hajaingia Mchechu...shirika hili hili lilikuwa likiendeshwa kwa hasara. Nafikiri unaelewa nini maana ya shirika kuendeshwa kwa hasara. Things have changed. Serikali inaweza kumiliki viwanda kwa kuajiri wataalamu kutoka sekta binafsi. Tatizo la hapa Tanzania....wale watu waliozoea sekta za umma ufanya kazi kwa mazoea sana...hivyo sio watu wa kuwatumia kwenye hivyo viwanda vitakavyoanzishwa. Ufumbuzi hapa ni kuchukua smart people kutoka sekta binafsi na kuwa absorb huku kwenye public sector...tutaona mabadiliko.
 
Mleta mada na wengineo naomba mtusaidie vigezo na mashariti vilivyotumika kugawa viwanda hivyo, yawezekana waliopewa walidanganya kuwa wana mtaji wa kutoka. Lakini hata kama waliambatanisha Bank statement na vitu vingine je havikuwa-verified?
 
Ktk eneo ambalo naona Magufuli akienda kufeli ni hili la viwanda. Inabidi atumie wataalamu kweli kweli, na siyo kufanya mambo kwa pupa au kisiasa.

Wazo la kuchukua hayo mashamba na viwanda toka kwa walioshindwa kutimiza masharti yake ni zuri na naliunga mkono asilimia mia.

Ila baada ya kuvichukua, what next? hapa ndo mawazo ya wataalamu yanahitajika sana. Kwa vyo vyote itakavyokuwa sitasapoti wazo la eti serikali ndo iviendeshe. Lengo iwe kutafuta mwekezaji mpya na si serikali kufanya biashara

Naam, serikali isijiingize moja kwa moja kwenye biashara, nakubaliana na wewe 100%,kwa sasa duniani nadhani ni China pekee(yenye ujamaa wa kweli),ambapo serikali inafanya biashara. Kwa kuwa sisi Ujamaa wa kweli umetushinda basi viwanda viwe vya umma kupitia PPP au Kiundwe chombo chenye meno ambacho kitaratibu kwa ukaribu Viwanda vyote kwa niaba ya Serikali. Kazi kuu ya Serikali iwe kutoa huduma.
 
Mheshimiwa rais, nikupongeze kwa juhudi zako tangu umeapishwa na watanzania tunakuombea afya njema na ulinzi wa mwenyezi mungu. Tunaomba serikali kupitia wizara yake ya makazi iangalie upya bei za kodi za nyumba kwa jiji la Dar.

Bei zimekuwa zikipanda kila kukicha bila utaratibu na hazilingani na ubora wa nyumba. Mbaya zaidi hakuna taasisi yoyote chini ya wizara ya makazi inayohusika kutatua suala hili.

Tunaomba wamiliki wa nyumba nao walipe kodi pamoja na madalali kwani hii ni biashara kama biashara zingine.

Hali ni mbaya na walio wengi wanashindwa kumudu bei za nyumba na kuongeza ugumu wa maisha na umaskin kwa ujumla.

Jenga nyumba yako ili uepuke huh usumbufu.
 
Naam, serikali isijiingize moja kwa moja kwenye biashara, nakubaliana na wewe 100%,kwa sasa duniani nadhani ni China pekee(yenye ujamaa wa kweli),ambapo serikali inafanya biashara. Kwa kuwa sisi Ujamaa wa kweli umetushinda basi viwanda viwe vya umma kupitia PPP au Kiundwe chombo chenye meno ambacho kitaratibu kwa ukaribu Viwanda vyote kwa niaba ya Serikali. Kazi kuu ya Serikali iwe kutoa huduma.

Mawazo mgando hayo. Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ni la serikali lakini lipo kibiashara ba linapata faida kubwa sana.
 
Umemwelewa lakini au unahara tu,

Teknolojia tuliyonayo ni tofauti na wakati viwanda vinabinafsishwa ni bora kujenga vipya kwa teknolojia ya kisasa.

Ulichotakiwa wewe ni kutoa maoni yako kuanzia alipoishia badala ya kutoa matusi.
Hiyo technology mpya inakataza hata kuchukua hayo maeneo ambayo yamegeuzwa matumuzi kama parking na yards?
 
Naamini kama magufuri upo makini kwa kuwapigania watanzania walala hoi ebu basi tembelea kiwanda cha kuzalisha matunda Azam mbagala ujionee jinsi watanzania wanaopeleka matunda yao kiwandani kuuza wanavyo firisika hapo kiwandani na kurudi makwao masikini.watu wanapeleka lori la embe au nanasi na wanakalishwa hapo nje zaidi ya siku 3 hadi 5 kabla ya kupokelewa matunda yao na matokeo yake matunda yanaoza.

mengi anawalipa watu 3000kwa siku mirerani bonite nako vibarua ,wako hoi halafu vyombo vya habari vinajifanya havijui
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom