Uchaguzi 2020 Maoni ya Jeffery Smith juu ya Uchaguzi wa Tanzania 2020

Uchaguzi 2020 Maoni ya Jeffery Smith juu ya Uchaguzi wa Tanzania 2020

Hivi magu mbona analazimisha watu wasahau hata yale mazuri aliyoyafanya? Hivi anajua kuwa mwelekeo ni kuwa ataondolewa vibaya kwenye hicho kiti kwa hii tabia inayo lazimishwa na wapambe wake ambao moto ukiwaka watamkana kuwa alikuwa haambiliki?

Yeye kama anaendesha mambo mpaka "atajisikiaje atakapoamka" halafu kina Pascal Mayalla wanamsifia kuwa hakuna kama yeye basi shauri yake. Kuna siku kilio kitakuwa chake pekee na wanae kina Jeska hao kina Pascal wakigongeana glass za whiskey!
 
Duh...!. Hawa mabeberu wa kizungu, wanahaha sana!. Wanadai kukiwa na uwanja sawa wa ushindani, Magufuli na CCM hawawezi kushinda!.
Duh...!.
Masikini Wazungu hawa tuwasamehe bure tuu!.
Sasa P kuiongoza Tanzania kunahitaji akili gani? Hivi kama M ameweza nani atashindwa kuongoza, huo upinzani una nini mpaka ushindwe kuongoza?
 
We are a cutting edge, wholly unique nonprofit launched in 2016 with a simple goal: to build and promote democratic solutions for African nations.
Ni muanzilishi wa hii NGO
NGO feki hizo,huyo anatumika tu na mabeberu wenzie
Kuleni pesa zao,Magufuli ni Rais
 
Hivi magu mbona analazimisha watu wasahau hata yale mazuri aliyoyafanya? Hivi anajua kuwa mwelekeo ni kuwa ataondolewa vibaya kwenye hicho kiti kwa hii tabia inayo lazimishwa na wapambe wake ambao moto ukiwaka watamkana kuwa alikuwa haambiliki?
Yeye kama anaendesha mambo mpaka "atajisikiaje atakapoamka" halafu kina Pascal Mayalla wanamsifia kuwa hakuna kama yeye basi shauri yake. Kuna siku kilio kitakuwa chake pekee na wanae kina Jeska hao kina Pascal wakigongeana glass za whiskey!
Wishful thinking
 
Twita ya Smith haiwezi kuwa benchmark kwa rangi ya ngozi yake na kwa kuwa kaishi Tanzania.

Wazungu wanapozungumzia equal grounds na Afrikan countries kwenye mahusinao yetu ikiwa ni ajira, biashara na kujenga uchumi, wao wenyewe hawaitumii eaqul grounds kama good practice kwenye vitu vingi sana.

Walimuua Dr. Martin Luther King Jr, simply alitaka haki na fairness itendeke bila kujali rangi ya mtu Marekani.

Jim Crow law, white supremacy, KKK mpaka sasa zipo nyuma ya pazia ndio maana athari za kuuwawa kwa George Floyd kumezua hasira na uchungu kwa namna polisi walivyomuua mtu ambae hakua mhalifu na wala hakuwa amegoma kutii amri ya polisi.

Equal ground is very very relative word to be spoken by Smith simply because he is a white man.

Wazungu wakubali tu kuwa roho zao zinawauma kwa kuwa Tanzania ina rais imara na mifumo yetu iko very stable.

Tuendelee na Magufuli 2020-25.
 
Pascal Mayalla, Duh... !
Una mawazo yale yale ya mkoloni ambaye siku hizi mnamwita beberu. Hawakutaka tupate uhuru kwa kigezo hicho hicho chako kwamba hutuwezi kujitawala. Na wewe unakuja na hoja kwamba huoni upinzani unaoweza kuongoza nchi.

Halafu unauita ukweli mchungu....!
Duh...!
Huo ni ujinga mchungu!!!!
 
Duh...!. Hawa mabeberu wa kizungu, wanahaha sana!. Wanadai kukiwa na uwanja sawa wa ushindani, Magufuli na CCM hawawezi kushinda!.
Duh...!.
Masikini Wazungu hawa tuwasamehe bure tuu!...
Wanajidanganya tu, wangejua upinzani Tanzania hata Ngazi ya mashina hawana ,hawajui hata wana mtaji wa wapiga kura wangapi ,

Ccm wanaweza kukuambia wana mtaji wa wapiga kura wangapi , kwa data zilizo rasmi , wana mtaji kuanzia ngazi ya mashina , hadi juu

Chadema na upinzani mwingine wanategemea Mikumbo tu ili kuokoteza kura .

Kwa Tanzania VYAMA vya upinzani ni makampuni ya watu binafsi ,

Hivi uliwahi kujiuliza kwanini waligomea uchaguzi wa Serikali za mitaa , lakini kuelekea uchaguz mkuu hawajagomea ?

Serikali za mitaa hazina faida kwa kikundi cha watu kama Mbowe, mdee,Zito , Sugu, Zina faida kwa vijana wanaochipukia kwenye Siasa .

Ila Uchaguzi mkuu kwao ni fursa ya kuongeza Ruzuku na kupata angalau ubunge , na sio kuchukua dola.

Sababu walizotumia kugomea Uchaguzi Serikali za mitaa je kwenye Uchaguzi mkuu zimerekebishwa?

Utagundua Tanzania hatuna Upinzani ,Bali tuna wasakatonge tu, na upinzani uchwara .
 
Pascal Mayalla, Magufuli Ni mwoga kuliko kunguru. Kwanini hakuwakemea wale Wasukuma wachawi wa Gamboshi waliposema watamuua mtu yeyote atakaye chukua fomu CCM kushindana na Magufuli?
Kwanini fomu ya urais CCM Tanzania 🇹🇿 Bara itolewe moja tu?
Jibu rahisi ni kwamba Magufuli kausoma upepo, kwamba hata angeshindana na Kingwendu kamati kuu ingempiga chini na kumpendekeza Kingwendu, full stop.
Simiyu: Waganga wa jadi kutoka Gamboshi na Bariadi wadai kumloga Mwana CCM atakayechukua fomu kumpinga Magufuli
Japo nchi yetu haina dini, lakini watu wake wana dini zao, na serikali haingilii imani za watu wake, hivyo miongoni mwa dini hizo ni dini za asili. Hao unaowaita wachawi wa Gamboshi sio wachawi bali ni 'wazee' wataalamu wa kiasili wa Kisikuma, ambao wanatumia utaalamu wa sayansi za asili, kufanya 'mambo' na kwa kutumia utaalamu huo, wamebaini ni rais Magufuli pekee ndiye aliepangiwa kuendelea kuwa rais wa JMT, na kwamba yoyote ambaye angechukua fomu CCM kumpiga, kifo cha kiasili kingemkumba.

Hivyo CCM kwa kutambua hilo na kwa kuwajali Watanzania, kuwapenda na kuwathamini, wakaamua kutoa fomu moja tuu pekee ya kugombea urais CCM ili kuwaepushia dhahama hiyo!.
P
 
Kuna siku kilio kitakuwa chake pekee na wanae kina Jeska hao kina Pascal wakigongeana glass za whiskey!
Duh...!. Huku ni kumtishia maisha Jesca kuwa kuna kitu kitamfika Baba Jesca!, hili ni kosa la jinai la kusababisha kilio kwa maneno!.
Usije kusema ni mimi nimekuchongea wakati ni wewe ndio unayesema kuna siku!. Please tuacheni haya mambo ya kutishia watu maisha kwa kauli za "kuna siku"!. Hakuna siku yoyote ya kutokea kilio chochote inayopangwa na mwanadamu!. Mpaji ni Mungu!, mpangaji ni Mungu.
P
 
Back
Top Bottom