Duh...!. Hawa mabeberu wa kizungu, wanahaha sana!. Wanadai kukiwa na uwanja sawa wa ushindani, Magufuli na CCM hawawezi kushinda!.
Duh...!.
Masikini Wazungu hawa tuwasamehe bure tuu!...
Wanajidanganya tu, wangejua upinzani Tanzania hata Ngazi ya mashina hawana ,hawajui hata wana mtaji wa wapiga kura wangapi ,
Ccm wanaweza kukuambia wana mtaji wa wapiga kura wangapi , kwa data zilizo rasmi , wana mtaji kuanzia ngazi ya mashina , hadi juu
Chadema na upinzani mwingine wanategemea Mikumbo tu ili kuokoteza kura .
Kwa Tanzania VYAMA vya upinzani ni makampuni ya watu binafsi ,
Hivi uliwahi kujiuliza kwanini waligomea uchaguzi wa Serikali za mitaa , lakini kuelekea uchaguz mkuu hawajagomea ?
Serikali za mitaa hazina faida kwa kikundi cha watu kama Mbowe, mdee,Zito , Sugu, Zina faida kwa vijana wanaochipukia kwenye Siasa .
Ila Uchaguzi mkuu kwao ni fursa ya kuongeza Ruzuku na kupata angalau ubunge , na sio kuchukua dola.
Sababu walizotumia kugomea Uchaguzi Serikali za mitaa je kwenye Uchaguzi mkuu zimerekebishwa?
Utagundua Tanzania hatuna Upinzani ,Bali tuna wasakatonge tu, na upinzani uchwara .