Maoni yangu juu mabadiliko ya katiba kwenye ukomo wa Urais

Mkuu kwa andiko lako nafikir hata mfumo wa Democracy pia hautufai bora turudi kwenye mifumo ya U-monarchy watu tutawalane kifalme......

Mkuu hivi kweli upo serious kabisa na hili andiko lako au maana unaona miaka 10 michache bhasi tutawale kiukoo tu ili turudi kabisa utumwani
 
hapana ni kura kuendelea na uongozi au kuitishwa uchaguzi mwingine bada ya miaka mitano...nilichoshauri kuondolewa ni ukomo wa miaka 10 na kuwepo kwa kura ya maoni kila miaka 5 ya kuendelea ama asiendelee kuongoza
Ndo nikakuuliza, nyie mkamuongezea huo muda halafu Mungu akamchukua itakuwaje? Sijui hata kama unaelewa
 
basi ndio maana nikapendekeza kura ya maoni ya aendelee ama laa
Watawala wa kiafrika hawaitaji kura kendelea kutawala watafanya lolote kuendelea kubaki pale uchaguzi ni kiini macho, Bongo alie pinduliwa juzi kati tuu hapo baadhi ya wananchi walinukuliwa na BBC Swahili walisema hata kama ange gombea na mbwa wange mpigia kura mbwa lakini kwenye uchaguzi akashinda
 
kuna kura ya maoni mkuu kila baada ya miaka mitano kuamua aendelee ama asiendelee
 
so changamoto iliyopo hapa ni mfumo wa kura sio rafiki ili kuunga hoja hii...kwamba ikiwa utakuwepo usimamizi wa kura wa haki basi wazo hili ni jema kwa namna ingine
 
kuna kura ya maoni mkuu kila baada ya miaka mitano kuamua aendelee ama asiendelee
àMkuu una miaka mingapi, Maana unataka kuturudisha nyuma unachokisema kilikuwepo Tangu tupate uhuru mpaka miaka ya 1992 pale ambapo Palipoanzishwa vyama vingi...
Maana uliyohadithia hiyo sio Ajenda mpya ililuwepo kipindi cha monoparty system na ndo maana unaona mpaka nyerere mwenyew aliomba poo maana aliongoza kwa muda mrefu sana
 
Shukrani mkuu ila kama wataweka ukomo basi walau hata 20 walau mtu anaweza kufanya mambo yakaeleweka
 
so changamoto iliyopo hapa ni mfumo wa kura sio rafiki ili kuunga hoja hii...kwamba ikiwa utakuwepo usimamizi wa kura wa haki basi wazo hili ni jema kwa namna ingine
Hapana labda tuu tungekua na mfumo wa kua na vipaumbele vya taifa ambavyo yeyote atakae ingia madarakani lazima avifanye kama ni viwanda au ni teknolojia au Kama ni kilimo basi yeyote atakae kuja lazima andeleze
kwa mfano Marekani haijalishi mgombea atakae shinda ni chama tawala au ni upinzani lakini kuna vitu lazima aendeleze kama kuendelea kuwekeza kwenye teknolojia ya silaha na vitu vingine vingi,
lakini huku ni kanyaga twende na kwa tabia yetu waafrika ukiruhusiwa mfumo kama huo itakua ni fimbo ya kuwachapa wanyonge, kama sasa hivi mtu anapata jeuri ya kusema "nilisema na ninasema tena kama unaonewa hamia Burundi" vipi huyu ukimpa mfumo kama huo kitatokea nini hapo 🤔🤔
 
shukrani mkuu basi hapa naona tupambane kwanza kupata uchaguzi huru nawa haki huenda mambo mengi yakawezekana
 
Ndo nikakuuliza, nyie mkamuongezea huo muda halafu Mungu akamchukua itakuwaje? Sijui hata kama unaelewa
nilishaelezea kwenye mada kuwa kifo pia ukomo hivyo utaitishwa uchaguzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…