Mapadri wakizeeka wanapewa mafao ya kujikimu?

Mapadri wakizeeka wanapewa mafao ya kujikimu?

Mi swali langu ni hivi kamanda! Mapadri na masista baada ya kustaafu kwao huwa wanaowa/wanaolewa? Au maisha yao yote wanakua single!
mkuu masista na mapadri hawaoi wao wametoa sadaka kitu kitam zaidi wanachokipenda kwa mungu sababu ya kutooa sio kwamba wamezuiwa na mungu hapana sema kazi yao ile unatakiwa ukafanyekazi popote duniani yani kuna kuhama hama sana sasa wangekua na familia ingekua usumbufu imagine miaka ile ya 1900 wanaambiwa waje africa huku namtumbo huko sasa ukiwa na familia inakua mtihani ila kwa maisha ya sasa papa alikua anafikiria kuwaruhusu waoe manake kesi za kula kondoo zimekua nyingi mi nimeishi nao nawafahamu vizuri
 
Mi nijuavyo kwa ufahamu wangu mapadre wa Rc wengi wao huhudumiwa hadi mwisho wa maisha yao,na hakuna watu wanaoishi maisha ufahari kama mapadre,Maisha yao ni raha mustarehe
Maisha ya kutokuwa na watoto,ni maisha ya upweke.
 
Hiyo miradi haipo kila sehemu/Parokia! Wapo Mapadre wengi tu wanaishi aina hiyo ya maisha. Na sikatai hicho ulichokisema.

Na usisahau pia hao Mapadre nao ni binadamu kama sisi. Hivyo wana tabia za ubinafsi, kupigana zewnge/majungu, ukuda, nk.
Sawa makanisa kwani yanajitegemea au miradi iliyopo sehemu inafahamika na shirika taasisi
Lakini mapadre ni wasomi wazuri lazima wawe na mipango mizuri ya maendeleo zaidi ya kukaa na kuongoza misa tu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Sawa makanisa kwani yanajitegemea au miradi iliyopo sehemu inafahamika na shirika taasisi
Lakini mapadre ni wasomi wazuri lazima wawe na mipango mizuri ya maendeleo zaidi ya kukaa na kuongoza misa tu

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
mkuu kwenye miradi yao hao wasomi wanatumika jamaa wako fiti kwenye kada zote kuna walim madaktari manesi yani kila professional wanazo hadi wengine wanajeshi refer padri wa kanisa la udsm
 
Sawaa Kuna padri mmoja was balangdalali uko kateshi Ni mmbulu Ni tajir haswa aliniambia Ana shamba la miti alifanyia tadhimini akapata milioni Mia nane .na pia alitunga nguruwe Mia mbili akauzaa in short Ana pesa yake nzuri tu cyo za kanisa
 
Hawalipwi mafao yoyote yale ya uzeeni! Ukishapokea Sakramenti ya Upadre, unakuwa umefunga ndoa na kanisa! Utatakiwa kuchunga kondoo wa Bwana maisha yako yote!

Ukizeeka kwa kiwango cha kushindwa kuendesha misa, utaenda kuishi kwenye nyumba maalum kwa ajili ya mapadre wazee. Huko mtapewa huduma zote muhimu. Na ukiumwa, Kanisa litakutibu mwanzo mwisho.

Mapadre hawalipwi mishahara! Isipokuwa tu posho ambayo hulipwa kila mwaka mara moja. Wakati nilipokuwa Mseminari, miaka mingi iliyopita, posho yao ilikuwa ni tsh. Milioni 1.5 kwa mwaka! Bila shaka kwa sasa itakuwa ni zaidi ya hapo.

Mapadre wa zamani walikuwa na wafadhili wao huko Roma - Italy na pia Austria (MIVA), ambao waliwatumia magari ya kutembelea na fedha kwa ajili ya kuanzishia miradi mbalimbali!

Ila kwenye miaka ya katikati kwa 90 na 2000, hawa wafadhili walipungua kwa kiwango kikubwa, na hivyo kufanya baadhi ya maisha ya mapadre kuwa magumu kwa kiasi chake.

NB: maisha ya USEJA ni magumu kwa Mapadri wengi! Maana wanakula vyakula vyenye mafuta, wanga na sukari nyingi! Sasa kinachotokea baada ya hapo, wanakijua wenyewe! Baadhi wanayamudu. Ila wengi yanawashinda.

Naamini ipo siku wataruhusiwa kuoa kama sisi Walei wao.
Sentenso yako ya mwisho ni mbovu!
 
Na masista nao maisha yao yanakuwaje nao wanapofikia umri wa kuzeeka nao wanalipwa nssf ama pssf
Kwanza Masista wao nadhani hufanya mikataba na kanisa kwa hm mda fulani tu na mda ukiisha huwa wanaongeza au wanaachana usista, ila nawao wanapata huduma kama zilezile za mapadre.
 
sikuhizi wanakua nao kwa siri mi nnamjua padri mmoja ana watoto wawili wakubwa tu mtaani
Hahahah ila wanalelewa kimya kimya 😂😂😂 sasa sijajua kwenye wosia huwa wanatajwa kama watoto wa marehemu au wanakausha?
 
Hawalipwi mafao yoyote yale ya uzeeni! Ukishapokea Sakramenti ya Upadre, unakuwa umefunga ndoa na kanisa! Utatakiwa kuchunga kondoo wa Bwana maisha yako yote!

Ukizeeka kwa kiwango cha kushindwa kuendesha misa, utaenda kuishi kwenye nyumba maalum kwa ajili ya mapadre wazee. Huko mtapewa huduma zote muhimu. Na ukiumwa, Kanisa litakutibu mwanzo mwisho.

Mapadre hawalipwi mishahara! Isipokuwa tu posho ambayo hulipwa kila mwaka mara moja. Wakati nilipokuwa Mseminari, miaka mingi iliyopita, posho yao ilikuwa ni tsh. Milioni 1.5 kwa mwaka! Bila shaka kwa sasa itakuwa ni zaidi ya hapo.

Mapadre wa zamani walikuwa na wafadhili wao huko Roma - Italy na pia Austria (MIVA), ambao waliwatumia magari ya kutembelea na fedha kwa ajili ya kuanzishia miradi mbalimbali!

Ila kwenye miaka ya katikati kwa 90 na 2000, hawa wafadhili walipungua kwa kiwango kikubwa, na hivyo kufanya baadhi ya maisha ya mapadre kuwa magumu kwa kiasi chake.

NB: maisha ya USEJA ni magumu kwa Mapadri wengi! Maana wanakula vyakula vyenye mafuta, wanga na sukari nyingi! Sasa kinachotokea baada ya hapo, wanakijua wenyewe! Baadhi wanayamudu. Ila wengi yanawashinda.

Naamini ipo siku wataruhusiwa kuoa kama sisi Walei wao.
Mkuu unasema "Ipo siku wataruhusiwa kuoa"

Swali langu ni kwamba,

Kwani nani kawakataza kuoa? Je ni sheria ya Mungu au ni binadamu tu ndiye aliyewawekea huo utaratibu?

Nauliza tu kiroho safi ili nijue.
 
Hua wanagewa kiinua mgongo cha alfu 65, redio ya bluetooth na flash na biblia.
 
Mi swali langu ni hivi kamanda! Mapadri na masista baada ya kustaafu kwao huwa wanaowa/wanaolewa? Au maisha yao yote wanakua single!
Kwanza kanisa katoliki mapadre wake hawastafu, ndoa yao na kanisa katoliki ni ya milele, katika kuachana na upadre kuna kuasi au kufukuzwa.
Ila kuhusu masista ninavojua mimi wao mikataba yao ni ya mda, mda ukiisha kama hataki kuendelea na usista, basi ana uhuru wa kuolewa!
 
Sawaa Kuna padri mmoja was balangdalali uko kateshi Ni mmbulu Ni tajir haswa aliniambia Ana shamba la miti alifanyia tadhimini akapata milioni Mia nane .na pia alitunga nguruwe Mia mbili akauzaa in short Ana pesa yake nzuri tu cyo za kanisa
Padre haruhusiwi kuwa na pesa au utajiri wake mwenyewe . Kila alichonacho ni mali ya kanisa
 
Back
Top Bottom