Mapato yanayokusanywa Soko la Vitunguu Singida yanaenda wapi? Hali ni mbaya, uchafu umezagaa

Mapato yanayokusanywa Soko la Vitunguu Singida yanaenda wapi? Hali ni mbaya, uchafu umezagaa

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
WhatsApp Image 2024-12-23 at 10.59.06_d1e4d5c9.jpg

20241210_130004 (1).jpg



Soko la Vitunguu Mkoani Singida lililopo maeneo ya Misuna ni moja ya vitega uchumi vikubwa mkoani humo.

Ni soko ambalo kipindi cha msimu linahusisha wafanyabiashara kutoka mataifa mengine yakiwemo Kenya, Uganda Malawi kuja kufanyabiashara kwenye soko hili.

Jambo la kusikitisha ni kuwa mazingira ya soko hili ni duni, hayavutii, soko halina hadhi ile ya 'kimataifa' kama lijulikanavyo.

Kipindi hiki cha mvua hali ni mbaya, ukifika eneo la tukio unakutana na matope, dampo la soko lilipo pembeni hapo ni chafu. Wafanyabiashara wa soko hilo wako katika mazingira magumu.

Wakati wa kiangazi Wafanyabiashara wanateseka juani wakati kipindi cha masika wanalazimika kufunika vitunguu na maturubai ili visinyeshewe.

Wafanyabiashara hao hulipia pesa ya taa Tsh. 1,500 kila wiki, kulipia taa zinazowaka usiku kwa ajili ya ulinzi wa vitunguu lakini sio taa zote zinazowaka, kati ya taa 6 zilizopo tatu zinawaka na tatu haziwaki.

Vilevile wafanyabiashara hao hulazimika kulipia ushuru wa kila gunia moja wanalonunua kwa Tsh 2,000/-. Mapato ya pesa hizo yanafanya kazi gani?

Tangu Serikali itoe ahadi ya kujenga soko imeshakuwa hadithi.

Soko hili lina jina kubwa na linaingizia Serikali pesa nyingi hasa msimu wa mavuno ya vitunguu ukifika lakini sasa ni wakati Serikali nayo iipe hadhi inayostahili kwa kufanya maboresho.

Ikiwa soko litajengwa uhifadhi wa vitunguu utakuwa mzuri, Wafanyabiashara wataondokana na hatari ya kuharibika kwa bidhaa hiyo.

Mbali na hapo hali ilivyo sio salama kwa afya, kumekuwa na taarifa kuwa kuna watu wanaokota vitunguu eneo hilo na kwenda kuuza sehemu nyingine.



 

Attachments

  • 20241210_130004.jpg
    20241210_130004.jpg
    853.8 KB · Views: 7
Hilo soko hapo lilipo si mahali pake, hapo ilikuwa ni uwanja tu usio na shughuli yoyote baadaye ikawa ni genge la kuuzia mbogamboga kabla ya soko la vitunguu kuhamia hapo likitokea Majengo Ukombozi lilikoanzia huko kuonekana ni padogo. Hapo lilipo kwa sasa Missuna ni pafinyu na hapajajengwa miundombinu inayosadifu kuwa ni soko la kimataifa, mvua, jua na upepo mkali unaovuma ni shida kwa wauzaji na wanunuzi wa bidhaa hiyo. Inafaa lihamishwe kwingine patakapokuwa na miundombinu yenye hadhi ya kuitwa soko la kimataifa la vitunguu pasipo na uchafu unaotia kinyaa. Wakajenge nje ya mji, manispaa ni kubwaa na ina maeneo mengi yaliyo wazi.
 
Pesa kujenga itoke Arusha au Moshi? Singida Maskini Tra Kwa mwaka Kodi ni 15 bilioni wakati Arusha Bila utalii tra wanakusanya 450 bilioni
 
Back
Top Bottom