Mapendekezo: Baraza la Mawaziri

Mapendekezo: Baraza la Mawaziri

Bado unapuyanga tu!

Ummy Mwalimu ni Mwanasheria by professional,lakini ni Waziri wa Afya! Doroth Gwajima ni Daktari by professional lakini ni Waziri wa maendeleo ya jamii,Makamba kasoma mambo ya conflicts,lakini ni Waziri wa Nishati, Dotto Biteko ni Mwalimu by professional ni Waziri wa Madini! Punguza njaa utaandika na yasiyoandikika! Mtu ni Rais aje kua Naibu Waziri kweli?? Nina njaa kama wewe,lakini njaa yako imenizidi
Shida yako ipo wapi?
Uchambuzi wangu kwa sehemu kubwa umelenga elimu ya mtu na uzoefu wake kwenye jambo husika hasa katika Mafanikio.

Udaktari wa Gwajima ndo mana akapendekezwa Wizara ya Afya. Ummy kapendekezwa Tamisemi Kwa sababu Kupitia uzoefu wake na uanasheria wake anaonekana anafaa hapo. Una lingine?
 
Bashe humujui kwa undani! Nimefanya nae kazi MCL! Bashe ni hatari,ni mpigaji mzuri sana! Hizo ni bla bla tu! Nikijana wa Rostam yule! Wizara ya fedha kwa Bashe hapana,atakula hadi basi! Bashe anadunda sababu ya nguvu ya Rostam tu,bila Rostam Bashe angekua huko mavumbini!

Mwaka 2010, kipindi cha Jakaya,kina Jakaya na Makamba Senior,waliwahi sema Bashe sio mtanzania,Masha akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani alimuokoa!
Alipiga nini hapo MCL? Tupe ushahidi? Kesi Ilipelekwa wapi na iliamliwaje?
 
We jamaa reasoning capacity yako ni zero kabisa!

CRDB kwa taarifa yako,ilikua moto sababu ya pesa za serikali nyingi zilikua zinapitia pale! Hadi mishahara ya watu wa serikali ilikua inapita pale,Baada ya Magu kupiga chini CRDB,Kimei akaachia ngazi faster,maana alijua kuna anguko lake linakuja! Sasa hivi NMB kamuacha CRDB mbali sana kwa kila kitu! Punguza njaa!
Kwa huo uwezo wake wa kushawishi tu Serikali kufanya malipo kupitia bank aliyokuwa anaiongoza inaonesha ni mtu creative atayeweza kutumia mbinu sahihi kuhakikisha anatengeneza tija na faida. That is how business is!

Bank nyingi sana zimeanzishwa lakini hakuna bank iliyoweza ku compete na hao NMB na NBC kama ilivyoweza ku compete CRBD chini ya Kimei. He is a Mogul kwenye sekta ya fedha na Uchumi. Period
 
Wamelivurugaje? Tupe sababu
Makamba na Nape wamelifundisha taifa kuwa wizi ni jambo jema kufanya ili kupata matokeo (goli la mkono).
Mwigulu... ukiacha dharau na hate-speech kuna unyama anaofanya kwenye tozo (Tuendelee kusubiri Singida BigStars ishuke daraja uwaziri ukiisha?)
 
Hivi January Makamba hanaga proffession?
Maana kwingine kote naona umewataja kwa sifa ikiwemo taaluma, Ila kwa huyu mwamba naona Kama umepata kigugumizi[emoji4][emoji4][emoji4][emoji4][emoji4][emoji4]

[emoji3]
 
Shida yako ipo wapi?
Uchambuzi wangu kwa sehemu kubwa umelenga elimu ya mtu na uzoefu wake kwenye jambo husika hasa katika Mafanikio.

Udaktari wa Gwajima ndo mana akapendekezwa Wizara ya Afya. Ummy kapendekezwa Tamisemi Kwa sababu Kupitia uzoefu wake na uanasheria wake anaonekana anafaa hapo. Una lingine?
Hujui kitu! Kwa hiyo uchambuzi wako unasema Waziri alichosomea ndiyo akifanyie kazi?? Nani aliyekuambia Waziri ni mtendaji kwenye Wizara husika?? Ningekuona wa manaa sana,kama ungesema Katibu Mkuu awe na Elimu ya kile anachokifanyia kazi! Mfano Katibu Mkuu Afya awe Daktari,Katibu Mkuu Ujenzi awe Mhandisi,Katibu Mkuu Maji awe Mhandisi,Katibu Mkuu Sheria,awe Mwanasheria, Katibu Mkuu fedha awe CPA flani! Katibu Mkuu Madini awe Geologist,Katibu Mkuu Nishati mmoja Mhandisi wa mafuta,na mwingine awe Mhandisi wa Umeme!
 
Tanzania hakujawahi kuwa na mapinduzi makubwa ya uchumi
Amani iwe nanyi wana bodi.

Hongereni na mapumziko ya mwisho wa wiki.
Leo napenda kutoa uchambuzi wangu kuhusu Baraza la Mawaziri ambalo ninatamani Rais wa Awamu ya 6 aanze nalo kama Baraza lake la kwanza la Mawaziri ambalo linatekeleza Bajeti yake ambayo imetengenezwa yeye akiwa Rais.

Hii ni kwa sababu Rais Samia kwa kipindi chote tangu awe Rais amekuwa alihudumu na Baraza ambalo kiuhalisia ni la mtangulizi wake ambalo alilifanyia mabadiliko madogo tu.

Kwenye Baraza hili uchambuzi wangu utajikita hasa kwenye Wizara huku nikiwataja watu ninaotamani washike wizara hizo na kwa sababu gani?

Kabla ya kuanza uchambuzi wangu naomba nianze kwa kumtaja mtu ambaye inasemwa ndo waziri bora zaidi kuwahi kuhudumu kwenye baraza la Mawaziri la Tanganyika na baadae Tanzania na kwa nini huyu mtu anatajwa kuwa Waziri bora zaidi

Mtu huyu ni Marehemu Amir Jamal ambaye alikuwa waziri wa fedha kuanzia mwaka 1965 na baadae alikuja kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara kuanzia mwaka 1972 mpaka 1975 na akarudi tena kuwa Waziri wa Fedha kuanzia 1975 mpaka 1977


Ikumbukwe huyu ndo Waziri aliyeongoza Wizara nyeti ambazo zilileta mapinduzi makubwa kwenye uchumi wa Tanzania katika kipindi chake. Viwanda vingi vilivyojengwa kipindi cha Mwl Nyerere vilijengwa huyu mtu akiwa Waziri wa Viwanda na Biashara na Waziri wa Fedha. Kikubwa zaidi aliongoza sera hizi na zikafanikiwa kipindi Tanzania ikiwa nchi ya kijamaa. Unaweza kumuita The mastermind of Tanzania economy

Kwa nini Amir Jamal?
View attachment 2336473

Ikumbukwe Amir Jamal alikuwa na degree ya Masuala ya Fedha na Uchumi kutoka chuo cha Calcuta nchini India. Aliporudi Tanzania ambapo ndo alipozaliwa na kupata elimu ya awali alijihusisha na biashara ikiwemo kusimamia biashara za wazazi wake zilizokuwepo Mkoani Morogoro. Uzoefu huo katika kusimamia biashara za wazazi wake kwa mafanikio ndiko kulikomfanya kuwa Waziri bora zaidi kuwahi kutokea Tanzania akiongoza Wizara za Fedha pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara

Hivyo uchambuzi wangu wa nani awe Waziri wa Sekta ipi utajikita katika eneo la elimu na uzoefu wa mtu husika kwenye eneo hilo

Mapendekezo yangu
1. Wizara ya Fedha, Charles Kimei na Daniel Sirro
kwa Charles Kimei kila mtu anamjua kama mchumi mahiri aliyetolewa Benki kuu ya Tanzania na kupelekwa kuanzisha Benki ya Wakulima CRDB. Tofauti na matumaini ya wengi mchumi huyu aliweza kuongoza CRDB na kuifanya kutoka kuwa benki ya kawaida kabisa na kuwa benki bora zaidi Tanzania na mpaka kufungua Matawi nje ya nchi. Kwa elimu yake ya PhD ya uchumi na uzoefu wake katika kuongoza Taasisi kwa mafanikio makubwa hana budi kuongoza Taasisi nyeti ya Fedha.

2. Wizara ya Viwanda na Biashara, Shabiby naTarimba Abass
Hawa ni wafanyabiashara wenye uzoefu mkubwa kwenye masuala ya Biashara. Wana biashara zinazofahamika na hata ulipaji wao kodi hautilii mashaka. Wana akili ya utafutaji na uzoefu kwenye utafutaji. Mapendekezo yangu wapewe Wizara ya Viwanda na Biashara

3. Wizara ya Kilimo: Wabaki Bashe na Mavunde. Hii ni kwa sababu wameonyesha wana mawazo chanya na uwezo. Bashe kwa uzoefu wake wa kusimamia biashara hasa kampuni za Rostam ameonyesha ameweza kusimamia kilimo kiwe cha Kibiashara.

4. Wizara ya Afya. Mama Gwajima na Ndugulile watafaa. Uzoefu wao kwenye masuala ya Afya ni muhimu sana. Sekta hii inahitaji sana mjuzi wa sekta. Ummy Mwalimu sio kwamba hafai kuwa Waziri ila Tamisemi itamfaa akisaidiana na Jerry Silaa ambaye nae ameonekana kuwa na uzoefu kutokana na kuwa Diwani na Meya kwa kipindi fulani

5. Wizara ya Katiba na Sheria. Hapa Ndumbaro anaweza kuendelea kutokana na uzoefu wake wa Sheria ila anahitaji Naibu Mwanasheria mwenye uzoefu pia wa masuala ya Sheria. Ridhiwani Kikwete na Abdullah Mwinyi au Joseph Thadayo mbunge wa Mwanga wanaweza kumsaidia kwa sababu kama Wanasheria waliofanya kazi kwenye Law firms kubwa zinazofahamika Tanzania wanaweza kuwa msaada mzuri kwa Waziri wao. Sekta ya Sheria ni sekta nyeti hivyo lazima iwe na waziri na naibu wanasheria

6. Wizara ya Maliasili na Utalii. Nape Mnauye na Toufik Salim Turky wanafaa kuongoza Wizara hii. Nape hana uzoefu kwenye sekta ya Utalii ila ameonesha ana passion na masuala ya utalii kupitia habari. Turkish ni mfanyabiashara ambaye kwa sasa anaongoza biashara za baba yake Zanzibar ikiwemo zile zinazohusiana na masuala ya watalii kama hoteli. Naamini kwa pamoja wataweza kuipeleka sekta hii juu

7. Wizara ya Madini. Sospeter Muhongo na Deo Mwanyika watafaa sana kwenye hii Wizara. Kwa uzoefu wa Muhongo kwenye Madini na uzoefu wa Deo mwanyika ambaye alifikia hadi cheo cha Makamu wa Rais wa Barrik kampuni kubwa inayomiliki migodi mikubwa zaidi Tanzania hakuna namna zaidi ya kuwatumia hawa watu kwenye sekta hii

8. Wizara ya Nishati. January Makamba ameonesha anaweza, nimevutiwa sana na ubunifu wake wa kusisitiza nishati mbadala hasa ya Gesi ambayo kwa hali inavyokwenda hasa mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu mkubwa wa misitu nasisitiza aendelee kuwepo kwenye wizara hii. Kwa Naibu aendelee Byabato

9. Ofisi ya Waziri Mkuu. Waendelee Simbachawene na mwenzake. Wametosha

10. Teknolojia na Habari. Pindi Chana na Zaytun Swai. Pindi Chana ni Mwanasheria ambaye ana uzoefu kwenye masuala ya Sheria. Uzoefu wake unahitajika sana kwenye kusimamia kanuni na taratibu kwenye sekta ya habari na mawasiliano. kwa zaytun swai huyu ni msomi mahiri kwenye suala la teknolojia aliyesoma shule za vipaji maalum na kuhitimu vizuri degree ya computer science. anafaa kuwa hapa.

11. Makamu wa Rais- Muungano, Mwigulu Nchemba. kwa uzoefu wake kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama ni dhahiri anazijua vizuri siasa za bara na visiwani. Ni vizuri akawa wizara hii akipewa Naibu yeyote kutoka upande wa Zanzibar

12. Ardhi. Kunambi na Mtemvu. kwa kunambi huyu akiwa Mkurugenzi wa Jiji Dodoma tuliona alivyosimamia vizuri Dodoma kupangwa. Mtemvu pia kupitia michango yake bungeni anaonekana kama mbunge mwenye uelewa mkubwa sana juu ya mipango miji. Ni vizuri wakapewa wizara ya Ardhi ili kwa mara ya kwanza Tanzania tushuhudie mipango miji mizuri na kuondokana na ujenzi holela.

13. Ujenzi na Uchukuzi. Waendelee waliopo. Wameonesha Wanaweza. Pia mambo ya nje ya Ulinzi hazihitaji mabadiliko

14. Maji. Waendelee waliopo kwa kuwa wameonesha wanaweza

15. Michezo. Mchengerwa na Gekul wamepamudu. Si vibaya wakaendelea. ila pakihitaji mabadiliko Hamis Mwinjuma akiwekwa kumsaidia mchengerwa hasa kwenye kuboresha Sanaa sio vibaya sana

16. Utumishi na Utawala Bora. Jessica kapamudu. sio vibaya akiendelea na Ndejembi ambaye pia anaonekana yuko composed na ana uelewa mzuri wa mambo.

17. Elimu wakiendelea waliopo sio mbaya wana uzoefu na exposure nzuri.

18. Mifugo na uvuvi hapa pasta kichwa. So far sioni mwenye exposure anayeweza kugeuza sekta ya uvuvi kuwa ya kisasa zaidi. Tunahitaji sana mtaalam au mzoefu kwenye masuala ya biashara na uwekezaji ili anyone na kuibadilisha hii sekta. Akitoka nje ya wabunge hawa itapendeza zaidi

Naomba kuwasilisha!
 
Hujui kitu! Kwa hiyo uchambuzi wako unasema Waziri alichosomea ndiyo akifanyie kazi?? Nani aliyekuambia Waziri ni mtendaji kwenye Wizara husika?? Ningekuona wa manaa sana,kama ungesema Katibu Mkuu awe na Elimu ya kile anachokifanyia kazi! Mfano Katibu Mkuu Afya awe Daktari,Katibu Mkuu Ujenzi awe Mhandisi,Katibu Mkuu Maji awe Mhandisi,Katibu Mkuu Sheria,awe Mwanasheria, Katibu Mkuu fedha awe CPA flani! Katibu Mkuu Madini awe Geologist,Katibu Mkuu Nishati mmoja Mhandisi wa mafuta,na mwingine awe Mhandisi wa Umeme!
Makatibu Wakuu mostly wana fani ya Taasisi wanazoziongoza. Kusema Waziri asiwe na fani inayohusu Taasisi anayoiongoza au asiwe na uzoefu wa Mafanikio katika jambo fulani inawezekana ndo imetufanya hadi leo Tupo hapa tulipo. Kila siku kupeana lawama kumbe Tatizo hatuna watu sahihi katika nafasi sahihi.

Nimekupa mfano wa Amir Jamal aliyejenga viwanda vingi zaidi na kuanzisha makampuni na mashirika mbalimbali katika kipindi cha Uchumi wa kijamaa only Kwa sababu alikuwa na elimu ya mambo ya Fedha na Uchumi pamoja na uzoefu katika mambo ya biashara.

Ukijua kuwa Baraza la Mawaziri ndo chombo cha juu kabisa cha maamuzi kwenye nchi huwezi kupuuzia hoja kuwa Waziri lazima awe na kitu kama Elimu na uzoefu katika jambo analoliongoza

Kuchagua watu sahihi katika nafasi za Uwaziri kutapeleka kubadilika hadi kwenye aina ya wabunge tunaochagua na kuwapeleka bungeni
 
Alipiga nini hapo MCL? Tupe ushahidi? Kesi Ilipelekwa wapi na iliamliwaje?
Walioiba Tanzania hii wote wako mahakamani?? Juzi Eng Kakonko katia timu na gari la JW huoni kama ni watu wanaojiamini??

Unajua kashifa ya January Makamba kipindi akiwa Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Nishati na Madini??

Unajua kina nani walibeba pesa za Tegeta Escrow pale Stanbic kwenye mifuko ya sandarusi?? Unajua nani alikua Waziri wa fedha wa kipindi hicho?? Kipi kilimkuta?? Jifunze!

Unajua kipindi kile Mizengo Pinda akiwa PM alisema yuko tayari kusurubiwa bungeni,lakini hayuko tayari kusema nani mmlimi wa Kagoda Agriculture??? Mifano ni mingi! Jifunze kwanza!
 
Amiri Jamal aliweza kufanya kwenye viwanda na Fedha during the glory days of Tanzania economy Awamu ya Kwanza
Tanzania hakujawahi kuwa na mapinduzi makubwa ya uchumi
 
Walioiba Tanzania hii wote wako mahakamani?? Juzi Eng Kakonko katia timu na gari la JW huoni kama ni watu wanaojiamini??

Unajua kashifa ya January Makamba kipindi akiwa Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Nishati na Madini??

Unajua kina nani walibeba pesa za Tegeta Escrow pale Stanbic kwenye mifuko ya sandarusi?? Unajua nani alikua Waziri wa fedha wa kipindi hicho?? Kipi kilimkuta?? Jifunze!

Unajua kipindi kile Mizengo Pinda akiwa PM alisema yuko tayari kusurubiwa bungeni,lakini hayuko tayari kusema nani mmlimi wa Kagoda Agriculture??? Mifano ni mingi! Jifunze kwanza!
Nimekwambia tupe ushahidi dhidi ya wizi ya bashe acha maneno maneno
 
Makamba na Nape wamelifundisha taifa kuwa wizi ni jambo jema kufanya ili kupata matokeo (goli la mkono).
Mwigulu... ukiacha dharau na hate-speech kuna unyama anaofanya kwenye tozo (Tuendelee kusubiri Singida BigStars ishuke daraja uwaziri ukiisha?)
Aliiba nini kwenye bao la mkono?
 
Makatibu Wakuu mostly wana fani ya Taasisi wanazoziongoza. Kusema Waziri asiwe na fani inayohusu Taasisi anayoiongoza au asiwe na uzoefu wa Mafanikio katika jambo fulani inawezekana ndo imetufanya hadi leo Tupo hapa tulipo. Kila siku kupeana lawama kumbe Tatizo hatuna watu sahihi katika nafasi sahihi.

Nimekupa mfano wa Amir Jamal aliyejenga viwanda vingi zaidi na kuanzisha makampuni na mashirika mbalimbali katika kipindi cha Uchumi wa kijamaa only Kwa sababu alikuwa na elimu ya mambo ya Fedha na Uchumi pamoja na uzoefu katika mambo ya biashara.

Ukijua kuwa Baraza la Mawaziri ndo chombo cha juu kabisa cha maamuzi kwenye nchi huwezi kupuuzia hoja kuwa Waziri lazima awe na kitu kama Elimu na uzoefu katika jambo analoliongoza

Kuchagua watu sahihi katika nafasi za Uwaziri kutapeleka kubadilika hadi kwenye aina ya wabunge tunaochagua na kuwapeleka bungeni
Kuna Waziri anayeweza kupinga suala,ambalo Rais atalisema kwenye Baraza la Mawaziri hata kama ni ujinga?? Rejea uuzwaji wa nyumba za serikali kipindi cha Mkapa, Magufuli alisimamia zoezi akiwa Waziri wa Ujenzi,lakini hadi anafariki,hii kitu ilikua inamtafuna kweli kweli,na kama ingekua kwenye democratic countries, Magufuli asingekua Rais wa Tanzania kwa hiyo scandal
 
Amani iwe nanyi wana bodi.

Hongereni na mapumziko ya mwisho wa wiki.
Leo napenda kutoa uchambuzi wangu kuhusu Baraza la Mawaziri ambalo ninatamani Rais wa Awamu ya 6 aanze nalo kama Baraza lake la kwanza la Mawaziri ambalo linatekeleza Bajeti yake ambayo imetengenezwa yeye akiwa Rais.

Hii ni kwa sababu Rais Samia kwa kipindi chote tangu awe Rais amekuwa alihudumu na Baraza ambalo kiuhalisia ni la mtangulizi wake ambalo alilifanyia mabadiliko madogo tu.

Kwenye Baraza hili uchambuzi wangu utajikita hasa kwenye Wizara huku nikiwataja watu ninaotamani washike wizara hizo na kwa sababu gani?

Kabla ya kuanza uchambuzi wangu naomba nianze kwa kumtaja mtu ambaye inasemwa ndo waziri bora zaidi kuwahi kuhudumu kwenye baraza la Mawaziri la Tanganyika na baadae Tanzania na kwa nini huyu mtu anatajwa kuwa Waziri bora zaidi

Mtu huyu ni Marehemu Amir Jamal ambaye alikuwa waziri wa fedha kuanzia mwaka 1965 na baadae alikuja kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara kuanzia mwaka 1972 mpaka 1975 na akarudi tena kuwa Waziri wa Fedha kuanzia 1975 mpaka 1977


Ikumbukwe huyu ndo Waziri aliyeongoza Wizara nyeti ambazo zilileta mapinduzi makubwa kwenye uchumi wa Tanzania katika kipindi chake. Viwanda vingi vilivyojengwa kipindi cha Mwl Nyerere vilijengwa huyu mtu akiwa Waziri wa Viwanda na Biashara na Waziri wa Fedha. Kikubwa zaidi aliongoza sera hizi na zikafanikiwa kipindi Tanzania ikiwa nchi ya kijamaa. Unaweza kumuita The mastermind of Tanzania economy

Kwa nini Amir Jamal?
View attachment 2336473

Ikumbukwe Amir Jamal alikuwa na degree ya Masuala ya Fedha na Uchumi kutoka chuo cha Calcuta nchini India. Aliporudi Tanzania ambapo ndo alipozaliwa na kupata elimu ya awali alijihusisha na biashara ikiwemo kusimamia biashara za wazazi wake zilizokuwepo Mkoani Morogoro. Uzoefu huo katika kusimamia biashara za wazazi wake kwa mafanikio ndiko kulikomfanya kuwa Waziri bora zaidi kuwahi kutokea Tanzania akiongoza Wizara za Fedha pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara

Hivyo uchambuzi wangu wa nani awe Waziri wa Sekta ipi utajikita katika eneo la elimu na uzoefu wa mtu husika kwenye eneo hilo

Mapendekezo yangu
1. Wizara ya Fedha, Charles Kimei na Daniel Sirro
kwa Charles Kimei kila mtu anamjua kama mchumi mahiri aliyetolewa Benki kuu ya Tanzania na kupelekwa kuanzisha Benki ya Wakulima CRDB. Tofauti na matumaini ya wengi mchumi huyu aliweza kuongoza CRDB na kuifanya kutoka kuwa benki ya kawaida kabisa na kuwa benki bora zaidi Tanzania na mpaka kufungua Matawi nje ya nchi. Kwa elimu yake ya PhD ya uchumi na uzoefu wake katika kuongoza Taasisi kwa mafanikio makubwa hana budi kuongoza Taasisi nyeti ya Fedha.

2. Wizara ya Viwanda na Biashara, Shabiby naTarimba Abass
Hawa ni wafanyabiashara wenye uzoefu mkubwa kwenye masuala ya Biashara. Wana biashara zinazofahamika na hata ulipaji wao kodi hautilii mashaka. Wana akili ya utafutaji na uzoefu kwenye utafutaji. Mapendekezo yangu wapewe Wizara ya Viwanda na Biashara

3. Wizara ya Kilimo: Wabaki Bashe na Mavunde. Hii ni kwa sababu wameonyesha wana mawazo chanya na uwezo. Bashe kwa uzoefu wake wa kusimamia biashara hasa kampuni za Rostam ameonyesha ameweza kusimamia kilimo kiwe cha Kibiashara.

4. Wizara ya Afya. Mama Gwajima na Ndugulile watafaa. Uzoefu wao kwenye masuala ya Afya ni muhimu sana. Sekta hii inahitaji sana mjuzi wa sekta. Ummy Mwalimu sio kwamba hafai kuwa Waziri ila Tamisemi itamfaa akisaidiana na Jerry Silaa ambaye nae ameonekana kuwa na uzoefu kutokana na kuwa Diwani na Meya kwa kipindi fulani

5. Wizara ya Katiba na Sheria. Hapa Ndumbaro anaweza kuendelea kutokana na uzoefu wake wa Sheria ila anahitaji Naibu Mwanasheria mwenye uzoefu pia wa masuala ya Sheria. Ridhiwani Kikwete na Abdullah Mwinyi au Joseph Thadayo mbunge wa Mwanga wanaweza kumsaidia kwa sababu kama Wanasheria waliofanya kazi kwenye Law firms kubwa zinazofahamika Tanzania wanaweza kuwa msaada mzuri kwa Waziri wao. Sekta ya Sheria ni sekta nyeti hivyo lazima iwe na waziri na naibu wanasheria

6. Wizara ya Maliasili na Utalii. Nape Mnauye na Toufik Salim Turky wanafaa kuongoza Wizara hii. Nape hana uzoefu kwenye sekta ya Utalii ila ameonesha ana passion na masuala ya utalii kupitia habari. Turkish ni mfanyabiashara ambaye kwa sasa anaongoza biashara za baba yake Zanzibar ikiwemo zile zinazohusiana na masuala ya watalii kama hoteli. Naamini kwa pamoja wataweza kuipeleka sekta hii juu

7. Wizara ya Madini. Sospeter Muhongo na Deo Mwanyika watafaa sana kwenye hii Wizara. Kwa uzoefu wa Muhongo kwenye Madini na uzoefu wa Deo mwanyika ambaye alifikia hadi cheo cha Makamu wa Rais wa Barrik kampuni kubwa inayomiliki migodi mikubwa zaidi Tanzania hakuna namna zaidi ya kuwatumia hawa watu kwenye sekta hii

8. Wizara ya Nishati. January Makamba ameonesha anaweza, nimevutiwa sana na ubunifu wake wa kusisitiza nishati mbadala hasa ya Gesi ambayo kwa hali inavyokwenda hasa mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu mkubwa wa misitu nasisitiza aendelee kuwepo kwenye wizara hii. Kwa Naibu aendelee Byabato

9. Ofisi ya Waziri Mkuu. Waendelee Simbachawene na mwenzake. Wametosha

10. Teknolojia na Habari. Pindi Chana na Zaytun Swai. Pindi Chana ni Mwanasheria ambaye ana uzoefu kwenye masuala ya Sheria. Uzoefu wake unahitajika sana kwenye kusimamia kanuni na taratibu kwenye sekta ya habari na mawasiliano. kwa zaytun swai huyu ni msomi mahiri kwenye suala la teknolojia aliyesoma shule za vipaji maalum na kuhitimu vizuri degree ya computer science. anafaa kuwa hapa.

11. Makamu wa Rais- Muungano, Mwigulu Nchemba. kwa uzoefu wake kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama ni dhahiri anazijua vizuri siasa za bara na visiwani. Ni vizuri akawa wizara hii akipewa Naibu yeyote kutoka upande wa Zanzibar

12. Ardhi. Kunambi na Mtemvu. kwa kunambi huyu akiwa Mkurugenzi wa Jiji Dodoma tuliona alivyosimamia vizuri Dodoma kupangwa. Mtemvu pia kupitia michango yake bungeni anaonekana kama mbunge mwenye uelewa mkubwa sana juu ya mipango miji. Ni vizuri wakapewa wizara ya Ardhi ili kwa mara ya kwanza Tanzania tushuhudie mipango miji mizuri na kuondokana na ujenzi holela.

13. Ujenzi na Uchukuzi. Waendelee waliopo. Wameonesha Wanaweza. Pia mambo ya nje ya Ulinzi hazihitaji mabadiliko

14. Maji. Waendelee waliopo kwa kuwa wameonesha wanaweza

15. Michezo. Mchengerwa na Gekul wamepamudu. Si vibaya wakaendelea. ila pakihitaji mabadiliko Hamis Mwinjuma akiwekwa kumsaidia mchengerwa hasa kwenye kuboresha Sanaa sio vibaya sana

16. Utumishi na Utawala Bora. Jessica kapamudu. sio vibaya akiendelea na Ndejembi ambaye pia anaonekana yuko composed na ana uelewa mzuri wa mambo.

17. Elimu wakiendelea waliopo sio mbaya wana uzoefu na exposure nzuri.

18. Mifugo na uvuvi hapa pasta kichwa. So far sioni mwenye exposure anayeweza kugeuza sekta ya uvuvi kuwa ya kisasa zaidi. Tunahitaji sana mtaalam au mzoefu kwenye masuala ya biashara na uwekezaji ili anyone na kuibadilisha hii sekta. Akitoka nje ya wabunge hawa itapendeza zaidi

Naomba kuwasilisha!
Tatizo la ncho hii sio aina ya Mawaziri, Hata yesu angeshukankuja kuwa Waziri matatizo yatakuwa pale pale
 
Kwa utalii ni safi sana.anahitajika mtu mwenye exposure na ubunifu kuliko mtu ambae ni hard wired protocol. Ingawa hamis alijarib kuleta ladha tofauf kwaa.kupeleka wale wasaniikupanda mlima haikua sahih wale sio influencers.sasa nan yule mzee wa kulia misiban akapande mlima ili ani motivate mim kweli?? Kwanza hata sijui hata anacho act na sio mpenz wa bongo muv kabisaa.
Utalii unahitaj creativeness kwerikweri.hiv mpaka leo suala la beach Agency sijui limefia kweny makbrasha? Hatu ja utileze beach kabisaaa kabisaa.nchi ndogo ndogo tu ambazo hazina vivutio vingi mfano sycheles ni beach tu zinawatoa.idad ya wagen ni kubwa compared na sehem nyingine.hakuna raia hasa utalii wa ndan asiyependa beach na masuala ya maji maji kama zile water packs.utalii unahitaj maono sana
 
Back
Top Bottom