Mapendekezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha: Igeuze Arusha kuwa ndo "Financial Centre" ya Tanzania na iwe mfano wa mikoa ingine na tafuta washauri maalum

Mapendekezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha: Igeuze Arusha kuwa ndo "Financial Centre" ya Tanzania na iwe mfano wa mikoa ingine na tafuta washauri maalum

Kwani financial centre ndiyo hutengenezwa namna hiyo? Na mtu Zerobrain lama Bashite.

Kwanza tupate maana ya 'financial centre". Kwa mujibu wa Investopedia

"A financial center or hub is a city that is strategically located and has a concentration of top-tier financial institutions, reputable stock exchanges, public and private banks, trading firms, and major insurance companies"

Je Arusha inaweza ikawa na financial structures kama hizo?

East Africa yenyewe naweza kusema inayo Nairobi pekee kama regional financial centre.

Globally top financial centres ni kama New York, London, Hong Kong, Singapore na San Francisco.

Sasa huyo bwege anaweza kufanya maajabu gani kuifanya Arusha ipate hayo ma institutions?

Labda ungeniambia tu kuwa aifanye Arusha kuwa regional tourist hub
Kuna sababu nyingi zaweza kuifanya city yoyote kuwa kugeuzwa kuwa financial center bila kuangalia sana nje ya nchi.

1. Tayari Arusha ni tourist destination na sio Tourist hub kama ilivyo Dubai ya leo.

2. Miji mingine uloongelea ni financial capitals kama London na New York ambayo ina pia soko la mitaji (Stock Exchange), hivyo Arusha yaweza tu kuwa Finacial center ya Tanzania ikihudumia mikoa jirani ili nayo iwezo kunyanyuka kiuchumi.

Kinotakwia ni kitu twaita kwa kiingereza revitalization yaani kuigeuza na kuibadili Arusha kuwa Financial Center kwani tayari kuna benki kuu hapo na kituo cha kimataifa cha AICC na biashara zingine kubwa tu.
 
Mkoa wenye advantage na resources kuwa industrial hub ni Pwani tu kutokana na logistical position na adequate land.

Acha kuandika pumba hapa na huku huijui Arusha
Kwani Arusha kijiigrafia haifai kuwa financial centre?

Au Arusha haina ardhi ya kutosha?

Arusha pia upo mpaka ambao kwa mtu mwenye maoni tayari ni kitega uchumi kizuri kwa mkoa.

Au weye ni mzaramo wa hapo Chalinze?
 
Ajitahidi tu aifanye kuwa kitovu cha utaii. Barabara nzuri, mazingira masafi, taa za barabarani mji wote na Usalama.
 
Nimemueleza hapo kwenye mada na nimegusia kuwepo kwa mahakama za haki za binadamu hapohapo Arusha.

Na kama kuna watu ambao wana msukumo wa kufungua mashtaka mbona mahakama ipo hapohapo Arusha?
Mkuu labda hatupo kwenye mjadala mmoja,ninachokitaka mimi ni Mr. Makonda to came clean na tuhuma zinazomkabili na sip kwenda kwa court,atumie hata social networks aelezee hasa why anahusishwa na jina la Bashite,tuhuma za utekaji na uuaji,tuhuma za dhuruma kwa binadamu wenzake etc etc,that's all
 
Labda atafute za kwake awekeze
Na ndio atakachofanya
Kwa utawala wa Afrika kuteuliwa tu ni utajiri tosha wa kuanza kujilimbokizia miradi ya haram na halali
Hapo akikaa mda utaona ana machimbo na hotel za kitalii

Hakuna anaejali haya unayosema kwani sio kazi yake hiyo
 
Mkuu labda hatupo kwenye mjadala mmoja,ninachokitaka mimi ni Mr. Makonda to came clean na tuhuma zinazomkabili na sip kwenda kwa court,atumie hata social networks aelezee hasa why anahusishwa na jina la Bashite,tuhuma za utekaji na uuaji,tuhuma za dhuruma kwa binadamu wenzake etc etc,that's all
Labda kwa ujeuri wake aweza kuendelea kiukaa kimya juu ya hilo na sidhani kama kuna alie na interest ya kufungua kesi ya madai.

Yule anetuhumu si ndie yule aneenda polisi kupeleka tuhumua zake au?

Na polisi si wapo? na watapokea tuhuma hizo na kuzifanyia maana hilo ni jukumu lao.

Tukiendelea kutoa tuhuma tu mitandaoni nafikiri haitasaidia kupata hakai ya kusikilizwa madai hayo na pia haki ya mtuhumiwa kupata nafasi ya jibu tuhuma kwa njia sheria ambayo ni polisi na mahakama.

Mimi hayo ni mapendekezo yangu hayamaanishi kuwa namuunga mkono Mr Makonda kwa kutojibu tuhuma.
 
Binafsi nimeona "potential" yako katika uongozi una uthubutu lakini ninahusudu uthubutu wako huo kwamba utachochea harakati za wananchi kujiletea maendeleo.

Mtu akikwambia kuwa, "samahani umefeli katika zoezi la usaili lakini tumeona "potential" ndani yako, fahamu kuwa bado waonekana una uwezo wa aina fulani na hunedna huko baadae ukapitishwa kweye usaili mwingine.

Neno hili "potential" lamaanisha kuwa na uwezo na kuendeleza kitu au mtu kwa ajili ya baadae. Hata mtu akiwa ana duka auza bidhaa, akitokea mteja ambae yupo tayari kununua bidhaa lakini hana fedha wakati huo ila akisema atakuomba uweke bidhaa alochagua pembeni, tayari huyo ni "potential customer".

Kwahiyo umeonekana una "potential" kwa ajili ya baadae nafikiri hichi kitendo kilotokea hivi karibuni ni uthibitisho kuwa una "future" huko mbele.

Hivyo kama kiongozi ulie na dhamana ya kuongoza mkoa ukiwa mwakilishi wa raisi wa Jamhuri ya Muungano, una jukumu la kuja na mikakati hii ikiwa imeweka malengo rasmi yaani kuinua kiwango cha maisha ya wananchi wa Arusha,kutatua migogoro ya ardhi, kuondoa kero za uhalifu, kuinua uchumi wa mkoa, kupunguza tofauti ya kipato, kuhakikisha kodi yakusanywa, kuwashughulikia kisheria wakwepaji kodi na wabadhilifu wa fedha za kodi hiyo na kusimamia na kuimarisha usalama wa mkoa wa Arusha.

Arusha tayari ni mji wa kibiashara kuanzia madini, Utalii mahoteli na biashara zingine nyingi tu.

Mapendekezo yangu kwako nikiwa ni mtu ambae nimeiona Arusha kuwa ina "potential" kiuchumi, basi keti chini na timu yako panga mikakati ya kuifanya Arusha kwa kituo cha biashara Tanzania yaani "Financial Centre of Tanzania".

Kama nilivyosema hapo juu Arusha ina madini, mbuga za wanyama, mahoteli ya kimataifa, kituo cha biashara cha AICC, uwanja mpya wa mpira waja na biashara zingine nyingi tu ambazo zina uwezo wa kuinyanyua Arusha kiuchumi.

Si tu Arusha yavutia wageni watalii kutoka mataifa mbalimbali duniani pakini pia yaweza kuvutia zaidi uwekezaji wa ndai ambapo watanzania wenye fedhawaweza kuleta biashara zao Arusha na kuibadilisha kimuenekano. Nimeona yupo mfanyabbiashara mmoja ambae amenunua hoteli ya kitalii na kuamua kuivunja yote.

Hii ni ishara tosha kwamba endapo tunapata wafanyabiashara zaidi wa ndani basi mzungunguko wa fedha mkoani Arusha waweza kupongeza pato la mkoa na pia kusaidia kuongeza na kupanua soko la ajira khasa kwa vijana mkoani humo.

Arusha ni mkoa unotoa madini pekee duniani ya Tanzanite ambayo hutumika kutengeneza vito ghali katika nchi nyingi duniani khasa Antwerp, Singapore, India na Sauri Arabia. Hii pekee yanofanya Arusha kuwa "Exporter" pekee wa madini hayo jambo linoweza kufutanya kuwa na uchumi imara unofanana na wenzetu wa Botswana.

Botswana walitengeneza mazingira mazuri ya kuwezesha madni ya Almasi kutengenezwa nchini humo na bandikuu ya Botswana kusimamia biashara hiyo kwa umakini.

Utalii pia bado waifanya Arusha kuendelea kuwa kivutio kwa raia wa kigeni nchini. Jambo hili laweza kuangaliwa zaidi ili kuongeza idadi ya watalii kila mwaka. Hii yaweza kufanikiwa tu endapo mkuu wa koa utafanikisha kuwa na programs maalum kwa ajili ya kuitangaza Arusha kupitia tovuti za kibalozi huko nje, matangazo katika sehemu mbalimbali,nje na ndani ya nchi na pia kuwa na vituo maalum katika balozi zetu ili kuvutia zaidi watalii.

Mapato yanopatikana katika mkoa wa Arusha kuanzia kodi ya maendeleo na Utalii , madini vina uwezo wa kuuboresha uwanja wa ndege wa KIA ili kuwa na hadhi inofanana na mkoa wa kimataifa. Majengo ya uwanja huo kwa sasa yana paa za mabati ambayo si taswira nzuri kwa mkoa. Hivyo litakuwa ni jambo la kimaendeleo kufikiria kujenga upya uwanja huo kwa kuupanua zaidi na kuujenga kisasa.

Ndugu mkuu wa mkoa, kama huelewi Arusha ni mkoa ambao ni mali yaani financial Asset ya nchi kutokana na hadi yake kimataifa. Kuwepo tu kwa kituo cha biashara cha kimataifa chaifanya Arusha kuwa kivutio na kuleta shauku kwa wawekezaji wa kimataifa.

Hivyo situ kuna kituo AICC lakini pia kuwa mahakama ya kimataifa ya haki za binadamu na kuna mahakama ya AFCHPR na pia kuna mahakama ya umoja wa mataifa ya ICTR inoshughulikia kseiza mauaji ya kimbari yalotokea Rwanda. Mambo haya yaifanya Arusha kuwa ni kioo cha sheria za nchi na za kimataifa na pia kioo cha sheria za haki za binadamu.

Mazingira mazuri yanoandaliwa na serikali katika sehemu yoyote ile, husababisha kukua kwa ari na mori kwa wananchi kujiletea maendeleo wao wenyewe. Watu wengi duniani bado waishangaa China na kuiangalia kwa jicho la uhasidi kwa namna ambavyo imeweza kuwanyanyua wananchi wa kuipato cha chini kwenda kwenye kipato cha kati.

Hivyo mkuu wa mkoa, huu ni wakati wako wa kuonyesha umahiri wako katika kuhakikisha wapata njia sahihi za kuwanyanyua wananchi wa kipato cha chini wa Arusha na kuwa na uwezo kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ni wakati wa kufanya tathmini ya kutambua ni viwanda vipi vyahitaji kuboreshwa au msaada wa fedha ili kujiimarisha. Tusisahau Arusha iliwahi kuwa na kiwanda cha kutengeneza matairi cha General Tyre ambacho leo hii ni historia,je ni kwanini tulishindwa kukiimarisha kiwanda hichi?, haya ndo masuali ambayo yataleta majibu na namna ya kuweza kuangalia uwezekanio wa kua na viwanda kama hichi.

Viwanda vidogovidogo "Smallscale industries" navyo ni sehemu ya uchumi wa sehemu yoyote na litakuwa ni jambo la kimaendeleo ikiwa kutatengwa eneo maalum au "Industrial Estate" ambalo litasheheni biashara zote ndogondogo ambazo zatambulika na zote kulipa kodi kulingana na mapato yao.

Mafuriko yanotokea sasa na kuathiri maeneo mengi ni dalili ya miundombinu mibovu au ulokosa kufuatiliwa. Hivyo ujenzi wa miundombinu bora itasaidia kupinguza athari za mafuriko na pia kuwezesha mkoa kuwa na njia safi na salama za magari na watembea kwa miguu.

Bado Arusha ni soko linokuwa yaani (emerging market). Soko linokuwa ni lile soko ambalo lina viashiria vyote vya soko liloendelea lakini halijafikia viwango vinotakiwa. Hivyo ni lazima viashiria hivi viwepo na hapo ndipo Arusha yaweza kuongeza uchumi wake na pia kuvutia aina zingine za uchuni kama ule uchumi wa gig enonomy ambao wahusisha biashara za kuagiza vyakula kupitia mtandao wa internet au simu ya mkononi.

Aina hii ya uchumi wa internet waweza kuwasaidia vijana kujiajiri katika maeneo ya usafirishaji abiria na kusambaza vyakula. Ajira za namna hii zitawafaa wale vijana ambao hawana ajira rasmi lakini ambao wanakuwa wamejiandikisha TRA. Hivyo biashara kama ya Uber na Uber Eat zaweza kuwa ni moto au Hot-cake katika mji.

Hivyo mkuu wa mkoa mimi nimekupa mawazo ambayo nina uhakika yaweza kukutoa katika siasa za malumbano na kutafuta kiki kama ambavyo itaweza kutafsiriwa na mahasidi wako. Kazi ya uongozi ni ngumu lakini kwa nchi hizi zetu za Kiafrika imegundulika kuwa bila msukumo (unofuata sheria) nchi yetu/ zetu haiwezi kuendelea.

Mwisho "but last", ndugu mkuu wa mkoa tafita washauri maalum wa kukusaidia kazi yako mkoani Arusha. Katika video ilowekwa hivi majuzi katika mitandao ya kijamii kuna makosa kadhaa ambayo yahitaji ushauri maalum. Washauri hawa maalumau "special advisors" ni watu maalum wenye uwezo na utaalm wa kushauri viongozi namna ya kujiweka kwenye macho ya umma.

Hawa watashauri namna ya kuandaa hotuba yako na pia watashauri na kutathmini hotuba hiyo hata kama haikuandikwa. Ukumbuke kuwa hotuba au maneno yoyote mara tu yatokapo kinywani hayawezi kurudi nyuma na hii ni kutokana na uhuru wa vyombo vyetu vya habari na kukua kwa teknolojia na uwepo wa mitandao wa internet.

Hivyo hawa washauri maalum ni muhimu sana ingawa wanalipwa na malipo ya kazi yao ni kutokana na utaalam wao wa kushauri.

Mwisho , hongera kwa kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha na piga kazi,weka siasa za kiki pembeni, na "make Arusha Great" kiuchumi na financial Center ya nchi ili iweze kuwa mfano kwa mikoa ya Tanzania.
UBINAFSI TU, GAZETI ZIMA
 
UBINAFSI TU, GAZETI ZIMA
Ni mapendekezo.

Leo, meya wa jiji katangaza wamekusanya kodi bilioni 66.6

Hizi ni mara mbili ya zile ambazo walikuwa wakikusanya kabla yaani bilioni 30.

Najiuliza kuna kitu kimepita wamekusanya na kuweka rekodi sasa hivi au tu wameamua safari hii hakuna upigaji?

Nayaheshimu maoni yako.
 
Binafsi nimeona "potential" yako katika uongozi una uthubutu lakini ninahusudu uthubutu wako huo kwamba utachochea harakati za wananchi kujiletea maendeleo.

Mtu akikwambia kuwa, "samahani umefeli katika zoezi la usaili lakini tumeona "potential" ndani yako, fahamu kuwa bado waonekana una uwezo wa aina fulani na hunedna huko baadae ukapitishwa kweye usaili mwingine.

Neno hili "potential" lamaanisha kuwa na uwezo na kuendeleza kitu au mtu kwa ajili ya baadae. Hata mtu akiwa ana duka auza bidhaa, akitokea mteja ambae yupo tayari kununua bidhaa lakini hana fedha wakati huo ila akisema atakuomba uweke bidhaa alochagua pembeni, tayari huyo ni "potential customer".

Kwahiyo umeonekana una "potential" kwa ajili ya baadae nafikiri hichi kitendo kilotokea hivi karibuni ni uthibitisho kuwa una "future" huko mbele.

Hivyo kama kiongozi ulie na dhamana ya kuongoza mkoa ukiwa mwakilishi wa raisi wa Jamhuri ya Muungano, una jukumu la kuja na mikakati hii ikiwa imeweka malengo rasmi yaani kuinua kiwango cha maisha ya wananchi wa Arusha,kutatua migogoro ya ardhi, kuondoa kero za uhalifu, kuinua uchumi wa mkoa, kupunguza tofauti ya kipato, kuhakikisha kodi yakusanywa, kuwashughulikia kisheria wakwepaji kodi na wabadhilifu wa fedha za kodi hiyo na kusimamia na kuimarisha usalama wa mkoa wa Arusha.

Arusha tayari ni mji wa kibiashara kuanzia madini, Utalii mahoteli na biashara zingine nyingi tu.

Mapendekezo yangu kwako nikiwa ni mtu ambae nimeiona Arusha kuwa ina "potential" kiuchumi, basi keti chini na timu yako panga mikakati ya kuifanya Arusha kwa kituo cha biashara Tanzania yaani "Financial Centre of Tanzania".

Kama nilivyosema hapo juu Arusha ina madini, mbuga za wanyama, mahoteli ya kimataifa, kituo cha biashara cha AICC, uwanja mpya wa mpira waja na biashara zingine nyingi tu ambazo zina uwezo wa kuinyanyua Arusha kiuchumi.

Si tu Arusha yavutia wageni watalii kutoka mataifa mbalimbali duniani pakini pia yaweza kuvutia zaidi uwekezaji wa ndai ambapo watanzania wenye fedhawaweza kuleta biashara zao Arusha na kuibadilisha kimuenekano. Nimeona yupo mfanyabbiashara mmoja ambae amenunua hoteli ya kitalii na kuamua kuivunja yote.

Hii ni ishara tosha kwamba endapo tunapata wafanyabiashara zaidi wa ndani basi mzungunguko wa fedha mkoani Arusha waweza kupongeza pato la mkoa na pia kusaidia kuongeza na kupanua soko la ajira khasa kwa vijana mkoani humo.

Arusha ni mkoa unotoa madini pekee duniani ya Tanzanite ambayo hutumika kutengeneza vito ghali katika nchi nyingi duniani khasa Antwerp, Singapore, India na Sauri Arabia. Hii pekee yanofanya Arusha kuwa "Exporter" pekee wa madini hayo jambo linoweza kufutanya kuwa na uchumi imara unofanana na wenzetu wa Botswana.

Botswana walitengeneza mazingira mazuri ya kuwezesha madni ya Almasi kutengenezwa nchini humo na bandikuu ya Botswana kusimamia biashara hiyo kwa umakini.

Utalii pia bado waifanya Arusha kuendelea kuwa kivutio kwa raia wa kigeni nchini. Jambo hili laweza kuangaliwa zaidi ili kuongeza idadi ya watalii kila mwaka. Hii yaweza kufanikiwa tu endapo mkuu wa koa utafanikisha kuwa na programs maalum kwa ajili ya kuitangaza Arusha kupitia tovuti za kibalozi huko nje, matangazo katika sehemu mbalimbali,nje na ndani ya nchi na pia kuwa na vituo maalum katika balozi zetu ili kuvutia zaidi watalii.

Mapato yanopatikana katika mkoa wa Arusha kuanzia kodi ya maendeleo na Utalii , madini vina uwezo wa kuuboresha uwanja wa ndege wa KIA ili kuwa na hadhi inofanana na mkoa wa kimataifa. Majengo ya uwanja huo kwa sasa yana paa za mabati ambayo si taswira nzuri kwa mkoa. Hivyo litakuwa ni jambo la kimaendeleo kufikiria kujenga upya uwanja huo kwa kuupanua zaidi na kuujenga kisasa.

Ndugu mkuu wa mkoa, kama huelewi Arusha ni mkoa ambao ni mali yaani financial Asset ya nchi kutokana na hadi yake kimataifa. Kuwepo tu kwa kituo cha biashara cha kimataifa chaifanya Arusha kuwa kivutio na kuleta shauku kwa wawekezaji wa kimataifa.

Hivyo situ kuna kituo AICC lakini pia kuwa mahakama ya kimataifa ya haki za binadamu na kuna mahakama ya AFCHPR na pia kuna mahakama ya umoja wa mataifa ya ICTR inoshughulikia kseiza mauaji ya kimbari yalotokea Rwanda. Mambo haya yaifanya Arusha kuwa ni kioo cha sheria za nchi na za kimataifa na pia kioo cha sheria za haki za binadamu.

Mazingira mazuri yanoandaliwa na serikali katika sehemu yoyote ile, husababisha kukua kwa ari na mori kwa wananchi kujiletea maendeleo wao wenyewe. Watu wengi duniani bado waishangaa China na kuiangalia kwa jicho la uhasidi kwa namna ambavyo imeweza kuwanyanyua wananchi wa kuipato cha chini kwenda kwenye kipato cha kati.

Hivyo mkuu wa mkoa, huu ni wakati wako wa kuonyesha umahiri wako katika kuhakikisha wapata njia sahihi za kuwanyanyua wananchi wa kipato cha chini wa Arusha na kuwa na uwezo kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ni wakati wa kufanya tathmini ya kutambua ni viwanda vipi vyahitaji kuboreshwa au msaada wa fedha ili kujiimarisha. Tusisahau Arusha iliwahi kuwa na kiwanda cha kutengeneza matairi cha General Tyre ambacho leo hii ni historia,je ni kwanini tulishindwa kukiimarisha kiwanda hichi?, haya ndo masuali ambayo yataleta majibu na namna ya kuweza kuangalia uwezekanio wa kua na viwanda kama hichi.

Viwanda vidogovidogo "Smallscale industries" navyo ni sehemu ya uchumi wa sehemu yoyote na litakuwa ni jambo la kimaendeleo ikiwa kutatengwa eneo maalum au "Industrial Estate" ambalo litasheheni biashara zote ndogondogo ambazo zatambulika na zote kulipa kodi kulingana na mapato yao.

Mafuriko yanotokea sasa na kuathiri maeneo mengi ni dalili ya miundombinu mibovu au ulokosa kufuatiliwa. Hivyo ujenzi wa miundombinu bora itasaidia kupinguza athari za mafuriko na pia kuwezesha mkoa kuwa na njia safi na salama za magari na watembea kwa miguu.

Bado Arusha ni soko linokuwa yaani (emerging market). Soko linokuwa ni lile soko ambalo lina viashiria vyote vya soko liloendelea lakini halijafikia viwango vinotakiwa. Hivyo ni lazima viashiria hivi viwepo na hapo ndipo Arusha yaweza kuongeza uchumi wake na pia kuvutia aina zingine za uchuni kama ule uchumi wa gig enonomy ambao wahusisha biashara za kuagiza vyakula kupitia mtandao wa internet au simu ya mkononi.

Aina hii ya uchumi wa internet waweza kuwasaidia vijana kujiajiri katika maeneo ya usafirishaji abiria na kusambaza vyakula. Ajira za namna hii zitawafaa wale vijana ambao hawana ajira rasmi lakini ambao wanakuwa wamejiandikisha TRA. Hivyo biashara kama ya Uber na Uber Eat zaweza kuwa ni moto au Hot-cake katika mji.

Hivyo mkuu wa mkoa mimi nimekupa mawazo ambayo nina uhakika yaweza kukutoa katika siasa za malumbano na kutafuta kiki kama ambavyo itaweza kutafsiriwa na mahasidi wako. Kazi ya uongozi ni ngumu lakini kwa nchi hizi zetu za Kiafrika imegundulika kuwa bila msukumo (unofuata sheria) nchi yetu/ zetu haiwezi kuendelea.

Mwisho "but last", ndugu mkuu wa mkoa tafita washauri maalum wa kukusaidia kazi yako mkoani Arusha. Katika video ilowekwa hivi majuzi katika mitandao ya kijamii kuna makosa kadhaa ambayo yahitaji ushauri maalum. Washauri hawa maalumau "special advisors" ni watu maalum wenye uwezo na utaalm wa kushauri viongozi namna ya kujiweka kwenye macho ya umma.

Hawa watashauri namna ya kuandaa hotuba yako na pia watashauri na kutathmini hotuba hiyo hata kama haikuandikwa. Ukumbuke kuwa hotuba au maneno yoyote mara tu yatokapo kinywani hayawezi kurudi nyuma na hii ni kutokana na uhuru wa vyombo vyetu vya habari na kukua kwa teknolojia na uwepo wa mitandao wa internet.

Hivyo hawa washauri maalum ni muhimu sana ingawa wanalipwa na malipo ya kazi yao ni kutokana na utaalam wao wa kushauri.

Mwisho , hongera kwa kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha na piga kazi,weka siasa za kiki pembeni, na "make Arusha Great" kiuchumi na financial Center ya nchi ili iweze kuwa mfano kwa mikoa ya Tanzania.
Safi
 
Kwa mfano China kupitia chama chake cha CCP kamati kuu yake imepanga mpango wa maendeleo tokea miaka ya 1800s.
Chai ina magaidi.

Chama cha kikomunisti cha China kimeanzishwa mwaka 1921 na mwaka 1949 kimeunda serikali.

Wewe hii 1800s umeipatia wapi ? 1800s unafahamu hata China ilikuwa katika hali gani ?
 
Tumekuwa twaambiwa kuna ilani ya uchaguzi yasema hivi na vile na pia kuna mpango wa maendeleo wa 2015-2025.

Je, haya yote yamefikia kiasi kipi?

Kwa mfano China kupitia chama chake cha CCP kamati kuu yake imepanga mpango wa maendeleo tokea miaka ya 1800s.

Mpango wa sasa hivi waitwa 14th five year plan wa 2021-2025 na wahakikisha mipango ya maendeleo hadi kufikia mwaka 2035 yote itakuwa imekamilika kwa manufaa ya wananchi wa China.

je, mpango wa maendeleo wa 2025 kwa CCM utapitiwa vipi ili kuona wapi umefikia na wapi umekwama?
Nyie Five Year Plans zenu huwa zipi toka kuanzishwa kwa taifa la Tanzania na huwa mnazitimiza ?
 
Labda atafute za kwake awekeze
Na ndio atakachofanya
Kwa utawala wa Afrika kuteuliwa tu ni utajiri tosha wa kuanza kujilimbokizia miradi ya haram na halali
Hapo akikaa mda utaona ana machimbo na hotel za kitalii

Hakuna anaejali haya unayosema kwani sio kazi yake hiyo
Ni kawaida kwa nchi za kiafrika viongozi kugeuza nafasi za kisiasa kuwa mitaji ya kujinufaisha binafsi na familia zao.

Hili haliepukiki na ni vigumu kwa nchi yenye mfumo wa Kleptokraia kama ya kwetu.

Lakini pia ipo nafasi kwa zile ngazi za chini kuhakikisha zpiga kazi ili kuboresha maendeleo ya chini kabisa yaani ya msingi au twasema basic needs.

Ndo maana leo meya wa jiji la Arusha katangaza mapato zaidi ya bilioni 66 ambayo yatapelekwa kwenye mahitaji ta msingi kabisa, elimu, afya, miundombinu imara itozuia mafuriko kuleta madhara na vingine vodogovidogo.

Lakini hapohapo maoni yangu yatoa fursa kwa mkuu wa mkoa kutukiza kichwa na kupiga kazi ili kuigeuza Arusha kuwa "financial centre" ya Tanzania.

Akiwa busy na hili atakosa ule muda wa kufuatilia mambo yaso maana.
 
Chai ina magaidi.

Chama cha kikomunisti cha China kimeanzishwa mwaka 1921 na mwaka 1949 kimeunda serikali.

Wewe hii 1800s umeipatia wapi ? 1800s unafahamu hata China ilikuwa katika hali gani ?
Mkuu, kufikia mwaka 1820 pato la taifa la China yaani GDP lilikuwa zaidi ya mara sita kwa Uingereza na Marekani.

Ni hapo baadae vita ya wenyewe kwa wenyewe Chinese Civil War kati ya mwaka 1927 na 1949 ndo ilirudisha nyuma uchumi wa China.

Na kuundwa kwa CCP ni mwendelezo wa tokea mapinduzi ya Russia au Russia Revolution ya mwaka 1917.

Soma historia uelewe.
 
Kuna sababu nyingi zaweza kuifanya city yoyote kuwa kugeuzwa kuwa financial center bila kuangalia sana nje ya nchi.

1. Tayari Arusha ni tourist destination na sio Tourist hub kama ilivyo Dubai ya leo.

2. Miji mingine uloongelea ni financial capitals kama London na New York ambayo ina pia soko la mitaji (Stock Exchange), hivyo Arusha yaweza tu kuwa Finacial center ya Tanzania ikihudumia mikoa jirani ili nayo iwezo kunyanyuka kiuchumi.

Kinotakwia ni kitu twaita kwa kiingereza revitalization yaani kuigeuza na kuibadili Arusha kuwa Financial Center kwani tayari kuna benki kuu hapo na kituo cha kimataifa cha AICC na biashara zingine kubwa tu.
Unaandika pumba tu kwa vile umetumwa na Bashite. Endelea kwa vile mnalipwa ujira wa siku kuandikq kwenye social media. Ila ni pumba
 
Kwani Arusha kijiigrafia haifai kuwa financial centre?

Au Arusha haina ardhi ya kutosha?

Arusha pia upo mpaka ambao kwa mtu mwenye maoni tayari ni kitega uchumi kizuri kwa mkoa.

Au weye ni mzaramo wa hapo Chalinze?
Hujui kitu unachoandika, unajaza servers na pumba tu
 
Mkuu, kufikia mwaka 1820 pato la taifa la China yaani GDP lilikuwa zaidi ya mara sita kwa Uingereza na Marekani.

Ni hapo baadae vita ya wenyewe kwa wenyewe Chinese Civil War kati ya mwaka 1927 na 1949 ndo ilirudisha nyuma uchumi wa China.

Soma historia uelewe.
Vitu gani hivi vya ajabu unaandika.

1800s chama cha kikomunisti cha China hakikuwepo wala itikadi za kikomunisti China hazikuwepo.

Unaandika vitu vya ajabu humu.
 
Unaandika pumba tu kwa vile umetumwa na Bashite. Endelea kwa vile mnalipwa ujira wa siku kuandikq kwenye social media. Ila ni pumba
Mkuu jikite kwenye mada, tuache chuki binafsi, halafu mie ni mjasiriamali nina kipato changu cha maana.

Hapa nimejituma kuandika mapendekezo tu basi.
 
Vitu gani hivi vya ajabu unaandika.

1800s chama cha kikomunisti cha China hakikuwepo wala itikadi za kikomunisti China hazikuwepo.

Unaandika vitu vya ajabu humu.
Mkuu, tafuta muda usome historia ya China hadi karne ya 19 ambayo ndo mwaka 1800 waanzia.

Kisha andika mada tuchangie.

Hapa twapoteza lengo la mada yangu.
 
Mkuu, tafuta muda usome historia ya China hadi karne ya 19 ambayo ndo mwaka 1800 waanzia.

Kisha andika mada tuchangie.

Hapa twapoteza lengo la mada yangu.
Mada ina assumptions zilizojengwa kwenye taarifa uwongo na kukosa uelewa wa unachotaka (lack of knowledge in the subject matter), haiwezi kujadilika. Ni kupoteza muda tu
 

Unayempa ushauri sasa ni typical zero brain.
 
Back
Top Bottom