Group conformity and African culture ni mojawapo ya sababu kubwa za Watu weusi kuendelea kuwa Maskini, Wakati weusi mnaitana majina yakukatishana tamaa km Mario, Goal keeper na kuogopa ke'' wenye hela. Wazungu wao wanaamini ''kila mwanaume mwenye mafanikio nyuma yake kuna Mwanamke'', wanajali, kulinda mke na mnyama kwa hali ya juu! ndiyo siri walio nayo!
Mwanaume Oa tu hata km amekuzidi kipato ukinyanyasika ni fursa adimu kwako, ichukulie kama changamoto, kichocheo cha kukutoa kwenye Umaskini, tumia hela zake kujinufaisha ili mwisho wa siku uwe hela kumzidi yeye!! na uendelee kumheshimu na kumpenda zaidi kwa kukunyanysa. uwe makini tu asikuue!
Hata ukikwepa ujue unaweza oa mwanamke Goal keeper, House girl maskini lkn na bado akatajirika kukupita kwa kutumia hela zako hizo!! kwakujiunga na vikoba tu akafika mbali sasa je utamuacha?
Mleta Mada kumbuka tuna Ma boss wanawake maofisini kwetu huko, Waalimu, wafanyakazi wenzetu ke'' tunaolingana kipato lkn wanazo, Jeshini huko ndo usiseme ki-mdada kinalingana na mdogo wako lkn unakapigia saluti na kanakutuma. utasikia ''weee kopro kuja hapa!!!
Umesahau JKT wakati ukiwa Kuruta? unaonaje vile vidada vikopro vilivyokuwa vinawaendesha, una ndevu na Degree yako ya mlimani!!! huko kooote ni wewe ujifunze ! sidhani kwa mtu aliyepita huku ataogopa kuitwa Mario!!! lkn wengine hatuwalaumu sababu hawajui.
Matajiri wengi ni wake zao ndo kisababishi, akimwaacha tu kwa dharau bila chochote na kuoa mke mwingine, lazima utajiri uporomoke! na wengine kuwa maskini kabisaa kama ''Yego store''. Matajiri hutafuta wanawake/ume wenye harufu ya utajiri. waoane na watoto wao!