Bwana Utam
JF-Expert Member
- Feb 15, 2016
- 19,559
- 36,514
Heheeee [emoji3]Weweee ni mwoga balaaa hata kovu la kiwembe mwilini mwako hakuna
Nakumbuka kuna mwaka wakati nipo zangu chuo
Natoka zangu nipo njiani sina hili wala lile kulikua na maandamano
Kinondoni makaburini pale nilishuka ghafla nasikia mabomu nilichapa mbio asee zabalaa maana sikutegemea kwakweli nikaingia ndani nyumba hata siijui
Kufika mule wenyewe wanakula pilau na juisi safi kabisa mida kama hii
Nikaambiwa vipi kijana nikawaambia natoka zangu chuo naona mabomu yanarindima nimekuja kujistiri
Nikasikia grace (jina silikumbuki ila walikua wakristo) leta glass moja na sanahani tumepata mgeni
Wenyeji kama waliona tumboni nikaekewa mzigo wakutosha nikaubonda pale mzee yule akanambia ngoja ngoja kidogo hapa patulie
Kweli kama saa nane kasoro kidogo nikasepa zangu
Allah ampe khairat yule mzee na familia yake
Vita sio maskhara mzee [emoji3][emoji1787][emoji3]