Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Nafuatia makala maalum kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 1964, zinazorushwa mfululizo na Idhaa ya KIswahili ya BBC kila siku kuanzia 1:00-1:30.

Katika kipindi cha leo, Mmoja wa askari aliyekuwa zamu ikulu ya Sultani, kwa jina maarufu la Mzee Sukari, anasimulia first hand information kuhusu mapinduzi hayo! akihojiwa na Baruan Muhuza wa BBC. Amekiri kuwa Sultani hakufukuzwa Zanzibar, alikuwa akitafutwa hivyo alitoroka mwenyewe!, na baada ya Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, waarabu hawakufukuzwa Zanzibar, bali walijiondokea wenyewe!

Huu ni ushuhuda uliotolewa na shuhuda halisi wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambae simulizi yake ni tofauti na urongo mwingi tuliolishwa na maandishi ya mahasidi wa Mapinduzi.

Kesho kutafanyika mjadala maalum kuhusu Mapinduzi hayo Matukufu ya Zanzibar utakaoanza saa 12:45-1:30.
Baada ya mapinduzi Zanzibar - BBC Swahili - BBC.com
Zanzibar na miaka 51 ya Mapinduzi - BBC Swahili


Siku ya kilele, kutatolewa nishani maalum za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, sijui kama yule shujaa halisi wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Field Marshal John Okello, atakumbukwa!

Paskali


 
Pasco,

Kumbe hivi ndivyo unavyofanya research au ndio umepanga na kina Salim Kikeke muyatkufushe hayo Mauwaji thru BBC na. wewe ndie field corespondent mpaka 13/1/2014. Teh teh. Poor Pasco
 
Pasco tatizo lako wewe ni ktk wale watanzania wachache ambao lengo na dhumuni lao kila waongeapo au waandikapo ni kuchokonoa vile ambavyo kwa namna moja au nyingine vitasababisha chuki!

Sijakuona hata siku moja ukiongelea ubaya na unyama waliotufanyia wazungu hapa!

Uwaonao wewe ni WAARABU TU!
And guess why! Yoote ni kwa kuwa walikuwa WAISLAMU!
Pasco hapa hakuna mtoto mdogo! Na japo utakana hili lkn nadhani tunakufahamu muda sasa!

Wewe ni msukuma ambae umewaasi hata hao wazee wako.
Nikuulize swali la msingi hapa!

Huu utukufu wa haya mapinduzi kwa mtazamo wako wewe ni UPI HASA!

Wazee wetu wamepoteza maisha yao. Watoto wetu wamechinjwa. Damu imemwagika kwa.pande zote mbili!
We hasa huo uuitao utuKufu ni NINI.?

HEBU tujuze kidogo! Manake we mtu wa baliadi unaonekana kuyafahamu mapinduzi kuliko wazanzibari wenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco

Tahadhali tujadiliane kwa hoja sababu haukawii kuita watu mainzi, njoo na ushahidi wako wa hayo Mapinduzi Matukufu na wengine waje na ushahidi wao kama Mapinduzi yalikuwa ni mauaji ya kimbari.
 
Last edited by a moderator:
Watu wanaofikiri kwa kutumia MAKATO utawajua tu. Mtu katoa hoja bila kuutaja uislamu wewe unaanza kujihami. Kwani waarabu kuwa waislamu ndio kwamba hawakutenda ubaya? Waarabu si ndio wanaua waislamu wenzao kule Dafur? Mada inawahusu waarabu na si wazungu. Tumia kichwa kufikiri na sio hicho kiungo cha biashara yenu kule znz na Tanga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…