Mapishi ya nazi ni overrated sana kwa vyakula vingi

Mapishi ya nazi ni overrated sana kwa vyakula vingi

Afu kuna wali ulotiwa njegere Nazi ikolee.Utajilamba mbona.Kisamvu mi nakifurahia kikiwa na karanga.(Sijui kwa sababu pishi hili nilijifunzia Mwanza kwa mara ya Kwanza alienifundisha aliniambia niweke karanga.)
 
Pilau la Dengu. Ni msukuma tu au aliekulia usukumani ndio anaweza kula lile pishi.
Mafuta ya samli. Kama hujakulia kwa wafugaji sijui kama utayaweza.
Umenikumbusha dengu na wali sijala kitambo
 
Umezaliwa mkoa wa mara nini? Wale jamaa hawana mbwembwe kwenye mapishi hata samaki huwa hawaoshi vizuri wanachemsha na nyanya nzima na maganda yake ukimaliza kula unanuka shombo ya samaki hata wiki 3
Ukweli mtupu
 
Back
Top Bottom