Mapokezi ya Mwenge Dodoma: Wilaya ya Bahi yafanya Kufuru

Mapokezi ya Mwenge Dodoma: Wilaya ya Bahi yafanya Kufuru

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi, kama kawaida yangu, nipatapo nafasi, huzungukia maeneo mbalimbali ya nchi yetu kushuhudia haya na yale.

Leo nimepata fursa kushuhudia shamra shamra za mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mkoani Dodoma.

Jana Mwenge ulilala Kijiji cha Mwitikira Wilaya ya Bahi. Mambo niliyoyaona usiku wakati wa mkesha wa mwenge, naomba nisiyateje yasije kuniharibia flow ya thread yangu hii.

Leo asubuhi Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Chalamila Mkwasa (Mama Master) amemtambulisha kiongozi wa Chadema wa eneo hilo na kusisitiza Wakuu wa wilaya ni watumishi wa wote, kazi yao ni kuhimiza maendeleo kwa kushirikiana na wote bila kujali itikadi za vyama ndio maana hata kiongozi wa Chadema amekaribishwa!.

Mwenge umeanza mbio zake wikayani Bahi saa 4:00 asubuhi hii kwa kuwekwa jiwe la msingi ukumbi wa kisasa wa mikutano uliogharimu shilingi Milioni 65 zilizochangwa na wananchi kwa asilimia 100%.

Kiukweli wilaya ya Bahi imefanya kufuru kwa jinsi walivyojipanga kuanzia sare maalum kwa watumishi wote wa umma wilaya ya Bahi.

Ule mtindo wa kuwatumia watoto wa shule kwenye shughuli za kitaifa unaendelea!. Japo leo ni siku ya Jumapili, wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wametinga uniform na kujitokeza kwa wingi (inaonyesha wamelazimishwa maana ni hadi watoto wa darasa la kwanza!

Japo significance ya mwenge wa uhuru ni issue debatable, mada hii sio subject matter ya thread yangu hii. Mimi najikita kwenye Kufuru za Bahi.

Fuatana nami kwa siku nzima ya leo nikiwaletea kila kinachojiri katika mapokezi ya Mwenge wilayani Bahi.

Karibu

Pasco
 
Nimerudia tena na tena kujaribu kukuelewa Pasco nimeshindwa. Ulitaka tujue kuwa Betty kamtambulisha kiongozi wa Chadema? Au kwamba Mkesha wa Mwenge unasababisha uchafu au Wana Bahi kuchangia Mil 65 kwa 100% au Suala la mwenge kuwa debetable? Au ulitaka kutusimulia hadithi tujue kuwa ulifika Bahi kijiji cha Mwitikira?
 
Last edited by a moderator:
Kuanzisha sare za wafanyakazi wa serikali? Pasco nani anagharamia?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco unaweza ukakadiria kutokana uzoefu wako ni kiasi gani cha pesa kimetekea ili kuuleta Mwenge Bahi kuzindua Mradi wa 60mil. Namaanisha

1. Sare
2. Posho
3. Mafuta ya mashangingi
4. Food and Entertainment
4. Overheads
 
Last edited by a moderator:
Hivi sasa wameweka jiwe la msingi la hostel ya wasichana shule ya msingi ya Mwitikira iliyogharimu Shilingi milioni 45!.
 
Dr Slaa yupo Dodoma?
Anatua leo saa 8 mchana na chopa ya Ndesa Pesa ambapo bado inaendelea kuitwa Helcopter ya Mbowe hata kama Mbowe hajatua nayo!

Nitawashauri Chadema endapo watachukua nchi 2015 kutokana na makosa ya CCM kutomsimamisha yule mgombea, then serikali ya Chadema iwajibike kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa kwa kuendeleza mbio za mwenge ila wauzungushe kwa helcopter!

P.
 
Dr Slaa yupo Dodoma?
Mkuu Deshmo, Dr. Anatua leo saa 8 mchana na chopa ya Ndesa Pesa ambapo bado inaendelea kuitwa Helcopter ya Mbowe hata kama Mbowe hajatua nayo!

Nitawashauri Chadema endapo watachukua nchi 2015 kutokana na makosa ya CCM kutomsimamisha yule mgombea, then serikali ya Chadema iwajibike kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa kwa kuendeleza mbio za mwenge ila wauzungushe kwa helcopter!
P.
 
Pasco, hebu jaribu kuleta post za maana, hizi habari za kibatari -mwaka 2013 ni utani usiokubalika!
 
Hivi sasa Mwenge umeingia kijiji cha Mtitaa ambapo wamezindua mradi wa ufugaji bora na kisasa wa ng'ombe wa maziwa kwa kikundi cha wazee wasioona wa Mtitaa uliogharimu Shilingi milioni 11.5
 
Mwenge upigwe marufuku ni uchafu mtupu unafanyika kwenye mkesha, pia pesa nyingi zinachangishwa toka kwa walimu bila ridhaa yao na wanaishia kujishonea sare huu ni upumb.av.u
 
Anatua leo saa 8 mchana na chopa ya Ndesa Pesa ambapo bado inaendelea kuitwa Helcopter ya Mbowe hata kama Mbowe hajatua nayo!.
Nitawashauri Chadema endapo watachukua nchi 2015 kutokana na makosa ya CCM kutomsimamisha yule mgombea, then serikali ya Chadema iwajibike kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa kwa kuendeleza mbio za mwenge ila wauzungushe kwa helcopter!.
P.

Kaka Pasco mgombea ameishaanza kuhundiwa zengwe nn? Mbona unajiahami mapema...Team EL mnawoga sana..by the way ulinihaidi kunambia salva wenu nani ila mpaka leo haujasema!
 
Mkuu Pasco haya mambo ya Kilosa hujayasikia kuwapo?
ImageUploadedByJamiiForums1376815149.194747.jpg
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi, kama kawaida yangu, nipatapo nafasi, huzungukia maeneo mbalimbali ya nchi yetu kushuhudia haya na yale.

Leo nimepata fursa kushuhudia shamra shamra za mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mkoani Dodoma.

Jana Mwenge ulilala Kijiji cha Mwitikira Wilaya ya Bahi. Mambo niliyoyaona usiku wakati wa mkesha wa mwenge, naomba nisiyateje yasije kuniharibia flow ya thread yangu hii.

Leo asubuhi Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Chalamila Mkwasa (Mama Master) amemtambulisha kiongozi wa Chadema wa eneo hilo na kusisitiza Wakuu wa wilaya ni watumishi wa wote, kazi yao ni kuhimiza maendeleo kwa kushirikiana na wote bila kujali itikadi za vyama ndio maana hata kiongozi wa Chadema amekaribishwa!.

Mwenge umeanza mbio zake wikayani Bahi saa 4:00 asubuhi hii kwa kuwekwa jiwe la msingi ukumbi wa kisasa wa mikutano uliogharimu shilingi Milioni 65 zilizochangwa na wananchi kwa asilimia 100%!.

Kiukweli wilaya ya Bahi imefanya kufuru kwa jinsi walivyojipanga kuanzia sare maalum kwa watumishi wote wa umma wilaya ya Bahi!.

Ule mtindo wa kuwatumia watoto wa shule kwenye shughuli za kitaifa unaendelea!. Japo leo ni siku ya Jumapili, wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wametinga uniform na kujitokeza kwa wingi (inaonyesha wamelazimishwa maana ni hadi watoto wa darasa la kwanza!.

Japo significance ya mwenge wa uhuru ni issue debatable, mada hii sio subject matter ya thread yangu hii. Mimi najikita kwenye Kufuru za Bahi.

Fuatana nami kwa siku nzima ya leo nikiwaletea kila kinachojiri katika mapokezi ya Mwenge wilayani Bahi.

Karibu

Pasco


sijui nani tu atakuja kuniondolea hii kero aiweke makumbusho.inatafuna kodi zetu tu bila sababu maalum
 
Nchii bhana mie mpaka leo sielewi umuhimu wa mbio za mwenge licha ya kutumia pesa nyingi! Mambo ya kizamani kweli
 
ulazima ni upi mwenge kuzindua mradi,hasara na faida ni ipi ikiwa mwenge hautahusika ama kuhusika kwenye uzinduzi wa chochote? nitafurahi keleweshwa hili
 
Sasa unataka kusema nini hapa? I mean what is your point?
Mkuu Mzito K, vuta subra, 'the nearer the bone, the sweeter the meat!'. Hapa ndio kwanza safari imeanza, just follow, I'm serving the best for the last!. Mwishoni utanielewa!.
P.
P.
 
Mbio za Mwenge zimeingia kijiji cha Nondwa na kuweka jiwe la msingi mradi mkubwa wa maji, uliogharimu Shilingi milioni 270!.
 
Back
Top Bottom