rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 16,784
- 23,312
Hata waliocheza jana sio wabaya..Viungo bora kabisa Fei,Banka na Bui wanakaaje jukwaani au Wanzanzibar???
mechi karibu 6, hadi sasa zimechezwa pale lakini hakuna hata moja iliyotoka na ushindi ndani ya dakika 90... timu zetu si mbovu kiasi hicho, hadi kushindwa kupata ushindi kwenye uwanja wetu wenyewe, ukilinganisha na timu pinzani...
Mimi ni Yanga na inajulikana cross za Gadiel hazina macho siku zote. Anafaa kuwa kuwa traditional left back sio attacking wing back.Timu ilicheza vizuri kuanzia nyuma mpaka katikati japo kulikuwa na mapungufu ya Gadiel na Maganga kupiga krosi ambazo hazina macho. Makocha tuwape muda waendelee kwani sasa hivi japo timu inafungwa walau kidogo inaonyesha uhai wa kupambana. Nikiitizama timu ya sasa na ile ya Amunike naona hii ya sasa inahitaji marekebisho kwenye upande wa ushambuliaji kwani mabeki na viungo walipeleka mipira mbele lakini Nado, Chilunda na Lyanga walikuwa wanajigonga tu. Lakini makocha wetu nao wajifunze sio kila wakati lazima ucheze na washambuliaji mbele tunaona hata timu kubwa ulaya mara nyingine zinawatumia viungo waliotulia kuwa washambuliaji kwenye baadhi ya mechi. Kwa sababu kama mipira ilikuwa inafika mbele mara nyingi tu kilichohitajika ni mtu tu hata beki mwenye utulivu wa hali ya juu na jicho la mwewe kuutumbukiza mpira ndani ya goli.
Kwa upande wangu naona matatizo ya timu ya taifa yapo zaidi kwa washambuliaji namba 9 na 10. Boko umri umeanza kumtupa mkono na ana majeraha ya mara kwa mara, hawa Nado na Chilunda ni washambuliaji wa pembeni zaidi au nyuma ya striker namba 9 na tuwategemee zaidi baadaye na sio sasa. Kiujumla hatuna mshambuliaji mwenye uwezo binafsi wa kuamua matokeo ndio maana tulicheza sisi mpira muda mwingi wa mchezo lakini Sudan walifika kwetu mara mbili tu na hapo wakapata bao moja. Baada ya bao ndio wakaanza wao kucheza mpira. Watanzania kwa ujumla tuwape moyo vijana wetu wenye maumbo makubwa waanze kucheza soka badala ya kukimbilia basketball na kuwa mabaunsa kwani soka la sasa pamoja na ufundi linahitaji pia nguvu.
Sijadili lolote na mtu asiye na hoja ulishanitukana basi yaishie hapotuanzie hapa.. ulikuwa na mantiki gani kunitag kwenye nukuu zile mbili...
ACHA KUPOTOSHA WEWE SASA KATIKA MAZINGIRA KAMA YALE ULITAKA KASEJA AFANYE NINI?Kuna watu niliwaambia acheni kumu_overrate Kaseja kipimo chake kinanza na Sudan ngoja nifukue makaburi sasa
sawa,Sijadili lolote na mtu asiye na hoja ulishanitukana basi yaishie hapo
Mi nadhani Kelvin Yondani alikasirika sana baada ya kuona kule mbele mipira inakwenda sana lakini wamalizaji wamezubaa tuu. Ndio maana kwa hasira akajaribu yeye mwenye kupiga mashuti ya mbali. Ingawa baadaye nadhani hasira zilipungua akarudi kwenye kucheza kitimu zaidi. Na kwa kweli ilikuwa inakera sana mipira mingi inafika mbele kabisa golini lakini kuna vijamaa vitatu hivi pale mbele vipo vipo tu hata kutuliza mpira haviwezi kabisa. Badala ya kufunga vinaokoa kama cross mbili hvi.wasudan ni warefu lakini cross nyingi zilikuwa zinapigwa mipira ya juu tatizo jingine ni timu yetu kushindwa kupiga mashuti ya maana wanapokuwa karibu na goli au kupiga mashuti sehemu ambayo hawastahili kama mashuti aliyokuwa anapiga kelvin yondan, Boniface naganga alikuwa na tatizo la kuchelewa kufanya maamuzi wachezaji wanacheza utafikili wana bifu fulani mtu yuko kwenye nafasi nzuri ya kupewa mpira hapewi badala yake mpira unapotezwa bila sababu ya msingi
We kazi yake huijui?ACHA KUPOTOSHA WEWE SASA KATIKA MAZINGIRA KAMA YALE ULITAKA KASEJA AFANYE NINI?
Kijana usipoteze muda wako kwa ku-assume mambo. Hayo mambo ya angekuwa yeye..... ni sawa na kujaza takataka kichwani mwako. Deal na mambo yaliyotokea uwanjani na yajayo!We kazi yake huijui?
.
Kash kash alizokuwa anakutana nazo Golikipa wa Sudan angezipata Kaseja ina maana angekula saba sasa.
Yani mtu kazi yake ni kuokoa mipira isiingie kwenye nyavu alafu unauliza angefanya nini looooh!
Mimi naujua mpira usidhani ni tumbotumbo mimi.Kijana usipoteze muda wako kwa ku-assume mambo. Hayo mambo ya angekuwa yeye..... ni sawa na kujaza takataka kichwani mwako. Deal na mambo yaliyotokea uwanjani na yajayo!
Tanzania kwa sasa ina washambuliaji namba 9 chipukizo wengi sema hawapewi nafasi.. kocha yupo radhi kilazimisha beki acheze namba 9 lakini sio kuwaita hawa chipukizi.
Kelvin John
Andrew simchimba
Onesmo mayaya
Salim aye
Hawa ni vijana wazuri sana kwa kufumania nyavu na wameomyesha uwezo wa hali ya juu sana kwenye timu za vijana.
Kwanini makocha hawataki kuwamini vijana hawa.
Mbele ya goli ni akili ya striker.. na sio umbo la mtu.
Haaaaaahaaaaa tupigwe tu!Timu imejaa wachezaji waliopigwa na Ud Songo unategemea vp kushinda
Hakuna timu imejaa usimba na Azam tupigwe tu tangu matola awe pale anaita madogo wote aliokuwa nao lipuli na Simba kocha wenu nae kijana wake chilunda anaruka ruka tu ple mbele!Hata waliocheza jana sio wabaya..
Akina FEI watagusa kule Sudan
Ah..huyo kocha humwambii kitu kwa wachezaji wake wa Azam!Mi nadhani Kelvin Yondani alikasirika sana baada ya kuona kule mbele mipira inakwenda sana lakini wamalizaji wamezubaa tuu. Ndio maana kwa hasira akajaribu yeye mwenye kupiga mashuti ya mbali. Ingawa baadaye nadhani hasira zilipungua akarudi kwenye kucheza kitimu zaidi. Na kwa kweli ilikuwa inakera sana mipira mingi inafika mbele kabisa golini lakini kuna vijamaa vitatu hivi pale mbele vipo vipo tu hata kutuliza mpira haviwezi kabisa. Badala ya kufunga vinaokoa kama cross mbili hvi.
MECHI YA JANA ILIKUWA NI YA TAIFA STAAZ ILA KWA KWELI WASHAMBULIAJI WALITUANGUSHA KABISA. NASHANGAA KWA NINI KOCHA HAKUALIONA HILO MAPEMA NA KUWAPA NAFASI WENGINI AMBAO WANGEWEZA KUBADILISHA MCHEZO PALE MBELE.