Mapungufu niliyoyaona mechi ya jana Tanzania VS Sudan

Mapungufu niliyoyaona mechi ya jana Tanzania VS Sudan

wasudan ni warefu lakini cross nyingi zilikuwa zinapigwa mipira ya juu tatizo jingine ni timu yetu kushindwa kupiga mashuti ya maana wanapokuwa karibu na goli au kupiga mashuti sehemu ambayo hawastahili kama mashuti aliyokuwa anapiga kelvin yondan, Boniface naganga alikuwa na tatizo la kuchelewa kufanya maamuzi wachezaji wanacheza utafikili wana bifu fulani mtu yuko kwenye nafasi nzuri ya kupewa mpira hapewi badala yake mpira unapotezwa bila sababu ya msingi
 
Taifa stars kichwa cha mwendawazimu nisha kizoea,

Siku zingine kipo sawa na siku zingine ndo kabisa hakisomeki kinaokota makopo.

Matokeo katili sana ya jana dah ndo mpira huo lakin wapambane rounde ya 2 ili tuwatoe ata kwa penalty.
 
Mkuu unahangaika na kikundi cha kubeti... hujawazoea tu hao?
Dah boss kuna mtu nilidhani anajitambu kumbe chenga kabisa yani hana hata za kufikiri alafu ni member mpya isitoshe kala ban hii ni akaunti yake mpya anaitafuta nyingine kwa nguvu
.
Ahyan
 
Kwa hiyo unataka kusemaje kitaalam?
mechi karibu 6, hadi sasa zimechezwa pale lakini hakuna hata moja iliyotoka na ushindi ndani ya dakika 90... timu zetu si mbovu kiasi hicho, hadi kushindwa kupata ushindi kwenye uwanja wetu wenyewe, ukilinganisha na timu pinzani...
 
Timu ilicheza vizuri kuanzia nyuma mpaka katikati japo kulikuwa na mapungufu ya Gadiel na Maganga kupiga krosi ambazo hazina macho. Makocha tuwape muda waendelee kwani sasa hivi japo timu inafungwa walau kidogo inaonyesha uhai wa kupambana. Nikiitizama timu ya sasa na ile ya Amunike naona hii ya sasa inahitaji marekebisho kwenye upande wa ushambuliaji kwani mabeki na viungo walipeleka mipira mbele lakini Nado, Chilunda na Lyanga walikuwa wanajigonga tu. Lakini makocha wetu nao wajifunze sio kila wakati lazima ucheze na washambuliaji mbele tunaona hata timu kubwa ulaya mara nyingine zinawatumia viungo waliotulia kuwa washambuliaji kwenye baadhi ya mechi. Kwa sababu kama mipira ilikuwa inafika mbele mara nyingi tu kilichohitajika ni mtu tu hata beki mwenye utulivu wa hali ya juu na jicho la mwewe kuutumbukiza mpira ndani ya goli.

Kwa upande wangu naona matatizo ya timu ya taifa yapo zaidi kwa washambuliaji namba 9 na 10. Boko umri umeanza kumtupa mkono na ana majeraha ya mara kwa mara, hawa Nado na Chilunda ni washambuliaji wa pembeni zaidi au nyuma ya striker namba 9 na tuwategemee zaidi baadaye na sio sasa. Kiujumla hatuna mshambuliaji mwenye uwezo binafsi wa kuamua matokeo ndio maana tulicheza sisi mpira muda mwingi wa mchezo lakini Sudan walifika kwetu mara mbili tu na hapo wakapata bao moja. Baada ya bao ndio wakaanza wao kucheza mpira. Watanzania kwa ujumla tuwape moyo vijana wetu wenye maumbo makubwa waanze kucheza soka badala ya kukimbilia basketball na kuwa mabaunsa kwani soka la sasa pamoja na ufundi linahitaji pia nguvu.
Mimi ni Yanga na inajulikana cross za Gadiel hazina macho siku zote. Anafaa kuwa kuwa traditional left back sio attacking wing back.
 
wasudan ni warefu lakini cross nyingi zilikuwa zinapigwa mipira ya juu tatizo jingine ni timu yetu kushindwa kupiga mashuti ya maana wanapokuwa karibu na goli au kupiga mashuti sehemu ambayo hawastahili kama mashuti aliyokuwa anapiga kelvin yondan, Boniface naganga alikuwa na tatizo la kuchelewa kufanya maamuzi wachezaji wanacheza utafikili wana bifu fulani mtu yuko kwenye nafasi nzuri ya kupewa mpira hapewi badala yake mpira unapotezwa bila sababu ya msingi
Mi nadhani Kelvin Yondani alikasirika sana baada ya kuona kule mbele mipira inakwenda sana lakini wamalizaji wamezubaa tuu. Ndio maana kwa hasira akajaribu yeye mwenye kupiga mashuti ya mbali. Ingawa baadaye nadhani hasira zilipungua akarudi kwenye kucheza kitimu zaidi. Na kwa kweli ilikuwa inakera sana mipira mingi inafika mbele kabisa golini lakini kuna vijamaa vitatu hivi pale mbele vipo vipo tu hata kutuliza mpira haviwezi kabisa. Badala ya kufunga vinaokoa kama cross mbili hvi.
MECHI YA JANA ILIKUWA NI YA TAIFA STAAZ ILA KWA KWELI WASHAMBULIAJI WALITUANGUSHA KABISA. NASHANGAA KWA NINI KOCHA HAKUALIONA HILO MAPEMA NA KUWAPA NAFASI WENGINI AMBAO WANGEWEZA KUBADILISHA MCHEZO PALE MBELE.
 
ACHA KUPOTOSHA WEWE SASA KATIKA MAZINGIRA KAMA YALE ULITAKA KASEJA AFANYE NINI?
We kazi yake huijui?
.
Kash kash alizokuwa anakutana nazo Golikipa wa Sudan angezipata Kaseja ina maana angekula saba sasa.
Yani mtu kazi yake ni kuokoa mipira isiingie kwenye nyavu alafu unauliza angefanya nini looooh!
 
We kazi yake huijui?
.
Kash kash alizokuwa anakutana nazo Golikipa wa Sudan angezipata Kaseja ina maana angekula saba sasa.
Yani mtu kazi yake ni kuokoa mipira isiingie kwenye nyavu alafu unauliza angefanya nini looooh!
Kijana usipoteze muda wako kwa ku-assume mambo. Hayo mambo ya angekuwa yeye..... ni sawa na kujaza takataka kichwani mwako. Deal na mambo yaliyotokea uwanjani na yajayo!
 
Kijana usipoteze muda wako kwa ku-assume mambo. Hayo mambo ya angekuwa yeye..... ni sawa na kujaza takataka kichwani mwako. Deal na mambo yaliyotokea uwanjani na yajayo!
Mimi naujua mpira usidhani ni tumbotumbo mimi.
.
Jukumu namba moja la Golikipa ni kuuzuia mpira usiguse nyavu zake na jukumu la walinzi wa mwisho ni kuzuia mipira isimfikie golikipa wao.
.
Sudan haina beki ya kutisha kabisa inapitika kirahisi ila wana golikipa mzuri sana aliziba madhaifu ya walinzi wake, Kaseja alifeli kubali hilo yani alifeli sanaaa lawama zinawahusu washambuliaji na Kaseja pumbavu zao
 
Tanzania kwa sasa ina washambuliaji namba 9 chipukizo wengi sema hawapewi nafasi.. kocha yupo radhi kilazimisha beki acheze namba 9 lakini sio kuwaita hawa chipukizi.

Kelvin John

Andrew simchimba

Onesmo mayaya

Salim aye

Hawa ni vijana wazuri sana kwa kufumania nyavu na wameomyesha uwezo wa hali ya juu sana kwenye timu za vijana.

Kwanini makocha hawataki kuwamini vijana hawa.

Mbele ya goli ni akili ya striker.. na sio umbo la mtu.

Huyo Salim Ayee mwenyewe kati ya goli 16 alizofunga msimu uliopita, unaambiwa goli 14 alipokea msaada (assist) kutoka kwa mchezaji mwenzake Ditram Nchimbi! Striker aliyekuwepo kwa mkopo akitokea Azam. Huyu ana sifa zote za kuchezea timu ya Taifa iwapo atapata nafasi!

Ni mchezaji mwenye kasi na nguvu nyingi uwanjani, lakini hana bahati ya kuonekana! Mfano mzuri ni kwenye mechi ya kirafiki msimu huu kati ya Yanga na Polisi Tanzania ambako anacheza tena kwa mkopo. Alifunga goli la pili kwa umaridadi mkubwa!
 
Hivi nchi yenye watu zaidi ya milioni 50, kweli tumekosa namba 9 mmoja mwenye uwezo wa kuifungia timu yetu magoli?
 
Hata waliocheza jana sio wabaya..
Akina FEI watagusa kule Sudan
Hakuna timu imejaa usimba na Azam tupigwe tu tangu matola awe pale anaita madogo wote aliokuwa nao lipuli na Simba kocha wenu nae kijana wake chilunda anaruka ruka tu ple mbele!
 
Mi nadhani Kelvin Yondani alikasirika sana baada ya kuona kule mbele mipira inakwenda sana lakini wamalizaji wamezubaa tuu. Ndio maana kwa hasira akajaribu yeye mwenye kupiga mashuti ya mbali. Ingawa baadaye nadhani hasira zilipungua akarudi kwenye kucheza kitimu zaidi. Na kwa kweli ilikuwa inakera sana mipira mingi inafika mbele kabisa golini lakini kuna vijamaa vitatu hivi pale mbele vipo vipo tu hata kutuliza mpira haviwezi kabisa. Badala ya kufunga vinaokoa kama cross mbili hvi.
MECHI YA JANA ILIKUWA NI YA TAIFA STAAZ ILA KWA KWELI WASHAMBULIAJI WALITUANGUSHA KABISA. NASHANGAA KWA NINI KOCHA HAKUALIONA HILO MAPEMA NA KUWAPA NAFASI WENGINI AMBAO WANGEWEZA KUBADILISHA MCHEZO PALE MBELE.
Ah..huyo kocha humwambii kitu kwa wachezaji wake wa Azam!
 
Back
Top Bottom