Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Tulipoishia.... Nikiwa na malaika kwenye mji wa waliokufa duniani.

Alivyokuwa akiendelea kuongea na mimi, nilipata nguvu ya kuongea. Nikamuuliza... Je, wewe umetoka wapi na jina lako ni nani. Akajibu akisema jina langu huwezi kulitamka utalijua, maana mimi najulikana si kwa jina bali kwa nguvu mimi ndivyo nilivyo, utakavyo nilivyo. Hakika siku ile sikuelewa alikuwa anaongelea nini. Vilevile akanijibu mimi sijatokea popote mimi nilikuwepo nipo na nitakuwepo. Majibu yale yalikuwa magumu sana kwangu yalipita tu.

Akiniita David wewe nimekufunulia leo habari kuu za ulimwengu, ongea na wote wenye kujua na wenye moyo mkunjufu wataelewa na kufuata haya nitakayo kuambia leo hii.

Waambie hakuna mkuu wa dunia zaidi ya mtu mwenyewe. Mtawala wa mtu ni yeye mwenyewe. Waambie wapate kujua kuwa yeye atakaye ufalme wa mwili atapata na atakaye ufalme wa milele atapata. Umeona wale wafu wa dunia, walikuwa wakifanya mambo yao kwa faida ya mwili, hakika nakuambia mwili ni ulimwengu wa macho, katika ulimwengu huo unapitia na kujifunza mengi. Lakini mwisho utafika kwenye uhalisia wako.

Waambie, mambo haya mawili humpata mtu akiwa katika ulimwengu wa macho, yeye huzaliwa na yeye hufa. Waambie hakuna tofauti katika hilo. Anayezaliwa leo hajui utajiri, mali, na vitu vingine kama hivyo. Anapozaliwa hutoa kilio, maana ameingia kwenye sehemu ya maisha mengine.

Mtu hufa ndilo tukio jingine akipotalo. Hilo ni kielelezo cha kuonesha kuwa ulimwengu wa macho si wa kudumu bali ni wa muda. Ni kielelezo cha kufahamu kuwa yote yaliyopo kwenye ulimwengu wa macho ni yakupita. Chuma hupata kutu, kinalika na kuisha, masika huja na kuondoka, maua huonekana mazuri na kisha hunyauka, utawala na ufalme huja na kupita. Haya yote ni kielelezo cha kukukumbusha kuwa kuna jambo unatakiwa ufanye muda ni sasa.

Waambie wenye ufahamu, waambie wenye akili wapate kujua siri za ulimwengu huu. Jambo utalo waambia ni hili, kwenye ulimwengu wa mwili yapo mambo mawili, hayo mambo hayapingani bali yanafanya ukamilisho. Kuna kuzaliwa na kufa, kuna giza na mwanga, kuna kulia na kushoto, kuna juu na chini, kuna hasi na chanya. Yote haya yawe kielelezo kwao wajue kuwa nguvu za giza ndizo hizo hizo ni nguvu za mwanga.

Waambie wajue .......

Tulipoishia.... Nikiwa na malaika kwenye mji wa waliokufa duniani.

Alivyokuwa akiendelea kuongea na mimi, nilipata nguvu ya kuongea. Nikamuuliza... Je, wewe umetoka wapi na jina lako ni nani. Akajibu akisema jina langu huwezi kulitamka utalijua, maana mimi najulikana si kwa jina bali kwa nguvu mimi ndivyo nilivyo, utakavyo nilivyo. Hakika siku ile sikuelewa alikuwa anaongelea nini. Vilevile akanijibu mimi sijatokea popote mimi nilikuwepo nipo na nitakuwepo. Majibu yale yalikuwa magumu sana kwangu yalipita tu.

Akiniita David wewe nimekufunulia leo habari kuu za ulimwengu, ongea na wote wenye kujua na wenye moyo mkunjufu wataelewa na kufuata haya nitakayo kuambia leo hii.

Waambie hakuna mkuu wa dunia zaidi ya mtu mwenyewe. Mtawala wa mtu ni yeye mwenyewe. Waambie wapate kujua kuwa yeye atakaye ufalme wa mwili atapata na atakaye ufalme wa milele atapata. Umeona wale wafu wa dunia, walikuwa wakifanya mambo yao kwa faida ya mwili, hakika nakuambia mwili ni ulimwengu wa macho, katika ulimwengu huo unapitia na kujifunza mengi. Lakini mwisho utafika kwenye uhalisia wako.

Waambie, mambo haya mawili humpata mtu akiwa katika ulimwengu wa macho, yeye huzaliwa na yeye hufa. Waambie hakuna tofauti katika hilo. Anayezaliwa leo hajui utajiri, mali, na vitu vingine kama hivyo. Anapozaliwa hutoa kilio, maana ameingia kwenye sehemu ya maisha mengine.

Mtu hufa ndilo tukio jingine akipotalo. Hilo ni kielelezo cha kuonesha kuwa ulimwengu wa macho si wa kudumu bali ni wa muda. Ni kielelezo cha kufahamu kuwa yote yaliyopo kwenye ulimwengu wa macho ni yakupita. Chuma hupata kutu, kinalika na kuisha, masika huja na kuondoka, maua huonekana mazuri na kisha hunyauka, utawala na ufalme huja na kupita. Haya yote ni kielelezo cha kukukumbusha kuwa kuna jambo unatakiwa ufanye muda ni sasa.

Waambie wenye ufahamu, waambie wenye akili wapate kujua siri za ulimwengu huu. Jambo utalo waambia ni hili, kwenye ulimwengu wa mwili yapo mambo mawili, hayo mambo hayapingani bali yanafanya ukamilisho. Kuna kuzaliwa na kufa, kuna giza na mwanga, kuna kulia na kushoto, kuna juu na chini, kuna hasi na chanya. Yote haya yawe kielelezo kwao wajue kuwa nguvu za giza ndizo hizo hizo ni nguvu za mwanga.

Waambie wajue .......
We jamaa ni liongo sana. Kwamba malaika akakwambia kuwa kuna hasi na chanya! Akugusia intergration na differentiation?
 
Siwezi kuyaandika yote.
Imenishangaza sana kwa jinsi ulivyoacha kutoa ujumbe uliopewa na “malaika “ kwa wanadamu! Nini kimekutokea hujaendelea tena tangu May 2022?! Hii inasema mengi kuhusu authenticity ya claims zako. Jihadhari na New Age Movement na mambo yake.
 
Mkuu endekea na hii kitu, ikiwezekana andika pembeni halfu post yote.

Halafu sasa ndio uje tujadili. Hii kupost nusunusu ndio inaleta mkanganyiko na kuanza kubiashana bila msingi wowote.

Tema nondo
 
Mwaka 2017 nilienda Rwanda na jamaa angu flan hivi!
Wakati tunarudi tukiwa njiani nyakati za usiku tukapita sehem tukapaki kwa muda... Lile eneo kwakipindi chote tulipopumzika akili inaniambia kuwa nilishawah kupiga hapo miaka kadhaa nyuma.
 
Aliendelea kuniambia,

Imani ni hisia, imani ipo moyoni. Basi sasa imani pasipo matakwa, imani pasipo akili haiwezi kufanya chochote.

Vivyo hivyo matakwa, akili pasipo imani haiviwezi kufanya chochote. Basi sasa mwenye imani lazima awe na akili. Na mwenye akili lazima awe na imani.

Kisha malaika akanichukua na kunipeleka sehemu nyingine. Akanionesha eneo kubwa lililojaa viumbe waliofanana na wanadamu. Miiliyao siyo ngozi kama za kwetu, ngozi zao mithili ya chuma. Malaika akaniambia, umeona wale!? Nikasema ndio nimewaona. Hao ni watu kama wewe wapo katika ulimwengu wa mwili mwingine. Wamevaa miili ya chuma maana ulimwengu unaoishi wewe ni tofauti na huu. Hapo wapo katika makutano makuu kwa imani yao wanamwabudu Mungu wao.

Kisha nikamuuliza je, hapo ni wapi!? Sisi tunaweza kufika hapo!?
Akanijibu na kusema hapo ni ulimwengu wa mwili mwingine ili uweze kwenda katika ulimwengu huo wa mwili ni lazima uondoke katika ulimwengu huu wa mwili wako na utaweza kwenda huko. Akaniambia katika ulimwengu wenu wa mwili mnaweza kusafiri kwenda sehemu yoyote ya ulimwengu wenu. Pale mtakapopata na maarifa na kuwa kitu kimoja mtaweza kusafiri katika ulimwengu wote wa mwili. Umesoma kuhusu sayari, umesoma kuhusu nyota ndivyo hivyo mtakuwa na uwezo wa kusafiri kutoka sayari nyingine na kwenda nyingine. Lakini hao unaowaona hawapo katika sehemu ya ulimwengu wenu wa mwili.

Hekima hii mwenye ufahamu aifahamu na mwenye kujua aijue. Ulimwengu wenu upo kwaajili yenu. Ndio maana mnaweza kuuona kwa macho yenu na vifaa vyenu. Lakini ulimwengu mwingine wa mwili hauwezi kuuona kwa macho yenu na vifaa vyenu. Hisia na matakwa yako yatakufanya uweze kuuona ulimwengu mwingine na siyo kuishi ukiwa kwenye mwili huu wa sasa.

Ulimwengu wa mwili upo mwingi tu, kila sehemu yao wanaishi kwa namna yao. Ukiwa katika ulimwengu wa roho utaweza kuuona bali hutaweza kuishi mpaka utakapovishwa mwili wa ulimwengu huo.

Mwenye ufahamu atambue haya....
Je, hii ni simulizi ya kutunga (fiction), au ni halisi?
Uliambiwa kweli?
 
ulijaribu kucheku maleria mkuu. maana kuna kitu kinaitwaga HALLUCINATIONS, hii kitu iogope. unaweza ukaona unapiga picha na yesu
 
Nadhani ulipofika darasani hiyo mida mibaya ukachukuliwa tena na usingizi mzito kuliko wa bwenini
 
Mwaka 2017 nilienda Rwanda na jamaa angu flan hivi!
Wakati tunarudi tukiwa njiani nyakati za usiku tukapita sehem tukapaki kwa muda... Lile eneo kwakipindi chote tulipopumzika akili inaniambia kuwa nilishawah kupiga hapo miaka kadhaa nyuma.
Kupiga nn mruzi au
 
Back
Top Bottom