Melki Wamatukio
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 6,156
- 10,974
Tulipoishia.... Nikiwa na malaika kwenye mji wa waliokufa duniani.
Alivyokuwa akiendelea kuongea na mimi, nilipata nguvu ya kuongea. Nikamuuliza... Je, wewe umetoka wapi na jina lako ni nani. Akajibu akisema jina langu huwezi kulitamka utalijua, maana mimi najulikana si kwa jina bali kwa nguvu mimi ndivyo nilivyo, utakavyo nilivyo. Hakika siku ile sikuelewa alikuwa anaongelea nini. Vilevile akanijibu mimi sijatokea popote mimi nilikuwepo nipo na nitakuwepo. Majibu yale yalikuwa magumu sana kwangu yalipita tu.
Akiniita David wewe nimekufunulia leo habari kuu za ulimwengu, ongea na wote wenye kujua na wenye moyo mkunjufu wataelewa na kufuata haya nitakayo kuambia leo hii.
Waambie hakuna mkuu wa dunia zaidi ya mtu mwenyewe. Mtawala wa mtu ni yeye mwenyewe. Waambie wapate kujua kuwa yeye atakaye ufalme wa mwili atapata na atakaye ufalme wa milele atapata. Umeona wale wafu wa dunia, walikuwa wakifanya mambo yao kwa faida ya mwili, hakika nakuambia mwili ni ulimwengu wa macho, katika ulimwengu huo unapitia na kujifunza mengi. Lakini mwisho utafika kwenye uhalisia wako.
Waambie, mambo haya mawili humpata mtu akiwa katika ulimwengu wa macho, yeye huzaliwa na yeye hufa. Waambie hakuna tofauti katika hilo. Anayezaliwa leo hajui utajiri, mali, na vitu vingine kama hivyo. Anapozaliwa hutoa kilio, maana ameingia kwenye sehemu ya maisha mengine.
Mtu hufa ndilo tukio jingine akipotalo. Hilo ni kielelezo cha kuonesha kuwa ulimwengu wa macho si wa kudumu bali ni wa muda. Ni kielelezo cha kufahamu kuwa yote yaliyopo kwenye ulimwengu wa macho ni yakupita. Chuma hupata kutu, kinalika na kuisha, masika huja na kuondoka, maua huonekana mazuri na kisha hunyauka, utawala na ufalme huja na kupita. Haya yote ni kielelezo cha kukukumbusha kuwa kuna jambo unatakiwa ufanye muda ni sasa.
Waambie wenye ufahamu, waambie wenye akili wapate kujua siri za ulimwengu huu. Jambo utalo waambia ni hili, kwenye ulimwengu wa mwili yapo mambo mawili, hayo mambo hayapingani bali yanafanya ukamilisho. Kuna kuzaliwa na kufa, kuna giza na mwanga, kuna kulia na kushoto, kuna juu na chini, kuna hasi na chanya. Yote haya yawe kielelezo kwao wajue kuwa nguvu za giza ndizo hizo hizo ni nguvu za mwanga.
Waambie wajue .......
We jamaa ni liongo sana. Kwamba malaika akakwambia kuwa kuna hasi na chanya! Akugusia intergration na differentiation?Tulipoishia.... Nikiwa na malaika kwenye mji wa waliokufa duniani.
Alivyokuwa akiendelea kuongea na mimi, nilipata nguvu ya kuongea. Nikamuuliza... Je, wewe umetoka wapi na jina lako ni nani. Akajibu akisema jina langu huwezi kulitamka utalijua, maana mimi najulikana si kwa jina bali kwa nguvu mimi ndivyo nilivyo, utakavyo nilivyo. Hakika siku ile sikuelewa alikuwa anaongelea nini. Vilevile akanijibu mimi sijatokea popote mimi nilikuwepo nipo na nitakuwepo. Majibu yale yalikuwa magumu sana kwangu yalipita tu.
Akiniita David wewe nimekufunulia leo habari kuu za ulimwengu, ongea na wote wenye kujua na wenye moyo mkunjufu wataelewa na kufuata haya nitakayo kuambia leo hii.
Waambie hakuna mkuu wa dunia zaidi ya mtu mwenyewe. Mtawala wa mtu ni yeye mwenyewe. Waambie wapate kujua kuwa yeye atakaye ufalme wa mwili atapata na atakaye ufalme wa milele atapata. Umeona wale wafu wa dunia, walikuwa wakifanya mambo yao kwa faida ya mwili, hakika nakuambia mwili ni ulimwengu wa macho, katika ulimwengu huo unapitia na kujifunza mengi. Lakini mwisho utafika kwenye uhalisia wako.
Waambie, mambo haya mawili humpata mtu akiwa katika ulimwengu wa macho, yeye huzaliwa na yeye hufa. Waambie hakuna tofauti katika hilo. Anayezaliwa leo hajui utajiri, mali, na vitu vingine kama hivyo. Anapozaliwa hutoa kilio, maana ameingia kwenye sehemu ya maisha mengine.
Mtu hufa ndilo tukio jingine akipotalo. Hilo ni kielelezo cha kuonesha kuwa ulimwengu wa macho si wa kudumu bali ni wa muda. Ni kielelezo cha kufahamu kuwa yote yaliyopo kwenye ulimwengu wa macho ni yakupita. Chuma hupata kutu, kinalika na kuisha, masika huja na kuondoka, maua huonekana mazuri na kisha hunyauka, utawala na ufalme huja na kupita. Haya yote ni kielelezo cha kukukumbusha kuwa kuna jambo unatakiwa ufanye muda ni sasa.
Waambie wenye ufahamu, waambie wenye akili wapate kujua siri za ulimwengu huu. Jambo utalo waambia ni hili, kwenye ulimwengu wa mwili yapo mambo mawili, hayo mambo hayapingani bali yanafanya ukamilisho. Kuna kuzaliwa na kufa, kuna giza na mwanga, kuna kulia na kushoto, kuna juu na chini, kuna hasi na chanya. Yote haya yawe kielelezo kwao wajue kuwa nguvu za giza ndizo hizo hizo ni nguvu za mwanga.
Waambie wajue .......