Kimwakaleli
JF-Expert Member
- Apr 16, 2018
- 7,755
- 11,737
Ukijidai nayo inakupoteaFamilia, nenda unapokwenda ila jua utakuwa na familia yako siku zote. Wengi wetu familia zetu ndo rafiki zetu, tumepoteza na tunaendelea kupoteza watu wengi wa karibu lakini familia haipotei.
Hayo ni matatizo ya baadhi ya familia, lakini familia nyingi duniani ndo mahali pekee kama sanctuary.Ukijidai nayo inakupotea
Hata mimi nina hiyo tabia, baada ya mda fulani naangalia phonebook na facebook, kuna watu kiukweli wanakuwa sio.sehemu ya maisha yako tena, hakuna haja ya kutunza namba zao.Jana i was revising my phone book. Nimepunguza contacts from 600 to 175
Hapo ndio kipimo Cha utu kinaposhindwa!TAtizo hapo wewe unatembelea makalio mwenzio anatembele miguu na aliongopa ungemuuliza siku hizi uko wapi mwenzangu.
Pole sana,Maisha ni safari yenye konakona kama mto Nile!Hii ilinitokea kwa rafiki yangu mmoja ambaye niliamini tutakua close mpaka tukiwa vibibi. Huu urafiki ulivyoisha (kwa sababu ya mgogoro wa kifedha, tulianzisha biashara pamoja) iliniuma kuliko breakup ya mwanaume yoyote. Alihama nchi na hivi karibuni niliona ameview status yangu whatsapp, sijui ilikua kimakosa au alidhamiria. Huwa namkumbuka sana, na kila nikipiga hatua mpya kwenye kazi au maisha nafikiria angekuwepo tungefurahiaje pamoja hilo tukio, nabaki kuumia tu!
Neno "gari" kwenye andiko lako umeliandika mara 80...., ndo kusema kwako gari ni kitu gani atii🥲rafiki wa mtaani, shuleni, chuo, n.k. mlikuwa washikaji sanaaaa kujuliana hali kila siku, muda mwingi mpo wote, kushare siri, n.k. lakini leo mmebaki kuchunguliana view stutus,
Halafu hata mkikutana ni salam za dakika 2 tu, baada ya hapo kila mtu anajidai yupo bize, mnabadilishana za kuchunguliana status,
Nje ya marafiki tunaoishia kuangaliana status nina visa hivi
Kuna siku flani nilikuwa napoteza muda naendesha gari mtaani nilikuwa nimerudi kusalimia mkoani nilikokulia, nikamuona rafiki yangu tuliwahi kuwa mabesti sana primary, vile nilivyomona na yeye aliniona ila akazuga kama hajaniona (niligungua badae) , nikaona niende kupaki gari sehemu ya mbele kidofo maana mazingira hayakuruhusu, nilivyopaki nimeshuka namuona mtu kaongeza mwendo wa kutembea kaingia njia nyingine, nikawasha gari fasta niende mtaa wa barabara atayotokea, mara hii macho yaligongana hakuweza kunizuia, tulisalimiana kidogo ila akaniambia ana haraka, namba aliyonipa haipatikani, sijui sababu lakini labda pengine ni gepu la maendeleo niliambiwa hali yake si nzuri
Niliwahi kuwa na rafiki tuliekuwa mbali kwa mwaka moja tu, lakini tunatazamiana status na kupeana hi mara kadhaa japo mara chache, alikuwa ameenda mafunzo idara ya ulinzi akabahatika kupata kazi, aliposti video anavishwa cheo kwenye bega, nilimpa hongera ila hakujibu (Blue tick), mara ya pili niliwahi kumpa heri ya mwaka mpya ila hakujibu, damn ! baada ya mwaka na mimi nilibahatika kwenye shughuli zangu, napenda sana magari nilinunua nikajipost status nikiwa safarini ndipo aliponijulia hali "za siku kaka naona mambo yamejipa" nilibaki na maswali mengi
Bond inayotengenezwa nje ya damu ni ngumu kuitunzaUrafiki ni bond inayotengenezwa kwa sababu flani au moment flani.
urafiki sio kufahamiana, urafiki ni kujuana.
Kwa hiyo kuwa katika shule, ofisi au mazingira yoyote ya kuwafanya mfahamiane, haimaanishi ni marafiki.
Na wengine mnaiva kwa season moja ila hali za kiuchumi au tu kukutana na watu wapya au ukuaji vinatufanya tutofautiane. Kwa walio na bond halisi, hili suala haliondoi urafiki ila kwa wengi. Urafiki hupotea