Khantwe
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 59,415
- 119,473
Habari za wakati huu,
Rejea swali hilo hapo juu...katika maisha ya ukuaji, masomo, utafutaji huwa tunajikuta tunakutana na watu wengi... wengine wanabaki kuwa tu watu tunaofahamiana nao na wengine wanakuwa marafiki tena wengine huwa tunashibana kiasi cha kuwa kama ndugu.
Nakumbuka shule ya msingi nilikuwa na rafiki yangu mmoja anaitwa A ..ni hulka yangu kuwa na rafiki mmoja tu wakizidi sana wawili. Of course wanaweza kuwa wapo na wengine ila wa karibu huwa ni mmoja.
Huyu tumekua wote hadi chuo lakini baada ya hapo kila mtu alipoingia kwenye kutafuta maisha tukajikuta tunakuwa mbali, mawasiliano yakapungua kama sio kukatika kabisa.
Kila mtu ana namba ya mwenzie ila tuna miaka zaidi ya mitatu hatujawasiliana, hata tukipigiana simu hatuna stori.
Huo ni mfano mmoja tu ila wapo niliokutana baada ya hapo , tulikuwa karibu sana ila sasa hivi tumekuwa total strangers.
Nilichogundua ili watu muwe na muendelee kuwamarafiki lazima kuna vitu muwe mnafanana, mazingira yaliyowakutanisha yakibadilika tu kila kitu kinabadilika.
Mfano mlikutana mkiwa single mmoja akiwa na familia urafiki kwa vyovyote utakufa tu.
Mlikutana hohehahe mmoja akifanikiwa urafiki utakufa au unabadilika kutoka urafiki hadi uchawa...labda yule aliyefanikiwa awe na moyo wa kumuinua mwenzake.
Mkikutana hamna ajira mmoja akipata kazi anakutana na marafiki wapya.
Au nyie wakuu mnaonaje? Niwatakie jioni njema
Rejea swali hilo hapo juu...katika maisha ya ukuaji, masomo, utafutaji huwa tunajikuta tunakutana na watu wengi... wengine wanabaki kuwa tu watu tunaofahamiana nao na wengine wanakuwa marafiki tena wengine huwa tunashibana kiasi cha kuwa kama ndugu.
Nakumbuka shule ya msingi nilikuwa na rafiki yangu mmoja anaitwa A ..ni hulka yangu kuwa na rafiki mmoja tu wakizidi sana wawili. Of course wanaweza kuwa wapo na wengine ila wa karibu huwa ni mmoja.
Huyu tumekua wote hadi chuo lakini baada ya hapo kila mtu alipoingia kwenye kutafuta maisha tukajikuta tunakuwa mbali, mawasiliano yakapungua kama sio kukatika kabisa.
Kila mtu ana namba ya mwenzie ila tuna miaka zaidi ya mitatu hatujawasiliana, hata tukipigiana simu hatuna stori.
Huo ni mfano mmoja tu ila wapo niliokutana baada ya hapo , tulikuwa karibu sana ila sasa hivi tumekuwa total strangers.
Nilichogundua ili watu muwe na muendelee kuwamarafiki lazima kuna vitu muwe mnafanana, mazingira yaliyowakutanisha yakibadilika tu kila kitu kinabadilika.
Mfano mlikutana mkiwa single mmoja akiwa na familia urafiki kwa vyovyote utakufa tu.
Mlikutana hohehahe mmoja akifanikiwa urafiki utakufa au unabadilika kutoka urafiki hadi uchawa...labda yule aliyefanikiwa awe na moyo wa kumuinua mwenzake.
Mkikutana hamna ajira mmoja akipata kazi anakutana na marafiki wapya.
Au nyie wakuu mnaonaje? Niwatakie jioni njema