Marekani: Aliyeua Watoto 19 alikuwa akizomewa na wenzake kwa kuwa masikini na kuvaa nguo mbaya

Marekani: Aliyeua Watoto 19 alikuwa akizomewa na wenzake kwa kuwa masikini na kuvaa nguo mbaya

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Capture1.JPG

Capture.JPG
Kijana Salvador Ramos ambaye amehusika na mauaji ya watoto 19 na watu wazima wawili jana Mei 24, 2022 katika Jimbo la Texas, Marekani, imebainika alikuwa akizomewa na kuchekwa na wanafunzi wenzake kutokana na hali ya umasikini wake na familia yake.

Rafiki wa karibu wa kijana huyo amesema Salvador pia alichekwa kwa kutovaa nguo nzuri, kutokana na hali hiyo alianza kukwepa kuingia darasani. Siku alipokuwa akitimiza umri wa miaka 18, alinunua bunduki mbili siku chache kabla ya tukio la mauaji.

Alipiga picha silaha alizonunua na kuzituma kwa rafiki yake licha ya kutomwambia sababu ya kuzinunua. Jirani wa kijana Ramos amenukuliwa akisema: “Alimjeruhi bibi yake kwa risasi baada ya majibizano, akaondoka na kwenda kufanya mauaji hayo.”

Inaelezwa kuwa tukio hilo limetokea siku moja baada ya wenzake aliokuwa akisoma nao kuhitimu masomo.

Capture2.JPG

Source: Daily Mail
 
Dogo alisubiri afike miaka 18 awe na ruhusu ya kumiliki chuma alipize kisasi vizuri sana

Niliangalia picha Moja ya kihindi jina nimesahau nzuri sana inamulezea kijana mmoja aliku polisi sasa kuna shule palikuwa panatokea mauaji sana watu wanauliwq then panaachwa kiji mdoli Cha kike kimona

Kisa kilikuwa ivi kulikuwa na dogo alizaliwa na ulemavu wa ngozi yaani ana ngozi ya kizee kama vile grand p na baba Ake yule dogo alikuwa mtu wa miujiza ndo wanajipatia pesa (mazingaombwe) na pia alikuwa na huo ulemavu sema anavaa nguo za mikono mirefu mpaka gloves za mikono yaaani ngozi ya kizee kabisa

Yule dogo alipokuwa alipelekwa shule siku ya kwanza kwenda alipoingia darasani tu ili apewe kiti cha kukaa kila mtu hataki akae nae kutokana na alivyo basi wanamkwepa asikae basi kuna dogo wa kike alimuita akakaa nae wakawa kama wachumb ila akitaka kukaa na watu mda wa break wanamkimbia yule demu ndo anamchukua Wana ongea
Yule dogo akirudi home analia anawaeleza wazazi wake anavyotengwa hana raha

Siku moja alivaa miwani akaenda shule akiwa kama mtu mwenye furaha dah kumbe wamemchora ubaoni wanamdhihaki wanamcheka alipoingia walikuwa kama wanamsukuma akitaka kufuta picha yake pale ubaoni wakawa kama wanashambulia mpaka wakamvua nguo

Akarudi kwao akasema nitalipiza na shule sitorudi Tena .Yule demu alipoona jamaa hajaja shule akaenda kwao mbaya zaidi jamaa akaona hata huyu ananichora ni wale wale akaanza nae anauwa na nyundo then anaacha kimdoli na kibox kama cha zawadi ya happy birthday

Movie kali sana humo ndani kuna katoto ni kiziwi pia
 
Kijana Salvador Ramos ambaye amehusika na mauaji ya watoto 19 na watu wazima wawili jana Mei 24, 2022 katika Jimbo la Texas, Marekani, imebainika alikuwa akizomewa na kuchekwa na wanafunzi wenzake kutokana na hali ya umasikini wake na familia yake.

Rafiki wa karibu wa kijana huyo amesema Salvador pia alichekwa kwa kutovaa nguo nzuri, kutokana na hali hiyo alianza kukwepa kuingia darasani. Siku alipokuwa akitimiza umri wa miaka 18, alinunua bunduki mbili siku chache kabla ya tukio la mauaji.

Alipiga picha silaha alizonunua na kuzituma kwa rafiki yake licha ya kutomwambia sababu ya kuzinunua. Jirani wa kijana Ramos amenukuliwa akisema: “Alimjeruhi bibi yake kwa risasi baada ya majibizano, akaondoka na kwenda kufanya mauaji hayo.”

Inaelezwa kuwa tukio hilo limetokea siku moja baada ya wenzake aliokuwa akisoma nao kuhitimu masomo.

Source: Daily Mail


Wasitafute mchawi. Wachawi ni wao wenyewe, tangu lini mtoto anauziwa bunduki kama njugu.
 
Acheni utani maskini wa Marekani ananunua bunduki tena mtoto!.. Sasa huku tunaoombwa vocha tu hatuna sisi ni nani..?[emoji1787]

Pole kwa wafiwa na marehemu.
Mbona silaha ni jambo la kawaida sana hata hapa TZ wakiruhusu kila Mtu kumiliki?

Sheria tu za USA ndizo zifanyazo yeyote aruhusiwe kumiliki silaha hata kama kipato chake cha kawaida kimaisha.
 
Back
Top Bottom