Uchaguzi 2020 Marekani: Kuanzia leo, tunaweka vizuizi kwa waliohusika na kuvuruga Uchaguzi nchini Tanzania

Hawa ndiyo ma GT wa JF ingawa JF kwa nature yake haiwatambui
 
Nawe umezidi upuuzi. Inaonesha elimu yako matatizo tu
 
Mmi nalichukia lisisiemu na vyote vilivyomo ila marekani imepoteza moral authority kulizungumzia hili hususani kwa huu mwaka
Mimi naona ndo wamejenga moral authority kwa kuonesha kuwa taasisi zao zipo huru, hata rais aliyepo madarakani hawezi ingilia. Sheria kwao inayo nguvu tofauti na Tz ambako Rais ndo katiba.
Trump angekuwa anaongoza nchi kama Tz et-al, angekaa madarakani kwa muda autakao yeye.
 
Hawawezi hawa ubabe wa ndani tu. Watatuonea sisi tuliopo ndani.
 
Kwa hiyo CEO wa Twitter yupo juu ya katiba,manake kufanya hivyo ni kumnyima Trump uhuru wa kujieleza na siku zote US wanakuaga wakali kama akitokea mtu akaubana uhuru wa kujieleza.

Sasa kwa nini hawa kumwambia kwamba hicho alicho kifanya ni kosa.
Tweeter siyo US.
 
Wauweni basi ili mpate amani, kwani mshaua wangapi.

Siku zote ninyi ni malaika, hamjawahi kuwa na tatizo.
 
Nikiziangalia sura zilizojazana NEC na kwa msajili wa vyama vya siasa kwa hakika wamejaa wazalendo watupu na wengi wao hata huko Marekani hawakujui...
Hujui lolote kuhusu sanctions bali unajiropokea tu!

Huwa wanawapiga ban kwanza viongozi walio nufaika na huo uchaguzi HARAMU na wakuu wao wa vyombo vya dola!

Ni aibu sana kwa Tanzania nchi iliyokuwa kioo cha demokrasia Afrika miaka 10 tu iliyopita.
 
Ndo hivyo hakuna Cha kucharuka, may be waliocharuka wako karibu na keki ya taifa,itoshe sema tz ni yetu wote, hakuna haja ya kujitoa hufaham kwamba pompeo anaongea asichokua na huakika nacho by the way ,hawezi angaika na hizo tweeter zenu,lazima kujiuliza na EA ikiwemo tz tunakwama wapi,tatizo nini, kwamba madaraka yamekua au ubinafsi, yamekua juu kuliko misingi ya utu, haki,cheki Uganda mgombea anakua under military,Kama vile Mseveni ndo kaumba, nchi ya Uganda tuna viongozi wa ajabu Afrika haijawai tokea,
 
Marekani waache kuingilia internal affairs za nchi nyingine wapambane na mambo yao.
 
Nikiziangalia sura zilizojazana NEC na kwa msajili wa vyama vya siasa kwa hakika wamejaa wazalendo watupu na wengi wao hata huko Marekani hawakujui...
Kwanza kuishi tu ukiwa umepigwa marufuku kutembelea au kutengwa na sehemu fulani ya dunia ni TESO LA KISAIKOLOJIA hata kama hukuwa na mpango wa kwenda huko.

Pili mingi ni Mijizi na pesa zao huwa inaficha huko, kwahiyo hilo ni pigo.

Bashite kapora prsa kibao lakini furaha anaitafuta kwa tochi, anazidiwa hata na anayekula miguu ya kuku kwa pesa ya halali.
 
Safi sana, Jaji Mitungi na Mahera
Hahaha hao hawana pesa ya kwenda Marekani hata wasingefungiwa sawa tu.

Vipi ma-DC wao wanafungiwa, vipi waliofukuzwa adhabu wanaambatana nayo au inakwisha wakitoka madarakani?!

Na vipi Magufuli, Samia, na Majaliwa wanahusika au wao wanaachwa kwa kigezo walikuwa wagombea?!
 
Ngoja tuwaangalie wakati wa uchaguzi wa October 2020 Mwenyekiti na wajumbe wa NEC Tume ya Uchaguzi Tanzania na Mkurugenzi wa NEC Tume ya Uchaguzi ambaye ni Mtendaji Mkuu na Katibu pia wa Tume .

Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi

Na. Jina Wadhifa


1. Mhe. Jaji Rufaa (Mst) Semistocles Kaijage, Mwenyekiti

2. Mhe. Jaji Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk, Makamu Mweyekiti

3. Mhe. Jaji (Mst.) Mary H.C.S Longway, Mjumbe

4. Mhe. Asina A. Omari, Mjumbe

5. Mhe. Jaji (Mst) Thomas Mihayo, Mjumbe

6. Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri, Mjumbe



Wajumbe wa Tume hukaa Madarakani kwa kipindi cha miaka mitano tangu kuteuliwa kwao, lakini Rais anaweza kuwateua tena kwa kipindi kingine kadri atakavyoona inafaa.

Katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume husaidiwa na Sekretarieti inayoongozwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye ndiye Mtendaji Mkuu na Katibu wa Tume. Kwa sasa Mkurugenzi wa Uchaguzi ni Dkt. Wilson Mahera Charles.

Source : NEC Website
Source : EISA Tanzania: National Electoral commission
 
There are key principles of democracy which apply everywhere regardless of the context - time and space.
 
Sio mfano tu, ni mfano wa uongo,kwa sababu umekariri vitu kama kasuku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…