Maria Sarungi apeleka ICC nyaraka muhimu za ukiukwaji wa Haki za Binadamu Tanzania wakati wa Uchaguzi Mkuu

Maria Sarungi apeleka ICC nyaraka muhimu za ukiukwaji wa Haki za Binadamu Tanzania wakati wa Uchaguzi Mkuu

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Hatimaye mwandishi wa habari na mwanaharakati huru wa Tanzania Maria Sarungi amethibitisha rasmi leo kupeleka ndani ya ICC nyaraka muhimu za ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa uchaguzi mkuu.

Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter amesema kuwa "Namshukuru Mungu kuwa hatimaye nimefanikiwa kupeleka nyaraka muhimu ICC zinazohusu ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa uchaguzi mkuu, nawashukuru pia wote tulioshirikiana"

Miongoni mwa nyaraka hizo zipo video, picha za mauaji, kauli za vitisho kutoka kwa watawala dhidi ya upinzani na video zinazoonesha polisi wakipiga raia.

Mtuhumiwa namba moja kwenye nyaraka hizo ni Rais John Pombe Magufuli. Aidha wapo pia IGP, DC Lengai Ole Sabaya, RC wa Mbeya Albert Chalamila na baadhi ya watendaji wakuu wengine wa serikali ya Tanzania na jeshi la polisi.

Kwenye Mtandao wa Twitter, Maria kaandika hivi:

Thank God! Alhamdulillah! I have used my skills, training and ability as a journalist to fulfill my duty and submitted to @IntlCrimCourt evidence and facts on Crimes against Humanity in #Tanzania - many thanks to everyone Nawashukuru nyote -

Leo nimekamilisha kazi Mungu atulinde!

1604924425856.png
 
Asante! Namshukuru Mzee Sarungi kwa kutupatia damu ya Kizungu, ni damu zenye akili na Jasiri itatusaidia kuliokoa Taifa hili.

Hata damu ya Kizungu iliyoko mwilini mwa Lissu baada ya kuwekewa damu ya kitasha huko Ubelgiji hospitali, imeongeza ujasiri wake na akili mara dufu, ndiyo maana vilaza wa Lumumba wanamshindwa kwenye kila move yao!

Vijana, mnaoenda huko nje masomoni, oeni wazungu mtuchanganyie damu tupate vizazi vya magenius na majasiri, viiokoe nchi hii kutoka kwa Interahamwe!
 
Hakika tumepata "washindi" (victors) na timu inazidi kuongezeka wanaharakati kuhakikisha ushindi katika Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu hatimaye upatikane pamoja ya kuwa waTanzania wengi wameamua kujisaliti na kutelekeza agano, kwa kujiunga na viongozi matapeli wa dini kuombea kwa maombi yawepo maisha mazuri baada ya uchaguzi.

Wakati dalili hizo maisha mazuri zinazidi kutoweka chini ya utawala wa CCM Mpya kwani kuisoma namba ktk kila kitu kutaongezeka bila kujali itikadi yako kwani wakimalizana na sisi wataanza kutafutana 'uchawi' baina yao ndani ya CCM hapo ndipo labda waTanzania watazinduka kutoka ktk njozi za kusadikika kuwa mambo yatakuwa murua chini ya awamu ya 5 inayodai imepewa ridhaa ya mitano mingine na wapiga kura 12.5 milioni uchaguzi wa 2020.
 
Kwani mahakama za ndani haziwezi kushughulikia hayo mpaka muende huko ICC?

Maana mpaka kesi ipelekwe huko maana yake ni mahakama za ndani kukosa uwezo wa kuendesha hayo mashitaka mfano Sudan(Darfur), DRC.
 
Uhuni tu na kujimwambafai kwa huyu dada. Huo upupu hauna vigezo vya kupokelewa kwenye ICC . Propaganda tu ; hela ya mabeberu siyo lelemama.
Tumetunza siti tu
 
Hakika tumepata "washindi" (victors) na timu inazidi kuongezeka wanaharakati kuhakikisha ushindi katika Uhuru, Haki na Maendeleo ya Watu hatimaye upatikane pamoja ya kuwa waTanzania wengi wameamua kujisaliti na kutelekeza agano kwa kuombea yawepo maisha mazuri baada ya uchaguzi...
#NIYEYE
 
Back
Top Bottom