Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Mjumbe wa Baraza Kuu UWT Taifa, Mariam Sagini amewataka vijana hasa wa kike kutengeneza historia nzuri maishani kwa kujaza nafasi za mbalimbali za uongozi hasa kadri zinavyojitokeza.
Akizungumza na vijana kwenye Hafla ya Ufungaji wa Kambi la Umoja wa Vijana mkoani Katavi iliyofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wanawake ya Mpanda, Mariam amesema kuwa Jumuiya ya UWT ipo kazini chini ha Mwenyekiti Merry Chatanda kuhakikisha inamsaidia mtoto wa kike katika nafasi mbalimbali za uongozi.
"Wanawake mkajaze nafasi kama sisi mama zenu tupo kazini vijana mnashindwaje?, usiende kusomwa kijana ambaye siku ukifa unaenda kusumbua padri, mchungaji au Sheikh yaani wanasoma historia ya marehemu kwamba Marehemu alizaliwa Akafa. Tengeneza historia ambayo ulikuwa nani? labda Katibu, Hamasa au Mwenyekiti hata wasikilizaji wanalia na kukuombea.
Ndivyo tulivyo andaliwa sisi na sisi tunawaandaa hivyo na tunategemea na nyie mtaandaa wadogo zeu kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi," amesema Mbaraza Mariam.
Akizungumza na vijana kwenye Hafla ya Ufungaji wa Kambi la Umoja wa Vijana mkoani Katavi iliyofanyika katika Shule ya Sekondari ya Wanawake ya Mpanda, Mariam amesema kuwa Jumuiya ya UWT ipo kazini chini ha Mwenyekiti Merry Chatanda kuhakikisha inamsaidia mtoto wa kike katika nafasi mbalimbali za uongozi.
Ndivyo tulivyo andaliwa sisi na sisi tunawaandaa hivyo na tunategemea na nyie mtaandaa wadogo zeu kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi," amesema Mbaraza Mariam.