Marioo afunguliwa kesi ya Madai ya Tsh. Milioni 550 kwa kukiuka Mkataba wa Tamasha

Marioo afunguliwa kesi ya Madai ya Tsh. Milioni 550 kwa kukiuka Mkataba wa Tamasha

Kapokea hela alafu katokea kwa tamasha amechelewa na kalewa. Kaanza kuimba eti toto bad in the building nakuwaambia watu eti ana demu mzuri. Watu wamefanya fujo mfululu mixer beto zilitembea sana. Imebidi toto bad akimbilie sentro pale chugani ambako amehifadhiwa mpaka mda huu Raia lombelombe wanataka kuruka naye kimasai. Wamesema mpaka atage yai hapo chugani.
Analeta tambo za kifoo chugastan, dah ila mashabiki wanaingia na beto za nn aisee
 
Hii ni kesi au mavi. Kwamba wao walitegemea wampe milioni 15 ili wao wavune faida ya milioni 550? Kwa show ipi ya mavi kama.hio ya kuwaimbia hao mamiss uchwara
Hauna akili unajua mkataba wewe,
Mkataba ni makubaliano basi.
Makubaliano kama yalifanyika basi hapo wewe una kesi na utalipa tu.
Mfano nimeandaa material ya gharama ya mil300 nimekukabidhi fundi unijengee nyumba
Na malipo yako labda ni mil20
Umesababisha hasara ya material yote na kazi haijafanyika
Mimi nitafungua kesi ya kudai milioni 500 na mahakama ikijiridhisha kwa hoja zangu utalipa




Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Hilo neno ni kama $300k. Hili ni somo kwa wabongo wote, tujaribu kuheshimu mikataba. Mambo siku hizi sio valuvalu kama zamani.
 
View attachment 2931230
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Omary Mwanga, maarufu Marioo, anayedaiwa zaidi ya Sh. milioni 500 kwa kuvunja mkataba, anatarajiwa kujitetea Mahakama Kuu Machi 18 na 19, mwaka huu.

Marioo na Meneja wake Sweetbert Mwinula wameshtakiwa katika Mahakama Kuu Masjala ya Wilaya ya Arusha mbele ya Jaji Joackim Tiganga, wakidaiwa jumla ya Sh. 550,000,000 kwa madai ya kuvunja mkataba wa kutumbuiza katika hafla ya Mr & Miss Vyuo Vikuu Kanda ya Kaskazini.

Mdai katika shauri hilo ni Kampuni ya Kismaty inayojihusisha na kuandaa matukio ya burudani mbalimbali nchini.

Mdai anayewakilishwa na Wakili John Lairumbe, anadai kuwa Septemba 23, 2021, aliingia mkataba na wadaiwa kutumbuiza siku ya mashindano hayo kwa gharama ya Sh. milioni 15.

NIPASHE
Hiyo kampuni hata kushika 30m yao hawajawahi...wanataka 550m kiulaini tu
 
Marioo kwa sasa anachukua mpaka 50m per show.
Hivi milioni 50 unazijua unazisikia?? Show ya 50M inataka mashabiki wasiopungua 5,000!! Kwa ukumbi hupi wa kuingiza watu 5 elfu?? Na sehemu gani kwa Tanzania utakusanya watu elfu 5 kwa mkupuo?? Labda kwenye majiji
 
😂😂 dah
Mil 15 kwa 550
Ni masuala ya legal justification tu ground ya kupambania ni mahakani, umehichanganya ukajaa unategema nini, kesi ya kuku tu inakuweka jela miaka mi 5 sembuse hizo 15milions za uwekezaji. Hapo inatajwa misamiati mikubwa mikubwa tu ya kiuwekezaji ili 15m ikukamue 550mls.

NB
usipende jasho la mwanaume mwenzio bure bure
 
Hivi milioni 50 unazijua unazisikia?? Show ya 50M inataka mashabiki wasiopungua 5,000!! Kwa ukumbi hupi wa kuingiza watu 5 elfu?? Na sehemu gani kwa Tanzania utakusanya watu elfu 5 kwa mkupuo?? Labda kwenye majiji
Wapumbavu tu hawa akina sinza pazuri ma pusha wa drugs tu ndio maana wamehifichia huko kwenye mamiziki. Ukamlipe 50M Marioo kwa show ya masaa ??? Bado bado
 
Ni masuala ya legal justification tu ground ya kupambania ni mahakani, umehichanganya ukajaa unategema nini, kesi ya kuku tu inakuweka jela miaka mi 5 sembuse hizo 15milions za uwekezaji. Hapo inatajwa misamiati mikubwa mikubwa tu ya kiuwekezaji ili 15m ikukamue 550mls.

NB
usipende jasho la mwanaume mwenzio bure bure
Unadhani maisha ni rahisi kiasi hicho?

Kwamba unaweza kuinvest 15m ukaleta porojo tu, within 1 month ikazalisha 35x?

Get a life bro.
 
Back
Top Bottom