Manager wa wema sepetu, martin kadinda ameibuka na kusema " Wema hana pesa ya kunilipa mimi. Ninachokifanya ni kuhangaika kutafuta dili mimi na yeye tusilale njaa, maisha ni kutegemeana."
Kadinda alisema yeye na wema hawana mkataba wa kulipana mshahara mwisho wa mwezi na kama ingekuwa hivyo, wema asingemudu.
Alisema "kikubwa ninachomudu ni kutafuta dili za kazi nyingi ili tuweze kupeana pasu, lakini si mshahara. Hata hivyo alisema yupo na wema kikaribu kikazi kwa sababu anajua ni mtu wa namna gani na anafanya kazi zake za uhuru bila kubanwa.