Maruhani au majini wanatoaje kw mwili mwa mtu?

Maruhani au majini wanatoaje kw mwili mwa mtu?

Ndiyo maana nikasema sina tatizo na unacho amini wewe,ila kiuhalisia ni ngumu kuniambia kwamba tiba ya matatizo ya uchawi na majini hupatatikana kupitia imani moja tu ya Yesu.

Hao wengine matatizo yao huyamaliza vp na hawajawahi kwenda huko kwenye maombi? hebu tuyalete mambo kwenye uhalisia.
Kuna watu wanazaliwa na matatizo na kuishi nayo maisha yao yoote! Kila wanapotafuta ufumbuzi wa tatizo wanatatuliwa kwa muda tu ila huendelea na matatizo yao mpaka wanayaacha haya makazi ya mwili wa damu na nyama. Ila suluhisho kamili lipo kwa Yeye ambaye ni Njia Kweli na Uzima.
 
Jina na Yesu linaondoa Majini kwa mtu yeyote, awe Mhindu, Mbudha au Mpagani.
Linafanya kazi kwa yeyote na popote.
Hata Sheick Yahya Hussein ali kiri hivyo enzi ya uhai wake.

Adui anayeweza kumshinda Shetani na watenda kazi wake (majini) ni Yesu pekee.

Ushahidi wa kihistoria unathibitisha kuwa mtu wa kwanza kufukuza majini kwa kauli tu, na kuyaamuru kwa kwenda, alikuwa Yesu Kristo wa Nazareti.
Majini pia yamethibitisha kuliogopa hilo jina, hayakuwahi kufanya upinzani na kushinda mbele yake.
Ni uamuzi wako sasa, ubaki na majini yako au uliite jina la Yesu liyaondoe.
Hakuna ushahidi mwingine wa wazi uliotolewa hadharani ulioweza kufanikisha zoezi la kufukuza majini kwa binadamu hadi hii leo.
Acha kudanganya watu jina la yesu limtoe shetani mwilini mwa Binadamu utakuwa unafikia kwa kutumia tumbo na si kichwa
 
Kutofautiana kwa uelewa kati ya mtu na mtu hutokana na mafundisho au mtazamo juu ya elimu kuhusu mambo haya. Wapo waliofundishwa kuwa kuna majini wazuri na wabaya. Lakini ukiangalia chanzo cha hao majini mpaka kuitwa majini ilitokana na uasi wao huko mbinguni, kabla hawajawa majini walikuwa ni malaika tena watakatifu.
Mi navyojua huyo malaika aliitwa shetani baada ya uasi na si jini,labda nikuulize kwanini aliitwa hivyo?
 
Ujue watu wanachanganya.
Kuna Historia na Hadithi

Hadithi ni Stori za kutunga kama zile za Adili na Nduguze, Bulicheka nk.

Historia ni Habari za kweli zilizotokea zamani. Mfano, Uhuru wa Tanganyika wa mwaka 1961.

Nadhani hii unayosema wewe ya Binadamu kuishi na kushirikiana na Majini na kuonana kwa macho ya mtu ya nyama, ni Hadithi tu za kutunga.

Nina uhakika wewe na mimi hatujawahi kumwona Jini uso kwa uso. Hata umbile la Jini au Ruhani hatulijui.
Aliyeliona Jini basi aje atueleze lipoje.

Hakuna Historia, wala Habari ya kweli inayosema Binadamu alishirikiana na Jini na kuonana ana kwa ana, uso kwa uso, na kufanya kazi zinazoonekana kama, Kulima, Kuvua, Kujenga nk.
Kama Historia hiyo ipo mahali basi anayeijua atuoneshe ni kitabu gani cha Kitaaluma au Kihistoria kimeandika habari hiyo.
Jini lipo katika hali ya Roho, tena ni Roho Mbaya, Chafu, yenye Uovu wote.
Unaosikia wanashirikiana na Majini ni hao Wagangawachawi, na wanashirikiana kiroho tu.
Yaani wanamwomba Shetani ili waingiwe na Majini kwenye mwili wao, Majini hayo yanawawezesha kufanya mambo mabaya kama, Kuroga, watu, Kuagua, Kutapeli watu, Kuiba, Kuua nk.

Ndio hivyo Mkuu.
Kwa nyongeza tu ni hivi, hakuna lisilowezekana katika roho. Hata mchawi anao uwezo wa kujionesha kwa mtu wa kawaida akiwa katika hali yake ya kiroho giza na akamtisha sana mtu. Halikadhalika kwa majini, wanao uwezo wa kujionesha mbele ya mtu physically! Ila wanajionesha zaidi au maranyingi sana katika ulimwengu wa kiroho kuliko damu na nyama. Kama majini hapo kabla walikuwa watakatifu (malaika) kisha wakaasi na kuwa mashetani basi wanao uwezo wa kujionesha kwa wanadamu waziwazi. Ukisoma kitabu cha Mwanzo katika kisa cha Lutu (Sodoma na Gomora) au kitabu cha waamuzi wazazi wa Samsoni walimwona malaika physically, pia kitabu cha Joshua alipokutana na malaika wa jeshi la mbinguni uso kwa uso, mzee Yakobo (Israel) alipambana naye mapaka alfajiri na pia Petro akiwa gerezani alidhani anaona maono kumbe ilikuwa ni physically mpaka akakiri kuwa hayakuowa maono bali ni wazi wazi.
Nyongeza:-
Mungu ni tajiri saana! Karama zake hazina majuto, alipomfukuza shetani na wafuasi wake hakuwanyang'anya uwezo waliokuwa nao, ila, aliliondoa Jina Lake ambalo ni Nuru. Ndiyo maana shetani amefungwa katika kifungo cha giza (hajui kutenda lililo jema tangu hapo) mpaka siku ya mwisho iliyowekewa mhuri, anayeijua ni Mungu pekee.
 
Kuna watu wanazaliwa na matatizo na kuishi nayo maisha yao yoote! Kila wanapotafuta ufumbuzi wa tatizo wanatatuliwa kwa muda tu ila huendelea na matatizo yao mpaka wanayaacha haya makazi ya mwili wa damu na nyama. Ila suluhisho kamili lipo kwa Yeye ambaye ni Njia Kweli na Uzima.
Bado upo kiimani zaidi ila kiuhalisia haupo sahihi.

Na tatizo lenu ni moja pale mnaposema kwamba kuna nguvu aina mbili yani ya Mungu na ya shetani,haoa huwa mnakosea shetani nguvu kazitolea wapi?
 
Anaishi mkoa gani? Majini yanaondolewa kupitia Jina la Yesu tu, mbali na hapo ni kuyatuliza.
 
Shetani tafsiri yake ni muasi. Wewe unaelewaje?
Upo sawa,kwa hivyo utaona kuwa neno shetani ni kiumbe aliyeasi kwa maana hata binaadamu huweza kuwa shetani endapo atamuasi Mungu.

Ila tunapozungumzia jini huyu ni kiumbe mwengine hana sifa za malaika.
 
Anaishi mkoa gani? Majini yanaondolewa kupitia Jina la Yesu tu, mbali na hapo ni kuyatuliza.
Kwanini iwezekane kuyatuliza na ishindikane kuyaondoa? hivi kwa mfano yale maombezi ya makanisani kwa wenye majini,huwa tunaona watu wakianguka na baadaye kurudia katika hali zao za kawaida je,pale ndiyo huwa majini yameshatoka kwa jina la Yesu?
 
Dah mi nina ndugu yangu nimehangaika mwaka wa 4 nisijue la kufanya yani. Si hospitali, si kanisani si kwa sharif majini ila bado ndugu yangu anateseka.
Hali ilianza kipindi amejipanga kuoa tu, alikuwa na wasichana wawili anawatazamia achukue mmojawapo kilichokuja tokea katikati ya mchakato barua ya posa ikakataliwa, akaanza badilika mara anakuwa kama ana loose memory, baadae akaanza kuongea mwenyewe, ukiskiliza kinachoongelewa ni kama mtu anamlazimisha kuoa mwanamke mmoja kati ya wale wawili. Alikua na biashara anafanya vizuri sana ikavurugika akaibiwa vitu baadae akarudi nyumbani kabisa.

This is the 4th year analazimishwa kuoa tu na kitu ambacho nadhani ni hilo pepo. Zamani alikuwa halali anaongea usiku kucha sahizi walau kimetulia kidogo tulimpa ma anti-depressant mwaka mzima tukijua labda alipata depression baada ya kukataliwa barua ya posa. Well sasa ni dhahiri haikuwa depression bali ni jini. Nilimtafuta hadi yule mtu mzito ila haikufaa nilipoteza pesa tu, nmeenda vatcan sinza kwa yule mchungaji holaaa... nimeenda kwa sharif majini mabibo chenga yani anaeweza kunipa reference ya kutatua hili tatizo anisaidie.
 
Acha kudanganya watu jina la yesu limtoe shetani mwilini mwa Binadamu utakuwa unafikia kwa kutumia tumbo na si kichwa
Jamii Forum ni jukwaa la kuelimishana na kubadilishana mawazo.
Kama limetolewa wazo na halifanani na mawazo yako unaweza kileta mawazo yako ili na sisi tuelimike.
Kitendo cha kumdhihaki mtu au kumtukana kwakuwa tu hajasema kama unavyofikiri si kitemdo cha kistaarabu hata kidogo.
Na haiwezekani jukwaa hili likawa na watu wanaozungumza wazo moja tu ambalo linapendwa na msomaji.
Kama una elimu mbadala tueleze na sisi tujifunze toka kwako na sio una nukuu watu na unaishia kuwadhihaki bila sababu.
Heshima ni kitu cha bule ndugu, na kama hupendi wazo fulani na huna cha kusema sio vibaya ukakaa kimya.

Huna tabia nzuri na inakulazimu ujirekebishe.
 
Ujue watu wanachanganya.
Kuna Historia na Hadithi

Hadithi ni Stori za kutunga kama zile za Adili na Nduguze, Bulicheka nk.

Historia ni Habari za kweli zilizotokea zamani. Mfano, Uhuru wa Tanganyika wa mwaka 1961.

Nadhani hii unayosema wewe ya Binadamu kuishi na kushirikiana na Majini na kuonana kwa macho ya mtu ya nyama, ni Hadithi tu za kutunga.

Nina uhakika wewe na mimi hatujawahi kumwona Jini uso kwa uso. Hata umbile la Jini au Ruhani hatulijui.
Aliyeliona Jini basi aje atueleze lipoje.

Hakuna Historia, wala Habari ya kweli inayosema Binadamu alishirikiana na Jini na kuonana ana kwa ana, uso kwa uso, na kufanya kazi zinazoonekana kama, Kulima, Kuvua, Kujenga nk.
Kama Historia hiyo ipo mahali basi anayeijua atuoneshe ni kitabu gani cha Kitaaluma au Kihistoria kimeandika habari hiyo.
Jini lipo katika hali ya Roho, tena ni Roho Mbaya, Chafu, yenye Uovu wote.
Unaosikia wanashirikiana na Majini ni hao Wagangawachawi, na wanashirikiana kiroho tu.
Yaani wanamwomba Shetani ili waingiwe na Majini kwenye mwili wao, Majini hayo yanawawezesha kufanya mambo mabaya kama, Kuroga, watu, Kuagua, Kutapeli watu, Kuiba, Kuua nk.

Ndio hivyo Mkuu.


Mkuu asante sana kwa kunifunza

Kuna kitabu niseme kama sijakosea nisahihishe .

Kinaitwa TOBITI katika biblia kinamuhusu Tobia je hicho kitabu ni HADITHI ZA KUTUNGA,HISTORIA AU UKWELI HALISI?
 
Mkuu unataka kusema kwamba hizi habari za majini unazoeleza hapa umezitoa kwa Sheikh Yahya?
Sio,
Mimi nasoma sana Kitabu Kitakatifu cha Biblia ambacho ndicho kinachonipa ufahamu wa Elimu ya Kiroho.
Ukisoma Biblia, Kwa umakini, polepole, na kwakurudirudia wakati umeituliza akili yako, utapata maarifa mengi yanayo husu Ufalme wa Mbingu na ule wa Kuzimu.
Kwa hapa duniani mafundisho ya Scoan ambayo nimekueleza kuangalia video zake yamenipa ufahamu zaidi wa Elimu ya Kiroho.
Sheikh Yahaya Husseini nilikuwa namsikiliza tu alipokuwa anatoa Elimu ya Majini.
Kwakuwa alikuwa hajasoma Biblia nakuielewa, yeye alijihusisha zaidi katika upande wa mahusiano ya Majini na Binadamu, kwa mtazamo wa wale wanaoona kuwa ati,
"kuna Majini Mazuri yanayoweza kushirikiana na Binadamu katika kazi za maendeleo"

Mimi nakanusha hiyo hoja. Nasema,
"Majini yote ni maovu kwa Binadamu"

Mimi uelewa wangu umetokana na kusoma Biblia kwa bidii.

Nawewe hebu nieleze unachojua kuhusu elimu ya Majini.
Je yako mazuri ?
Je yanashirikianaje na binadamu ?
Je yakimwingia mtu yanatolewaje ?
Unayapenda Majini ?

Lete habari mkuu unavyoelewa wewe.
 
Mkuu asante sana kwa kunifunza

Kuna kitabu niseme kama sijakosea nisahihishe .

Kinaitwa TOBITI katika biblia kinamuhusu Tobia je hicho kitabu ni HADITHI ZA KUTUNGA,HISTORIA AU UKWELI HALISI?
Kitabu cha TOBITI ni cha hadithi za Wayahudi, na hakipo kwenye vitabu vya Historia za Wayahudi.
Kitabu hicho pamoja na YUDITHI ni hadithi za kutunga tu za Wayahudi.
Vitabu hivyo vimeongezwa tu kwenye Biblia wanazotumia Wayahudi.
Havipo kwenye Biblia wanazotumia Wakristo.
Vitabu vya Tobiti, Yudithi, Wamakabayo wa 1, na Wamakabayo wa 2, Hekima ya Sulemani, Hekima ya Yoshua Bin Sira, vinaitwa vitabu vya DEUTEROKANONI,
vipo kwenye biblia ya Kiyahudi kama nyongeza ya Hadithi na Simulizi zao.
Biblia ya Wakristo haina hivyo vitabu, Ina vitabu 66.
Biblia ya Kiyahudi ina vitabu 72 pamoja na hivyo nilivyokutajia.

Unajua Historia inaendana na ukweli.
Kwa mfano,
Kwenye Biblia, vitabu vya Injiri vinasema Yesu Kristo azaliwa huko Israeli na alikuwa Masihi wa Mungu.
Vitabu vya Historia ya Israeli navyo pia, vinasema Yesu Kristo alizaliwa na kuishi Israeli, alikuwa Nabii na mafundisho yake yapo.
Leo ukienda kutalii Israeli utaambiwa kuhusu maisha halisi ya Yesu Kristo huko Israeli, na utaoneshwa alipozaliwa, alipohubiri, alipoteswa, alipokufa, alipozikwa, alipofufuka na alipopaa Mbinguni.
Hivyo unaona Historia na Ukweli vinaenda pamoja.
Lakini maelezo ya vitabu vya TOBITI na YUDITHI hayaonekani kwenye Historia wala kwenye Utalii wa Israeli.
Hapo ndipo utakapo hakikisha kuwa hizo zilikuwa Hadithi tu za kutunga za Waisraeli.
Kwenye Biblia hivyo vitabu havipo.
Vitabi vya DEUTEROKANUNI.
 
Kuna ushahidi gani wa mtu kutolewa majini kwa jina la Yesu? hebu nipe huo ushahidi.
Hata huko makanisani hayaondoki, ukitaka kudhibitisha hilo, nenda kwenye makanisa haya yanayoitwa ya kiroho, utaona watu wanaondolewa mapepo, kama wanavyoyaita ni walewale wa wiki iliyopita.
 
Sio,
Mimi nasoma sana Kitabu Kitakatifu cha Biblia ambacho ndicho kinachonipa ufahamu wa Elimu ya Kiroho.
Ukisoma Biblia, Kwa umakini, polepole, na kwakurudirudia wakati umeituliza akili yako, utapata maarifa mengi yanayo husu Ufalme wa Mbingu na ule wa Kuzimu.
Kwa hapa duniani mafundisho ya Scoan ambayo nimekueleza kuangalia video zake yamenipa ufahamu zaidi wa Elimu ya Kiroho.
Sheikh Yahaya Husseini nilikuwa namsikiliza tu alipokuwa anatoa Elimu ya Majini.
Kwakuwa alikuwa hajasoma Biblia nakuielewa, yeye alijihusisha zaidi katika upande wa mahusiano ya Majini na Binadamu, kwa mtazamo wa wale wanaoona kuwa ati,
"kuna Majini Mazuri yanayoweza kushirikiana na Binadamu katika kazi za maendeleo"

Mimi nakanusha hiyo hoja. Nasema,
"Majini yote ni maovu kwa Binadamu"

Mimi uelewa wangu umetokana na kusoma Biblia kwa bidii.

Nawewe hebu nieleze unachojua kuhusu elimu ya Majini.
Je yako mazuri ?
Je yanashirikianaje na binadamu ?
Je yakimwingia mtu yanatolewaje ?
Unayapenda Majini ?

Lete habari mkuu unavyoelewa wewe.
Mkuu unaitaja tu biblia,unaonaje sasa ukatoa vifungu kutoka kwenye biblia vinavyoeleza haya uliyoyaeleza hapa kuhusu majini?

Hebu tumia biblia kutupa somo la hawa viumbe.
 
Kitabu cha TOBITI ni cha hadithi za Wayahudi, na hakipo kwenye vitabu vya Historia za Wayahudi.
Kitabu hicho pamoja na YUDITHI ni hadithi za kutunga tu za Wayahudi.
Vitabu hivyo vimeongezwa tu kwenye Biblia wanazotumia Wayahudi.
Havipo kwenye Biblia wanazotumia Wakristo.
Vitabu vya Tobiti, Yudithi, Wamakabayo wa 1, na Wamakabayo wa 2, Hekima ya Sulemani, Hekima ya Yoshua Bin Sira, vinaitwa vitabu vya DEUTEROKANONI,
vipo kwenye biblia ya Kiyahudi kama nyongeza ya Hadithi na Simulizi zao.
Biblia ya Wakristo haina hivyo vitabu, Ina vitabu 66.
Biblia ya Kiyahudi ina vitabu 72 pamoja na hivyo nilivyokutajia.

Unajua Historia inaendana na ukweli.
Kwa mfano,
Kwenye Biblia, vitabu vya Injiri vinasema Yesu Kristo azaliwa huko Israeli na alikuwa Masihi wa Mungu.
Vitabu vya Historia ya Israeli navyo pia, vinasema Yesu Kristo alizaliwa na kuishi Israeli, alikuwa Nabii na mafundisho yake yapo.
Leo ukienda kutalii Israeli utaambiwa kuhusu maisha halisi ya Yesu Kristo huko Israeli, na utaoneshwa alipozaliwa, alipohubiri, alipoteswa, alipokufa, alipozikwa, alipofufuka na alipopaa Mbinguni.
Hivyo unaona Historia na Ukweli vinaenda pamoja.
Lakini maelezo ya vitabu vya TOBITI na YUDITHI hayaonekani kwenye Historia wala kwenye Utalii wa Israeli.
Hapo ndipo utakapo hakikisha kuwa hizo zilikuwa Hadithi tu za kutunga za Waisraeli.
Kwenye Biblia hivyo vitabu havipo.
Vitabi vya DEUTEROKANUNI.
 
Kitabu cha TOBITI ni cha hadithi za Wayahudi, na hakipo kwenye vitabu vya Historia za Wayahudi.
Kitabu hicho pamoja na YUDITHI ni hadithi za kutunga tu za Wayahudi.
Vitabu hivyo vimeongezwa tu kwenye Biblia wanazotumia Wayahudi.
Havipo kwenye Biblia wanazotumia Wakristo.
Vitabu vya Tobiti, Yudithi, Wamakabayo wa 1, na Wamakabayo wa 2, Hekima ya Sulemani, Hekima ya Yoshua Bin Sira, vinaitwa vitabu vya DEUTEROKANONI,
vipo kwenye biblia ya Kiyahudi kama nyongeza ya Hadithi na Simulizi zao.
Biblia ya Wakristo haina hivyo vitabu, Ina vitabu 66.
Biblia ya Kiyahudi ina vitabu 72 pamoja na hivyo nilivyokutajia.

Unajua Historia inaendana na ukweli.
Kwa mfano,
Kwenye Biblia, vitabu vya Injiri vinasema Yesu Kristo azaliwa huko Israeli na alikuwa Masihi wa Mungu.
Vitabu vya Historia ya Israeli navyo pia, vinasema Yesu Kristo alizaliwa na kuishi Israeli, alikuwa Nabii na mafundisho yake yapo.
Leo ukienda kutalii Israeli utaambiwa kuhusu maisha halisi ya Yesu Kristo huko Israeli, na utaoneshwa alipozaliwa, alipohubiri, alipoteswa, alipokufa, alipozikwa, alipofufuka na alipopaa Mbinguni.
Hivyo unaona Historia na Ukweli vinaenda pamoja.
Lakini maelezo ya vitabu vya TOBITI na YUDITHI hayaonekani kwenye Historia wala kwenye Utalii wa Israeli.
Hapo ndipo utakapo hakikisha kuwa hizo zilikuwa Hadithi tu za kutunga za Waisraeli.
Kwenye Biblia hivyo vitabu havipo.
Vitabi vya DEUTEROKANUNI.
Asante mkuu.

Je ni vitabu gani vingine ambavyo ni hadithi za kutunga vipo katika biblia ya wakristo?
Je biblia ya wautumiayo wakatoliki si ya wakristo na wao si wakristo na kwanini unazani waliweka vitabu vya Tobiti na Yudithi ile hali havina ukweli?

Je kuna uwezekano kuwa kuna stori za kutunga hasa ukisoma Luka moja na kuendelea?

Maana inaonesha watu walijitungia injiri wakawepo watu maalumu wa kuipitisha iwe kwa matakwa yao ama lah.

Kwanini tuamin Yohana,Warumi na tusiamin Tobia na Yuditdhi?

Kwanini nisiseme tunaamin kile tulichokalilishwa na wale wenye nguvu na kipaji cha kuaminisha?

Kwanini isiwe vitabu vyote ni utunzi wa watu maalumu kwa malengo maalumu?
 
Back
Top Bottom