Masahihisho kwa Wapotoshaji: Mdude Nyagali aliishinda Serikali Mahakamani, hakutolewa jela kwa Msamaha wa Rais

Masahihisho kwa Wapotoshaji: Mdude Nyagali aliishinda Serikali Mahakamani, hakutolewa jela kwa Msamaha wa Rais

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Pamoja na yote yanayoendelea kuhusu Mdude, ambayo nisingependa kuyarudia hapa, kinachopaswa kufahamika ni kwamba Mdude Nyagali alitolewa gerezani baada ya kuishinda serikali ya Tanzania Mahakamani.

Hakutolewa kwa Msamaha wa Rais wala hakutolewa kwa Huruma ya Mtu yeyote yule, alishinda Kesi ya kubambikwa, ya uongo iliyotungwa ili kumkomoa, shukrani kwa Chama chake na Jopo la Mawakili wake wakiongozwa na Mangula.

Wale wanaotaka anyamaze kama zuzu, yaani akae tu kimya kama ndondocha wa kiarabu pamoja na unyama wote aliotendewa kuanzia kule walikoshindwa kumuua baada ya Mungu na Wazungu kuingilia kati, hadi hizi njama za madawa ya kulevya, hatukuwasikia wakikemea unyama aliotendewa, na itambulike wazi kwamba waliomtesa na ambao walitaka kumuua Mdude bado wapo na wapo madarakani, kuanzia viongozi wa juu, watekaji, polisi na wengine wengi, aliyepungua ni mmoja tu, kwahiyo tunapomkosoa Mdude kwa kauli zake tufikirie pia aliyotendewa na watu hawahawa tunaowatetea.
 
Pamoja na yote yanayoendelea kuhusu Mdude , ambayo nisingependa kuyarudia hapa , kinachopaswa kufahamika ni kwamba Mdude Nyagali alitolewa gerezani baada ya kuishinda serikali ya Tanzania Mahakamani...
Yote hayo hayajalishi haina maana ya yeye kutumia maneno machafu na matusi kukosoa utawala kwani akitumia lugha ya kistaarabu atapungukiwa na nini?
 
Pamoja na yote yanayoendelea kuhusu Mdude , ambayo nisingependa kuyarudia hapa , kinachopaswa kufahamika ni kwamba Mdude Nyagali alitolewa gerezani baada ya kuishinda serikali ya Tanzania Mahakamani...
Hawakuwa na haja nae tena. Mdude toka zamani ana lugha za matusi tena ya nguoni kwa viongozi. Hana maadili na ni aibu Chadema kumlea namna hii.

Kama kweli ana ngozi ngumu arudie yale matusi yake kama alivyofanya kwa JPM then ndio mtajua ni vipi kuna mambo yana mipaka.
 
Hawakuwa na haja nae tena. Mdude toka zamani ana lugha za matusi tena ya nguoni kwa viongozi. Hana maadili na ni aibu Chadema kumlea namna hii.

Kama kweli ana ngozi ngumu arudie yale matusi yake kama alivyofanya kwa JPM then ndio mtajua ni vipi kuna mambo yana mipaka.
Ni kwamba labda tuwe wastaarabu tu kutokana na nyakati, jambo ambalo ni jema, lakini usitutishe, kama pamoja na ukatili wa jiwe lakini bado alipigwa Spana unadhani ndio tuogope sasa?
 
Yote hayo hayajalishi haina maana ya yeye kutumia maneno machafu na matusi kukosoa utawala kwani akitumia lugha ya kistaarabu atapungukiwa na nini?
Anajua akina Kibatara watamtetea tena! Stupid arrogance.

Rais anakosolewa kwa staha, kuheshimu Mkuu wa nchi ni lazima hata vitabu vya dini vinaelekeza. Huwezi kuzungumzia Rais kama unaongea na wahuni.
 
Anzeni kumtukana ndo mtajua kama mwanga umeonekana.

Mkoa niliopo leo asubuhi.kuna kijana mmoja katapika maneno kuwa huyu mama hafai kuwa raisi na maneno yenu yale machafu police wamepita nae kma kipanga kwa sasa yupo kuho kituoni.

Anajutia mdomo wake.

Sasa kama mnaona mwanga basi mtukaneni kama mlivyokuwa mnamtukana Magufuli.
at least kidogo mwanga unaonekana siyo kama kipindikile cha uongozi wa kishetani wa Meko
 
Mimi nimejitolea kumtetea mdude Nyagali nyie Chadema mnamharibu huyu kijana kwa siasa za majitaka muacheni afurahie maisha ya uraiani mngekuwa,mnampenda msingeweza kuanza kumzungusha zungusha saa hizi mnafanya siasa za kitoto kijinga na za kipumbavu kumbukeni watoto wenuu hamuwatangulizi mnaanza tena kumtumia kijana wa watu akamatwe tena kuweni na huruma kabisa.
 
Wakati vitabu vya dini vinaandikwa hakukuwepo na Marais kama hawa wa sasa, kulikuwa na madikteta tu wanaojitwalia madaraka.
Anajua akina Kibatara watamtetea tena! Stupid arrogance.

Rais anakosolewa kwa staha, kuheshimu Mkuu wa nchi ni lazima hata vitabu vya dini vinaelekeza. Huwezi kuzungumzia Rais kama unaongea na wahuni.
 
Back
Top Bottom