Anayedaiwa kuwa Afisa Usalama (TISS) afanya vurugu, amjeruhi mwananchi.
Tukio la kutisha lilitokea jana usiku (26.10.2024) katika klabu maarufu inayojulikana kama 1245 Lounge, Bar and Restaurant iliyopo Masaki, ambapo Afisa Usalama wa Taifa anayefahamika kwa jina la Derick Junior Lima (maarufu kama Chief Abayomi) alianzisha fujo na kujaribu kumpiga risasi Julian Bujulu baada ya kutokea sintofahamu kati ya Derick na Julian iliyosababishwa na Derick kujaribu kulazimisha kuondoka na mwanamke aliekuwa ameenda kustarehe katika Club hiyo akiambatana na Julian.
Taarifa zinaeleza zaidi kwamba Derick ni mtu mwenye mke na watoto na kwamba mwanamke anayehusishwa na ugomvi huo ni Dada yake Julian ambapo walikuwa wametoka pamoja kwenda kwenye starehe.
Kwa mujibu wa mashuhuda, ghasia zilianza baada ya Derick kutaka kuondoka na mwanamke huyo kwa nguvu bila kujali yupo na kina nani, jambo lililopelekea Kaka mtu kuingilia kati akizuia Dada yake kuondoka na Derick. Mzozo huo ulipopamba moto, Derick alitoa bastola akiwa na lengo la kumpiga risasi Julian lakini kwa bahati nzuri, bastola ya Derick iligoma kutoa risasi. Baada ya kushindwa kupiga risasi, kwa hasira Derick aliamua kumpiga Julian kichwani kwa kutumia kitako cha bunduki hiyo na kumsababishia majeraha makubwa.
Kamera za CCTV katika klabu hiyo zimenasa tukio zima jinsi Derick alivyotenda na kusababisha majeruhi makubwa kichwani yaliyopelekea kuwahishwa hospitali na baadae kuhamishiwa Hospitali ya Muhimbili ambapo amelazwa kwa matibabu zaidi.
Mpaka wakati huu, Derick Lima anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Oysterbay huku uchunguzi ukiendelea. Kuna wasiwasi mkubwa kwamba haki haitatendeka kutokana na uhusiano wake wa karibu na wakubwa. Mpaka sasa kuna baadhi ya βMatajiriβ wa mjini ambao wamekuwa wakimtumia Derick katika kukwepa kodi na kutekeleza mambo yao haramu wamekuwa wanaendelea na jitihada kuhakikisha anatoka mikononi mwa polisi bila kuwa na kesi.
Polisi wamechukua mashine za CCTV katika Club hiyo na katika kuhakikisha mmiliki wa Club hiyo anaminywa na asitoe ushirikiano, wameachia makusudi video inayomuonyesha mmiliki huyo akifanya mapenzi na mmoja wa aliekuwa mfanyakazi wake katika moja ya ofisi za Club hiyo.
kKwamba derick anachukiwa au mmiliki wa bar aliepiga tako tatu au au uyo mwamba aliyenusurika kuuawa?
au ni chuki dhidi ya jeshi letu pendwa la mapongo?
Kama ilivyokuwa kwa Nguza Samike katibu binafsi wa Rais Magufuli na sasa tuna Waziri Rajab Salum katibu binafsi wa Rais Samia. Huyu ndiye mtendaji wa shughuli zote binafsi za Rais Samia katika masuala ya utawala na serikali. Huyu ndiye mwandishi wa hotuba za Rais, hivyo Rais siku akipatia...
Mbombo ngafu, ila vijana wa Dar laini sana, yaani huyo jamaa unampiga kumbo la horse power milioni Mia, mnaenda chini wote, halafu yanayofuata ni balaa tupu.
Ila huyo msaidizi wa rais mimi huwa namuangalia halafu simuamini
Aisee, Wahuni wanapokuwa na nguvu wanyonge wapo mashakani. Pole kwa wote mnaoonewa haya yote yanamwisho. Mie sahivi mtu akijichanganya ni radi au namroga anapasuka moyo. Hii haina ushahidi kila mtu ashinde mechi zake
Jamaa sijui alitema shit gani mpaka ashushiwe kipondo nusu achapwe shaba.
Ni kesi kubwa kwa kajamba nani, ila kama yupo karibu na wenye vyeo na anafanya kazi zao vyema basi hamna kesi hapo kibongobongo
Aisee! Kuna aina ya watu hutakiwi hata uji associate nao na kuna club siendi, call me old school but wacha tu baadhi ya vitu vinipite.
Alafu wakinadada sisi nao kuna saa tuko cheap π Yani nkiangalia hapo hao wanaofanya wakaka watoane damu na huyo aliyeinamishwa hapo on the other video nikiwacombine wote sijui kama hata 5M kwnye account wanazo lakini ndio wamejiassociate na watu wa ovyo hivyo π
Tusharudi tulikotoka, ukitoka kwenda club na mkeo ama dada yako uwe makini - anaweza kubebwa wa nguvu akaingizwa wa gari akafanywa live huku ukishuhudia au lah ukubali kupoteza maisha.
Aisee! Kuna aina ya watu hutakiwi hata uji associate nao na kuna club siendi, call me old school but wacha tu baadhi ya vitu vinipite.
Alafu wakinadada sisi nao kuna saa tuko cheap π Yani nkiangalia hapo hao wanaofanya wakaka watoane damu na huyo aliyeinamishwa hapo on the other video nikiwacombine wote sijui kama hata 5M kwnye account wanazo lakini ndio wamejiassociate na watu wa ovyo hivyo π
Taasisi ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi iko wapi?? Askari anaskika akisema kabisaa hiii siiachi yaani Video ya ngono na hakuishia hapo akairusha mtandaoni. Aibu sana kwa jeshi letu. Aibu sana hii.