Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

Hapo lile tukio limeangukia kwny kifungu gani..?
9cbe1dee0f038d34d0ba7d659663a377.jpg
 
Unajua iyo risasi ni kodi yetu sisi? Bei ya risasi unaijua?
Ni kodi zenu sawa ndo mvunje sheria??kwa vile ni kodi zenu shuleni si mlikuwa mnapeleka rimu kwa ajili ya matumizi ya mitihani kuna siku ulipewa alama 100%kuwa mwalimu amekupa baada ya kuwa mpeleka rimu bora???
 
Askari hovyo sana huyu eti ameapa. Kiapo chako hakizui Mwananchi kuhoji uhalali wa vitendo vyako hasa unapoenda kinyume na haki za raia. Askari mpuuzi kweli.
 
Binafsi nachukizwa sana na hii operation liyoibuka hivi karibuni hapa Dar es salaam inayoitwa wrong parking.
Wahanga wa hii operation ni wa wamiliki wa vyombo vya moto hasa magari.
Kampuni za udalali zinaenda vtuo vya polisi na kuwachukua askari wenye silaha na kuanza kutembetea mitaani kutafuta magari yaliyoegeshwa vbaya,wanasumbua sana watu barabarani kisa wako na polisi na matokeo yake ndo kama hayo.Inafanyika kati ya saa tatu asubuhi hadi saa kumi jioni na kila askari anashiriki katika operation hiyo hupewa kifuta jasho cha sh elfu 20.
Rai yangu ni kuwaomba viongozi wa wa manispaa zetu kuona namana mbadala ya kuliondoa tatizo hili na kuifuta operation hii maana ni kero kubwa sana,,kibaya zaidi ni kwamba sehemu kubwa ya pesa zinazotozwa zinawanufaisha hawa jamaa wanaokamata na sio serikali,,wanakamata magari 20 wanaandikia 5,,,iliyobaki ni halali yao.
 
Kwa ulichokiona, kulikuwa na ulazima gani kwa hao jamaa kupaki gari mahala siyo ruhusa kupaki!?

Kwa ulichokiona, kwa nini waongee hivyo kuwadharau polisi!?

Kwa ulichokiona, kwa nini wasitii Sheri na kuwa waadilifu!?

Polisi alifanya hivyo kukomesha midomo na wanaopenda kufata gari lao kwenda kituo cha polisi.

Ila polisi wetu wasilaumiwe
kwa sababu, nchi zingine huwa watu wanatii sheria bila shuruti mfano, kama ni no parking ( No ) wenzetu hawapaki kabisaa sasa sisi huko Tanzania inakuwaje!?

Tuache kutetea wavunja sheria kwa sababu ya vyeo, fedha au sababu zingine zingine tunazozijua.

Mfano, Barabara nyingi hapo Dar zimewekewa uzio wa kukataza kukatisha zile bustani sasa angalia barabara ya Mandela, Nyerere, kijitonyama kwenda city centre kila bustani hizo waenda kwa miguu wanakatiza na wenye magari wanazigonga.

Swali, mbona pale Mwenge mkono wa kushoto pana hizo bustani lakini watu hawakatishi na Magari hayagongi zile bustani!?

Jibu lake pale bustani ya Mwenge pana kakibao kadogo sana kameandikwa ONYO kukatisha bustani (JWTZ) na hakuna kweli anayegusa wala gari halijawahi kugusa wala kugonga ile bustani.

Sasa kwa nini, hao wasitii Sheria!?

Hili jambo, ukiliangalia kwa chuki zako kwa polisi utaona kuwa polisi kakosea ila hekima ya Malina ilipungua pale yeye Kama kiongozi tena mkubwa alipaswa kuonesha weredi na uwezo wa kuchambua mambo na hekima.

Acha , nisiseme sana ila haya mambo yanahitaji hekima na kutii sheria au amri bila shuruti.
Wangelipaki wapi na barabara zimejengwa kama corridor za guest house.
 
mkuu ile gari ndio wameichukua hao polisi au vipi, na hao majembe siku hizi wamekuwa walinzi
Tanzania haieleweki mlinzi halisi ni nani.Leo hii viongozi wa madereva bodaboda walishajigeuza nao trafic wanakamata na kutoza watu faini barabarani bila utaratibu.
Makampuni ya maegesho nao vivyo hivyo ni full kusumbua watu.Mbona majuzi ilitolewa taarifa kuwa hata kama ni wrong packing mtu akamatwe tu ikiwa kapaki zaidi ya saa moja.
In short kuna mapungufu mazito ktk sheria zetu(by laws).Imebaki udhalilishaji tu.
 
Wangelipaki wapi na barabara zimejengwa kama corridor za guest house.

Acha mawazo finyu.

Yeye tu ndiye ana gari au yeye pekee ndiye aliyepita barabara hiyo!?

Mbona hawajakamata wote watumiaji wa eneo hilo!?

Binafsi, huwa sitetei wavunja sheria hata wawe kwenye familia yangu!
 
Binafsi nachukizwa sana na hii operation liyoibuka hivi karibuni hapa Dar es salaam inayoitwa wrong parking.
Wahanga wa hii operation ni wa wamiliki wa vyombo vya moto hasa magari.
Kampuni za udalali zinaenda vtuo vya polisi na kuwachukua askari wenye silaha na kuanza kutembetea mitaani kutafuta magari yaliyoegeshwa vbaya,wanasumbua sana watu barabarani kisa wako na polisi na matokeo yake ndo kama hayo.Inafanyika kati ya saa tatu asubuhi hadi saa kumi jioni na kila askari anashiriki katika operation hiyo hupewa kifuta jasho cha sh elfu 20.
Rai yangu ni kuwaomba viongozi wa wa manispaa zetu kuona namana mbadala ya kuliondoa tatizo hili na kuifuta operation hii maana ni kero kubwa sana,,kibaya zaidi ni kwamba sehemu kubwa ya pesa zinazotozwa zinawanufaisha hawa jamaa wanaokamata na sio serikali,,wanakamata magari 20 wanaandikia 5,,,iliyobaki ni halali yao.
Umenena. Hii ndo inayotakiwa.
 
Acha mawazo finyu.

Yeye tu ndiye ana gari au yeye pekee ndiye aliyepita barabara hiyo!?

Mbona hawajakamata wote watumiaji wa eneo hilo!?

Binafsi, huwa sitetei wavunja sheria hata wawe kwenye familia yangu!
Wanayakamata sana wengine hawapendi kudai haki zao wanaona bora wanyamaze. Kelele zililetwa na wenye maduka yao na migahawa barabara ile maana wao ndio wahanga, wateja wao wakija kununua vitu lazima wawasumbue mpaka imepelekea wengine wasiwe wanaenda maeneo hayo
 
Binafsi nachukizwa sana na hii operation liyoibuka hivi karibuni hapa Dar es salaam inayoitwa wrong parking.
Wahanga wa hii operation ni wa wamiliki wa vyombo vya moto hasa magari.
Kampuni za udalali zinaenda vtuo vya polisi na kuwachukua askari wenye silaha na kuanza kutembetea mitaani kutafuta magari yaliyoegeshwa vbaya,wanasumbua sana watu barabarani kisa wako na polisi na matokeo yake ndo kama hayo.Inafanyika kati ya saa tatu asubuhi hadi saa kumi jioni na kila askari anashiriki katika operation hiyo hupewa kifuta jasho cha sh elfu 20.
Rai yangu ni kuwaomba viongozi wa wa manispaa zetu kuona namana mbadala ya kuliondoa tatizo hili na kuifuta operation hii maana ni kero kubwa sana,,kibaya zaidi ni kwamba sehemu kubwa ya pesa zinazotozwa zinawanufaisha hawa jamaa wanaokamata na sio serikali,,wanakamata magari 20 wanaandikia 5,,,iliyobaki ni halali yao.
Wanjusanya kodi, hujusikia bosi sao alivosema?
 
mimi nimeapa!!!

umeapa kufanya nini??

Swali zuri kweli kweli.Kuna huyu askari mwenzake aliyekuwa anajaribu kumtuliza huyu mwenzake,kwangu mm ningekuwa amiri jeshi huyu aliyekuwa anayemtuliza mwenzake ndiye anastahili kupandishwa cheo.Unapokuwa na silaha kama hiyo ya SMG hutakiwi kuwa na jazba.Askari ali-over react.Sitashangaa kama huyu aliyefyatua risasi atachukuliwa hatua.Malima alikuwa hana silaha ametulia,unafyatua risasi hewani ya nini?Tukio kidogo linafanana na Bw.Nape.Anyway,it could be doctored,who knows.
 
Kwahyo ww ulitakaje?
Hebu jivishe uhusika wa askari halafu Malima kapaki gari wrong packing wanashuka watu unaowasindikiza kwaajili ya kazi hyo ya kukamata wanaoegesha magari ovyo anawaita kuwa ni majambazi mpaka watu wanajaa kwaajili ya kuwadhuru.. Je ungefanyeje?
Acheni ishabiki
868803f0be597e253cdd025118aa0cb9.jpg
Shabiki ni wewe unayedhani kuwa wengine wote ni wageni hapa nchini. Ikiwa scenario ile ndio imeleta kadhia yote hiyo, basi kusingekuwa na salio la risasi huko maghalani. Ubishi mdogo ule risasi zinapigwa, je huko masokoni na kwenye stendi za dala dala si risasi zingekuwa zinarindima kila uchao?

Endeleeni kujitoa fahamu, lkn najua kuwa ndani ya mioyo yenu mnafahamu kuwa SI SAWA. Hata huku kuzomewa ni matokeo ya kuishi vibaya na watu.
 
Askari wa pili anaonekana kumzuia mwenzake asipige risasi juu.

Kama kweli alikuwa hatarini kwanini mwenzake amzuie na kumsihi aache?

Concentration na macho ya askari wote wawili ilikuwa kwa mtuhumiwa.

Hivyo ni wazi hapakuwepo na hatari yeyote kwa askari hao na kwa ushahidi mwingine yule askari aliwasogelea wale wananchi huku akiongea mbona hakuogopa kuwasogelea wale watu waliokuwa wengi kiasi kile.

*Malima ana makosa pia alipoambiwa mzee ondoka Mara mbili alibakia bado huku akilalamika kwa tendo hilo lazima askari wangekasirika ,Malima pia analo la kujibu.



55135007dcee16dfa8c003b5192fed58.jpg
Lakini tambua kuwa hata yule askar mwingine aliyekuwa anamzuia ilifika wakati naye akalazimika kukoki silaha yake,maana yake ni kuwa hali haikuwa nzuri hapo
 


Mchana huu pamesikika milio ya risasi maeneo ya Masaki karibu na Double tree Hotel.

Yalikuwa ni majibizano kati ya PRE SCAN AUCTION MATT waliokuwa wameambatana na Polisi walipojaribu kukamata gari lilokuwa limeegeshwa pembeni ya barabara hali ya kuwa Dereva yupo ndani.

Inasemekana gari lilikuwa la Mwanae Kighoma Malima aliyeenda IOM kufatilia ishu zake.

Mtu wa Majembe akavamia gari hilo na alipodaiwa kuonyesha vitambulisho aligoma kutoa ndio wananchi walipolizingira gari wakitaka kumpiga wakijua ni jambazi.

Polisi aliingilia kati na katika majibizano akafyatua risasi juu kumtishia ndugu Malima aliyekuwa hana hata silaha wala hakukuwa na mwananchi aliyekuwa na silaha.

Adam Kighoma Malima alikuwa mbunge wa jimbo la Mkuranga na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, aliwahi kuwa pia Naibu Waziri wa Fedha enzi za Kikwete. Anatokea katika chama cha CCM.

====

UPDATES:

Adam Malima afikishwa Mahakamani kwa Kumzuia Askari kufanya kazi yake. Habari zaidi soma=>News Alert: - Adam Malima afikishwa Mahakama ya Kisutu na kusomewa shtaka la 'Kumzuia askari kufanya kazi yake'

Mimi maneno yangu ni yale yale.
Watanzania tuamke na tujue sharia zetu hasa waandishi . wawo ndio wanaweza kuziandika na watu wote kujua.

Tukio lililotokea ingekuwa kama hivi ingekuwaje.
Mzee umepaki gari sipo naomba uondoshe gari yako hapa . nakupa dakika tano .
Dereva kakaidi hataki kuondoka, askari achukuwe plate number halafu aombe leseni ya Dereva, aombe insurance ya Gari. ili ufunguwe mashtaka. Katoa andika kila kitu na kumpa karatasi ya kuja mahakamani.

Kama Dereva hataki kutoa vyote hivyo Askari ita polisi wengine waje kusaidia na kumkamta .

Haina haja ya kutupiana maneno wala kupiga risasi juu.

Safari ndefu tunayo watanzania
 
Mimi maneno yangu ni yale yale.
Watanzania tuamke na tujue sharia zetu hasa waandishi . wawo ndio wanaweza kuziandika na watu wote kujua.

Tukio lililotokea ingekuwa kama hivi ingekuwaje.
Mzee umepaki gari sipo naomba uondoshe gari yako hapa . nakupa dakika tano .
Dereva kakaidi hataki kuondoka, askari achukuwe plate number halafu aombe leseni ya Dereva, aombe insurance ya Gari. ili ufunguwe mashtaka. Katoa andika kila kitu na kumpa karatasi ya kuja mahakamani.

Kama Dereva hataki kutoa vyote hivyo Askari ita polisi wengine waje kusaidia na kumkamta .

Haina haja ya kutupiana maneno wala kupiga risasi juu.

Safari ndefu tunayo watanzania
Inaonesha kijana uwezo wako wa kufikiri bado ni mdogo! Kuna msemo unasema; TII SHERIA BILA SHURUTI. Malima angetii amri na kumwambia dereva wake aondoa gari pale alipo park unadhani haya yaliyotokea yangejitokea? Mbona tunakuwa wepesi wa kulaumu tena upande mmoja?
Pindi walivyouawa wale askari wa 8 kuna wajinga baahdi humuhumu kwenye mitandao walikuwa wanafurahia, Ila waungwana wakawa wanawauliza; wangekuwa ndugu zenu Ungefurahia!?..
Enzi ya kubembelezana ya Mzee bure ilishaisha. Vijana mjitambue, sio kuishia kulaumu tu, mnapoteza muda wa fikra chanya. Sisemi kwamba askari polisi eti wapo perfect kwa 100%, 100% hapana. Ila kwa hili mh. Malina kachemka.

Sent from my TECNO-L5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom