Mashindano ya Draft - Ronaldo Awa Bingwa Kwa Kumfunga Issa Mamba

Mashindano ya Draft - Ronaldo Awa Bingwa Kwa Kumfunga Issa Mamba

Umenikumbusha kitambo sana...

Halafu huu mchezo sijui upo vp, at least kwa upande wangu!!!

Enzi hizo ilikuwa nikicheza na watu wengine, ilikuwa wafanye kazi hasa... in short, mara nyingi kama sio zote nilikuwa najihakikishia ubingwa!!!

Kinyume chake, kulikuwa na Side Boy (RIP) na West... hawa walikuwa washikaji zangu wakubwa, tangu tukiwa vijana wadogo hadi kesho!!

Hawa wadudu, wote wawili, walikuwa wananisumbua sana...

Ingawaje kwa wengine walikuwa wanapigwa, nikikutana nao lazima wanitoe nishai, ama droo za kumwaga!!

Sijui walikuwa wananipatia wapi hawa, sema dah, games zetu zilikuwa zinavuta watu hasa!!

Hapo kwa hao jamaa zako ni kwamba miguu yako yote wanaijua, na wanakuwa wanaweza ku-predict move zako kwa sababu ya kucheza muda mrefu na wewe.

Hata hawa mabingwa huwa wakikutana wa kambi moja utaona sare zinakuwa nyingi sana kwa sababu copy zao zote wanazo (wanajuana).

Na Bingwa akifungwa mchezo fulani atatafuta mtu wa kumwelekeza jinsi ya kutoa sare au kushinda hiyo game, na unakuta anaanza kutafuta either kutoka kwenye kambi yako au anaenda moja kwa moja kwa mtaalamu Mangwez.
 
Hapo kwa hao jamaa zako ni kwamba miguu yako yote wanaijua, na wanakuwa wanaweza ku-predict move zako kwa sababu ya kucheza muda mrefu na wewe.

Hata hawa mabingwa huwa wakikutana wa kambi moja utaona sare zinakuwa nyingi sana kwa sababu copy zao zote wanazo (wanajuana).

Na Bingwa akifungwa mchezo fulani atatafuta mtu wa kumwelekeza jinsi ya kutoa sare au kushinda hiyo game, na unakuta anaanza kutafuta either kutoka kwenye kambi yako au anaenda moja kwa moja kwa mtaalamu Mangwez.
SURE... manake hata mnapokuwa wawili tu, wakati hamna pressure yoyote toka wa watu, bado mtakuwa mnacheza hadi anakuwa anakujua nje ndani!!
 
Jana nilipata bahati ya kushuhudia Nusu Fainali pamoja na Fainali ya mashindano ya Draft yaliyofanyika Kinondoni - Manyanya.

Washiriki walikuwa 32, na walioingia nusu ilikuwa:

Ronaldo vs Saia (Spelling sina uhakika sana) Ronaldo alishinda 3 - 1.

Issa Mamba vs Dogo Yassin, Issa Mamba alishinda 3 bila.

Fainali Ronaldo aka (Christian Bela, Scientist, Allien, Field Marshall) akimshinda Issa (Meno ya Mamba) goli 3 kwa 1.

Wao wanasema ilikuwa ni warm up wakisubiria ligi ambayo mshindi ataondoka na kitita cha shilingi milioni 1.

Kwa mara ya kwanza niliweza kuwaona mabingwa ambao nimekuwa nikiwasikia kwenye vijiwe tofauti tofauti vya madraft.

Baadhi yao ni Mangwelele, Nduli, Dogo Sisqo, Dogo Yassin, Bedui (kawa chapombe siku hizi), Chaula, Ronaldo na Issa Mamba.

Nilifurahi sana kumwona Mangwelele, huyu mwamba nimeanza kumsikia miaka kama 10 iliyopita, dah!
hawa bado nawasikia tu sijawahi kuwaona
 
Hongera sana kwa kunipa update kuhusu mchezo wa draft, mm ni mdau mkubwa sana wa mambo hayo, huyo Mangwengwele au Mangwes aliwahi kunifunga michezo 10 bao 10, kiukweli ameshindikana ktk mchezo wa draft ndio maana siku hizi amekuwa refarii tu, huyo na Noel ni hatari, kuna mwingine simsikii cku hiz anaitwa Shaaban Katoto, wana balaa hao, endelea kutupa habari zao kaka
 
Back
Top Bottom