Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mashine za kutotoleshea mayai za kampuni ya mge
sisi kama mge tunaunda mashine za kutotoleshea mayai ya ndege wa aina zote.
Tunaunda mashine zenye kutumia mafuta ya taa au umeme.
Mashine za umeme zipo za aina tatu.
Moja ni inayochukua mayai chini ya mia hamsini,hii unageuza mayai kwa mkono.
Ya pili inachukua mayai zaidi ya mia hamsini mpaka idadi unayotaka,hii unageuza nanualy kwa kutumia handle maalumu.
Ya tatu ni ile inayojiendesha yenyewe,automatic,hii inachukua mayai zaidi ya mia themanini.
Tunapenda wateja wetu waelewe kuwa tunahitaji sana kuwapa bidhaa kwa bei rahisi zaidi ya hapo,lakini tunaogopa kushusha ubora wa bidhaa zetu.
Naamini hakuna kampuni ya kizalendo kwa hapa tanzania kwa sasa ambayo inaunda mashine za kutotoleshea mayai kwa bei ya chini kama mge.
Tunawaomba wateja wetu,wasituombe kupunguziwa bei ya bidhaa zetu kwani hapa tumepunguza sana.
Kabla ya kuja kwetu uulizia makampuni mengine wanauzaje,sio kukurupuka tu badala ya kufanya utafiti.
Mfano,mteja mmoja alihitaji automstic ya mayai mia tatu,nikamwambia ni milioni moja na laki mbili,akasema ni gharama kubwa sana,akaniambia watu wa kenya wanauza zao supermarket,ya mayai 1400,wanauza milioni sita na laki sita.
Nilishangaa sana,kwani sisi tunauza ya mayai 2000 kwa milioni nne na nusu,na tunauza na backup.
Hapo nadhani wasomaji mtafahamu yupi bei yake iko chini kati ya wakenya na sisi mge.
Pia napenda kutoa tahadhari,sio vizuri sana kuomba kupunguziwa bei kwani unaweza kusababisha utengenezewe kitu chenye thamani ya pesa yako. Angalieni bidhaa za kichina,samsung galaxnote3,inauzwa sabini elfu au laki moja,je original insuzwa hivyo?
Hatutaki wateja wetu wapate bidhaa hafifu zisizodumu,tunataka wateja wetu wakinunua bidhaa zetu warudishe asante na pongezi nyingi sana kwetu.
Hatutaki leo wachukue baada ya siku mbili wapige simu za matatizo.
Huu ni mwaka wa saba nashukuru hakuna malalamiko kwa bidhaa za mge.
Karibuni wote na nsiokuwa na mayai tutawaunganisha na wauzaji wa mayai aina zote.
Piga simu.0784413039.
Mwankole,mashine zetu ni rahisi sana kuzitumia,bada ya nusu saa unakuwa tayari unaweza kuitumia.
Kuhusu umeme zinatumia umeme kidogo sana,ni kama friji,feni au tv
mashine hazizidi wati mia sita.
Umeme ukikatika kwa muda wa masaa manawili hakuna madhara ktk mayai,ila zaidi ya masaa hayo mayai yanaharibika.
Njia ya uhakika ni kuwa na jenereta au solar.au vinginevyo utumie ya mafurmta ya taa.
Karibu sana ndugu zangu.